Friday, June 30, 2017

CHANZO CHA MIMBA KUHARIBIKA NA DALILI ZAKE

HABARI ZENU WADAU!!

LEO NATAKA NIZUNGUMZIE
CHANZO CHA KUHARIBIKA KWA MIMBA MARA KWA MARA

KUHARIBIKA kwa MIMBA ni TATIZO linalowapata WANAWAKE wengi.

Si TATIZO linalowapata WANAWAKE MASIKINI TU ,hata MATAJIRI linawakumba.

MIMBA hutoka ikifikisha WIKI 36 hadi WIKI 38 wakati MTOTO anakuwa karibu KUZALIWA.

WENGI wenye MATATIZO haya wamekuwa wakitafuta MATIBABU hospitalini, kwenye MAOMBI maalum na hata kwa WAGANGA wa KIENYEJI .

SABABU za MIMBA kuharibika mara kwa mara KITAALAM hazijulikani ila kuna VYANZO vinavyojulikana kusaidia MIMBA kutoka.

Mbali na MIMBA zinazotolewa KIHARAMU, sababu za MIMBA zinazotoka bila kulazimishwa zinatajwa kuwa ni MAUMBILE ya KURITHI kwa maana ya kuwa na VINASABA ambavyo si vya KAWAIDA na kwa hiyo KIUMBE kinakuwa katika HALI ambayo KWA ASILI MIMBA haiwezi KUKUA na kama itakua na MTOTO kuzaliwa basi MTOTO huyo atakuwa na MATATIZO ya AJABU ya KIMAUMBILE na AKILI. Ni kwa SABABU hiyo MIMBA huharibika na kutoka yenyewe.

SABABU ya PILI ni KUTOKUA kwa YAI lililorutubishwa. Katika UUMBAJI.

YAI hukutana na MBEGU ya MWANAUME na MCHAKATO wa KIUMBE kukua huanza kwa YAI KUJITENGA mara MBILI .
UPANDE mmoja hutengeneza KONDO la NYUMA na KIFUKO cha kutunza MAJI na SEHEMU ya PILI hutengeneza KIUMBE au MTOTO .
HAPA hutokea SEHEMU ya KONDO la NYUMA ikiendelea KUKUA wakati SEHEMU ya MTOTO HAIKUI kabisa.

Katika MAZINGIRA kama haya,kama MAMA hajafanya VIPIMO vinavyoweza KUANGALIA moja kwa moja, anaweza kuendelea KUJIDANGANYA kama ni MJAMZITO kwani KIPIMO cha MKOJO kinaweza kuendelea KUONYESHA kuwa MAMA ni MJAMZITO.
Hata hivyo bado UJAUZITO utapotea kabla ya WIKI ya 24.

UVUTAJI wa SIGARA na UNYWAJI wa POMBE kupita KIASI wakati wa UJAUZITO huchangia MIMBA kuharibika.

Vilevile MSONGO wa MAWAZO na UKOSEFU wa LISHE huchangia kwa kiasi KIKUBWA UHARIBIKAJI wa UJAUZITO .

MAGONJWA yanayoathiri MWILI wa MAMA TUMBONI kama vile MALARIA , KASWENDE , na kadhalika.

DALILI za MIMBA KUHARIBIKA zinaanza na MJAMZITO kutokwa na MATONE ya DAMU na kupata MAUMIVU ya TUMBO chini ya KITOVU .

WAJAWAZITO wengine wanaweza KUTOKWA na DAMU bila KUHISI MAUMIVU ya TUMBO kabisa.

ASILIMIA kubwa ya MIMBA kuharibika hutokea katika KIPINDI cha AWALI kabisa cha UJAUZITO au NDANI ya WIKI 14 za UJAUZITO .

WANAWAKE wengi aidha kwa UELEWA MDOGO au DHARAU, hupuuza DALILI za KUTOKWA DAMU hasa kama ni KIDOGO huchelewa kwenda kumuona DAKTARI na MATOKEO yake MIMBA huharibika wakati ingeweza KUZUILIKA .

Iwapo MIMBA zinatoka bila KUWA na SABABU inayojulikana unatakiwa ufanyiwe UCHUNGUZI wa MAGONJWA ya KURITHI na MAGONJWA mengine yanayosabaisha MIMBA kuharibika.

ENDELEA KUWA NAMI MAKALA IJAYO TUTAJUA JINSI YA KUFANYA ILI MIMBA ISIHARIBIKE

Tuesday, June 27, 2017

UGONJWA WA MOYO [CORONARY HEART DISEASE]

HABARI ZENU WADAU WA MAKALA ZANGU ?

Leo nimeona nikushirikishe kuhusu
UGONJWA WA MOYO ( Coronary heart disease )

MAGONJWA ya MOYO yamezidi sana siku hizi.
Tatizo hili huanza katika MISHIPA ya DAMU ,na huweza kuendelea mpaka kuanza kuziba MISHIPA hiyo.Hii hufuatiwa na MOYO kukosa HEWA safi (Oxygen) kwa kiasi kinachotakiwa kwa sababu MISHIPA ya kupitisha DAMU imeziba na DAMU ndiyo inayopeleka HEWA ya OKSIJENI kwenye MOYO .

TAFITI mbalimbali zinaonyesha UGONJWA wa MOYO huanza kumwandama MTU pale MAMBO fulani yanaposababisha sehemu ya ndani ya KUTA za MISHIPA ya DAMU kuharibiwa.
MAMBO hayo fulani ni pamoja na kuwepo kiwango KIKUBWA cha aina fulani cha  MAFUTA pamoja na LEHEMU katika DAMU.

CHANZO kingine KIKUBWA ni kutozingatia utaratibu BORA wa ULAJI .Hii ni moja ya MAMBO yanayoongeza uwezekano wa MTU kupata MAGONJWA ya MOYO .

Mfano ULAJI wa VYAKULA vyenye MAFUTA mengi, VYAKULA vyenye SUKARI nyingi, CHUMVI nyingi na LEHEMU nyingi.
Wakati huo ULAJI wa MBOGAMBOGA na MATUNDA ukiwa ni wa KIWANGO cha CHINI.
Pia kuwa na UZITO uliozidi nalo ni TATIZO linaloweza kukusababishia UGONJWA wa MOYO.
Pia UVUTAJI wa SIGARA au UTUMIAJI tumbaku.
Kutofanya MAZOEZI kila siku japo nusu saa SHINIKIZO kubwa la DAMU (high blood pressure),UGONJWA wa KISUKARI na kadhalika.

LEHEMU inahitajika MWILINI lakini kwa kiasi KIDOGO .Hata  hivyo huwezi kujua una LEHEMU nyingi kupita kiasi MWILINI mpaka upime (inatakiwa iwe chini ya 200mg/dl).

Kiasi KIKUBWA cha LEHEMU mwilini husababisha mkusanyiko wa MAFUTA katika MISHIPA ya DAMU.

Punguza HATARI hii kwa kupunguza utumiaji wa MAFUTA yanayotokana na WANYAMA ikiwa ni pamoja na NYAMA iliyonona (nyama ya mafuta),MAZIWA yenye MAFUTA mengi (whole milk),JIBINI (cheese),NGOZI ya KUKU na SIAGI .

Pia ni VIZURI kupunguza ULAJI wa MAYAI , NYAMA (isizidi nusu kilo kwa wiki),MAFUTA tumia kwa kiasi kidogo.
Ongeza MATUMIZI ya NAFAKA hasa zile ZISIZONG'ARISHWA ( whole grains ) kama UNGA wa DONA na kadhalika. ONGEZA pia MATUMIZI ya aina za VYAKULA jamii ya kunde,maharage,mbogamboga na matunda.

Fanya MAZOEZI japo dakika 30 kila SIKU .
Epuka MATUMIZI ya POMBE kupita kiasi pamoja na UVUTAJI wa sigara/tumbaku kwani VITU hivi vina MADHARA katika MOYO na MISHIPA ya DAMU .
Epuka HASIRA ,shinikizo la AKILI na SONONA .

KIUJUMLA ,wingi wa LEHEMU unakadiriwa kusababisha VIFO vya WATU takribani MILIONI 2.6 DUNIANI kila MWAKA.

Kuwepo kwa SUKARI nyingi katika DAMU ,husababisha UGONJWA wa KISUKARI ,ambao unamweka MTU katika HATARI ya kupata UGONJWA wa MOYO au KUPOOZA/KIHARUSI (stroke) mara MBILI zaidi ya ASIYE na KISUKARI .

Kumbuka UGONJWA wa MOYO huweza kumpata MTU yeyote bila kujali UMRI ,na katika siku za karibuni mtindo wa MAISHA umewafanya WATU wengi kupata MARADHI haya kutokana na ULAJI holela wa MLO usiozingatia AFYA na kuacha kufanya MAZOEZI .

Monday, June 26, 2017

TATIZO LA UVIMBE KWENYE KIZAZI KWA WANAWAKE NA TIBA YAKE

TATIZO LA UVIMBE  KWENYE KIZAZI (FIBROID) NA TIBA YAKE !!

Siku hizi kuna ongezeko kubwa sana la huu ugonjwa hebu tega sikio.
Fibroid ni uvimbe ambao hutokea kwenye tumbo la kizazi ambao huu uvimbe unaweza kuwa ndani ya kizazi(ukutani mwa kizazi) au ndani ya nyama ya kizazi na nje kwenye ukuta wa kizazi.

Kuna aina kuuzifuatazo za fibroids:

1.Submucosal fibroids(ndani ya kizazi)
2.intramural fibroid(ndani ya nyama za kizazi)
3. Subserosal(nje ya kizaz)

Watu wafuatao wako hatarini ya kupata ugonjwa huu fibroids

1.Mwanamke ambae hajawahi kupata mtoto mpaka umri mkubwa
2.miaka kuanzia kubarehe mpaka hedhi kukoma
3.kurithi 4.unene 5.kuingia hedhi mapema

Fibroids sio kansa ni uvimbe wa kawaida tu ambao unakua kwa kutegemea kichocheo cha estrogen hormone ndio maana kuanzia kubarehe mpaka kukoma kwa hedhi ndio wako hatarini. Na mara nyingi uvimbe huu waga unaongezeka kukua sana hasa wakati wa ujauzito kwani vichocheo hivi huongezeka wakati huu kulinda makazi ya mtoto.
Ni watu waliofikia kikomo cha hedhi hawapati fibroids au kitaalam leomyoma.

Dalili za fibroids

1.Kutokwa damu kwenye via vya uzazi katikati ya mwezi.
2.kutokwa na uchafu wenye kiaharufu mbaya au ambao hauna harufu lkn mwingi na mweupe.
3.maumivi ya kiuno hasa wakati wa hedthi ambayo husababishwa na kizazi kujaribu kusukuma huo uvimbe..wengi hupata maumivu makali sana.
4.Tumbo kuuma sana chini ya kitovu.
5.hedhi zisizokuwa na mpango
6.maumivu wakati wa tendo la ndoa
7.Kukosa hamu ya tendo la ndoa
8.maumivu makali wakati wa hedhi

Uvimbe unapokua mkubwa unaweza kusababisha dalili zifuatazo.

1.Kukojoa mara kwa mara kwani uvimbe unakandamiza kibofu cha mkojo
2.Mkojo kubaki kwenye kibofu cha mkojo
3.Haja kuwa ngumu
4.miguu kuvimba
5.kupungukiwa damu

Jinsi fibroids zinavyoweza kuzuia kupata mtoto:

1.Fibriods zikikua sana zinakandamiza mishipa ya kupitisha mayai kutoka kwenye kiwanda yan ovari
2.Uvimbe pia unazuia yai lililorutubishwa kujishikiza kwenye kizazi..hasa submucosal fibroids
3.Pia husuia mfuko wa kizazi kukaza kusukuma mbegu kwenda kwenye mishipa ya kupitisha mayai.

MATIBABU

1.Wanawake wengi wanafibroids ndogo ndogo lakini kwa sababu hazina dalili hahawezi kwenda hospitali na hawa ndo sku wakibeba ujauzito uvimbe unaongexeka coz ya vichocheo kuongezeka hvyo hawa watu tunawabaini tunapofanya ultrasoudi ndipo wanakutwa navyo.lkn kitaamu hospitali hawatibu uvimbe wa namna hii

2.Uvimbe ambao ni mkubwa wenyewe hutibiwa kwa namna zifuatazo (hospital)

A.Dawa ambazo ni gharama sana mfano donazol wengi masikini hawawez kumudu kununua
B.Vidonge vya maumivu

C.Vidonge vya kuzuia damu km tranexamic acid na dawa za uzazi wa mpango(COCs)

2.Njia ya pili ni operation nazo zipo operation aina nyingi inategemea na uvimbe ukubwa na wingi wake.
1.Myomectomy hii ni operation ya kuondoa uvimbe mmoja mmoja bila kuondoa kizazi kwa wale wenye uvimbe mmoja uko sehemu nzuri
2.Total abdominal hysterectomy. Hii operation unaondoa kizazi chote kama uvimbe umekaa vibaya na viko vingi.
Swali la kujiuliza kwa nini mpaka upate dalili ndo utaanza kushughulikiwa kutibiwa???? Kwa nini ubebe ujauzito huku una uvimbe kisa bado mdogo???
Kumbuka uvimbe huu sio kansa hvyo ondoa hofu. Mbali na donazole ambayo ni ya gharama na haishauliwi itumiwe kwa mda mrefu ina sababisha mwanamke anakua na sifa za kiume.UKIFANYIWA OPERATION USIDHANI UVIMBE UMEISHA UNAOTA PEMBENI HADI UTAKAPOWEKA VICHOCHEO SAWA.

**AFYA NDIO KILA KITU**

Sunday, June 25, 2017

UFAHAMU UGONJWA WA FIGO (SABABU NA JINSI YA KUJIKINGA)

HABARI ZENU WADAU WA MAKALA ZANGU..?

LEO nimeona ni VYEMA nikushirikishe kuhusu CHANGAMOTO ya UGONJWA wa FIGO.

FIGO ni OGANI inayoshirikiana na MOYO. KUATHIRIKA kwake kuna ATHARI KUBWA kwa MFUMO wa DAMU na MAPIGO ya MOYO.

MAGONJWA SUGU ya FIGO hutokea pale OGANI hiyo inapopoteza UWEZO wa kutenda KAZI zake kikamilifu.

TATIZO huanza TARATIBU na KUDUMU kwa MUDA mrefu hadi kuonyesha DALILI za WAZI .
HUU ni kati ya MAGONJWA yasiyoambukiza kwani UNATOKANA na MIENENDO na MITINDO ya KIMAISHA .

FIGO huwa na KAZI ya kuchuja TAKAMWILI zilizo NDANI MWILINI na kuzitoa NJE kwa NJIA ya MKOJO na KUPUNGUZA kiasi cha MAJI kilichozidi MWILINI.

FIGO hutoa HOMONI inayochochea OGANI zingine MWILINI ikiwamo KUHAMASISHA utengenezwaji wa CHEMBE NYEKUNDU za DAMU,utendaji wa MADINI ya KALSIAMU na HOMONI zinazoongeza MWENDO KASI wa MISULI ya MOYO.

Vilevile ,FIGO hufanya KAZI ya KUFYONZA na KUVIRUDISHA vitu MUHIMU ambavyo vingehitajika kutoka kwa NJIA ya MKOJO.

Hudhibiti MADINI kama POTASIUMU,MAGNESIUMU,na TINDIKALI ili kuweka sawa MAZINGIRA sawia katika DAMU.

FIGO inapopoteza UWEZO wake wa kutenda KAZI husababisha KUKOSEKANA kwa UFANISI wa SHUGHULI za MWILI.
HALI hii husababisha KUWAPO kwa KUSANYIKO na LIMBIKIZO la MAJI,UCHAFU na SUMU hutokea MWILINI mwa MGONJWA.

Pia husababisha KUTOKEA kwa MARADHI mengine kama vile, UPUNGUFU wa DAMU MWILINI, SHINIKIZO la DAMU na ONGEZEKO la TINDIKALI kwenye DAMU.

Vilevile husababisha ONGEZEKO la LEHEMU na MAFUTA kwenye DAMU na MAGONJWA ya MIFUPA.

INAELEZWA kuwa karibu WATU nusu MILIONI wapo katika UCHUJAJI DAMU na MASHINE MBADALA wa FIGO ( dialysis ) na huku WAKIWA wameshawahi kubadilishiwa FIGO.

MAMBO kadhaa YANAHUSISHWA na TATIZO la UGONJWA SUGU wa FIGO ikiwamo UGONJWA wa KISUKARI, SHINIKIZO LA DAMU,UNENE ULIOPITILIZA na UZEE.

Vilevile MABADILIKO katika TABIA na namna WATU wanavyohishi.

Ili KUJIEPUSHA na HATARI ya kupata UGONJWA wa FIGO fanya yafuatayo.

1.USICHELEWE kwenda HAJA.

Kutunza MKOJO kweye KIBOFU chako  kwa muda MREFU ni WAZO BAYA.KIBOFU kikijaa kinaweza kusababisha uharibifu.  
MKOJO ambao unakaa kwenye KIBOFU  huzidisha BAKTERIA haraka.
Pia MKOJO unaporudi NYUMA ya NJIA husababisha  MAAMBUKIZI katika FIGO pia NJIA ya mkojo "nephritis", pamoja na "uremia".
Wakati WITO ASILI (unahisi mkojo) fanya haraka iwezekanavyo nenda KAKOJOE .

2.Kula CHUMVI kupita kiasi nalo ni TATIZO.

Inatupasa kula Chumvi isiyozidi 5.8 gramu kwa SIKU .

3.Kula NYAMA kupita kiasi.

PROTINI ikizidi sana katika MLO wako inadhuru FIGO zako. MMENG'ENYO wa PROTINI unazalisha AMONIA-  SUMU DUTU ambayo ina UHARIBIFU mkubwa kwa FIGO zako. NYAMA nyingi  inaleta UHARIBIFU zaidi wa FIGO.

4.UNYWAJI mwingi wa "CAFFEINES".

CAFFEINE hutokana na VINYWAJI vya SODA na VINYWAJI vingine LAINI kama KAHAWA, RED BULL n.k.                              Hupandisha SHINIKIZO la DAMU na FIGO zako kuanza kupata MATESO .
Unapaswa KUPUNGUZA kiwango  cha COKE, PEPSI, RED BULL, nk. ambavyo HUNYWA kila SIKU.

5.PIA Kutokunywa MAJI.

FIGO zetu LAZIMA zichakatwe VIZURI kutekeleza MAJUKUMU yake VIZURI .                       

Endapo HATUNYWI MAJI ya KUTOSHA , SUMU DUTU inaweza kuanza KUKUSANYIKA katika DAMU , kama hakuna KIMIMINIKA cha  KUTOSHA kutoa kwa NJIA ya FIGO .                        KUNYWA zaidi ya BILAURI 10 za MAJI kila SIKU.

Kuna NJIA RAHISI ya KUANGALIA kama  unakunywa MAJI ya KUTOSHA nayo ni kuangalia RANGI ya MKOJO wako,WEPESI wa RANGI ndiyo VIZURI.

6.PIA Kuchelewa MATIBABU .


Pia EPUKA VIDONGE hivi ni HATARI sana:-

D- baridi.
Vicks Action- 500
Actified
Coldarin
Cosome
Nice
Nimulid
Cetrizet- D

Hivi VIDONGE vina Phenyl propanol- amide PPA ambayo husababisha STROKE na zimepigwa MARUFUKU huko MAREKANI.

NAMALIZIA kwa KUKUPATIA MAONYO MUHIMU ya AFYA

1. JIBU (pokea) SIMU WITO na SIKIO  la KUSHOTO.
2. Usinywe  DAWA kwa MAJI BARIDI.
3. Usile MILO MIZITO baada ya SAA KUMI na MOJA JIONI .
4. Kunywa MAJI VUGUVUGU mengi ASUBUHI na kiasi USIKU . Usinywe MAJI BARIDI KAMWE .
5. MUDA BORA wa KULALA ni kutoka SAA NNE usiku hadi SAA KUMI alfajiri.
6. USILALE mapema BAADA ya KUMEZA DAWA au BAADA ya MLO wa USIKU, Kula CHAKULA laini.
7. Usipokee SIMU yako ikiwa HAINA CHAJI kwani WAKATI huo MIONZI huwa ina NGUVU mara 1000 .

Saturday, June 24, 2017

TATIZO LA KUNUKA MDOMO NA JINSI YA KUJILINDA

TATIZO KA KUNUKA MDOMO

Kuwa na harufu mbaya mdomoni ni kitendo kinachoweza kuathiri maisha ya mtu kimahusiano si kwa mpenzi tu bali marafiki na jamii kwa ujumla.
Pia kuwa na harufu mbaya mdomoni hupunguza mtu kuwa lovable kwani hata unapoongea wengi watakwepa kuongea direct na wewe kwa sababu ya harufu mbaya inayotoka mdomoni.
Kile unakula kina affect hewa unayotoa iwe mdomoni au sehemu nyingine. Na baadhi ya vyakula vina matokeo mabaya sana kwa hurufu unayotoa mdomoni.

Harufu mbaya mdomoni si ugonjwa wa kuambukiza haina haja kuogopa ukikutana na mtu mwenye harufu mbaya mdomoni kwamba atakuambukiza.

Pia tatizo kubwa ni kwamba watu wenye harufu mbaya mdomoni hawajijui kwamba wana harufu mbaya.
Asilimia 85 – 90% ya tatizo la harufu mbaya mdomoni asili yake ni kinywa chenyewe. Pia kiwango cha harufu hutofautiana kutokana na muda (mchana, usiku na asubuhi).
Harufu nyingi mbaya mdomoni hutokana na vyakula vyenye asilia ya protein.
Kuna zaidi ya aina 600 ya bacteria wanaoishi kwenye kinywa cha Binadamu (sehemu ya juu ya ulimi, fizi na kuzunguka meno).

NINI HUSABABISHA KUWA NA HARUFU MBAYA MDOMONI

Kutokuwa makini na usafi wa kinywa kama vile kupiga mswaki vizuri kunakoacha mabaki ya chakula ambayo huoza na kusababisha harufu mbaya mdomoni.
(Wengi hupiga mswaki haraka haraka na kuacha mabaki ya chakula)
Maambukizi ya magonjwa kama vile fizi kutoka damu, mfumo wa upumuaji na kisukari.
Kinywa kuwa kikavu kutokana na medications
Kuvuta sigara, kunywa kahawa

JINSI YA KUTAMBUA KWAMBA UNA HARUFU MBAYA MDOMONI

Wanasayansi wamekiri kwamba ni ngumu sana mtu kujijua mwenyewe kama ana harufu mbaya kwa sababu ya mazoea (habituation).
Ni rahisi sana kutambua harufu kutoka kwenye kinywa cha mtu mwingine.
Unaweza kutambua kama una harufu mbaya mdomoni kwa kumuuliza mtu unayemuamini.
Pia unaweza kujua harufu mbaya kwa kulamba nyuma ya kiganja na kunusa, wengine hupumua mbele ya kioo na kunusa.
Pia unaweza kutumia kijiti cha kuchokonolea meno na kukinusa.
Kisayansi unaweza kutumia vifaa kama Halimeter, Gas Chromatography na BANA Test.

JINSI YA KUJILINDA NA HARUFU MBAYA MDOMONI (TIBA)

Kula vyakula vyenye afya na pia kula vyakula ambavyo wakati unakula vinaweza kusafisha kinywa vizuri.
Kusafisha meno mara mbili kwa siku asubuhi na baada ya mlo wa usiku, unashauriwa kutumia tongue cleaner kusafisha ulimi.
Tumia chewing gum ambazo husaidia kuongeza kiasi cha mate kwenye kimywa kilichokauka. Baadhi ya gums zina viungo vinavyoondoa harufu mbaya mdomoni na zingine husafisha kinywa na bacteria wanaosababisha harufu mbaya.
Tumia dawa ya kusukutua mdomoni (mouthwash) kabla ya kulala usiku.
Kuwa makini na afya ya kichwa chako kama vile kupiga mswaki vizuri, kuondoa mabaki ya vyakula kwenye meno na kumuona daktari kila unapoona una Matatizo ya meno au kinywa.
Kuhakikisha unakunywa maji ya kutosha kila siku angalau glass mbili za maji.
Mwone daktari wako ukiona una tatizo la harufu mbaya mdomoni.

Tuesday, June 20, 2017

UJUE UGONJWA WA KISUKARI NA JINSI YA KUJIKINGA

UJUE UGONJWA WA KISUKARI (Diabetes)
Kisukari ni ugonjwa unaotokana na mtu kuwa na sukari nyingi kupita kiasi kwenye damu. Ugonjwa huo huvuruga utaratibu wa kuingiza sukari ndani ya chembe kutoka kwenye damu kwa kuwa chembe huhitaji sukari ili kupata nishati.
Ugonjwa wa Kisukari hutokea pale ambapo tezi ya kongosho inaposhindwa kutengeneza kichocheo (Homoni) aina ya insulin au pale mwili unaposhindwa kutumia vizuri kichocheo hicho na kusababisha kuongezeka kwa sukari (Hyperglycemia) au kushuka kwa kiwango cha sukari (Hypoglycemia). Ugonjwa wa kisukari unaweza kusababishwa na kuwa na kiwango kidogo cha insulin mwilini, mwili kutosikia kichocheo hicho au yote mawili

KISUKARI NI NINI HASWA?
Sukari mwilini hutokana na vyakula pamoja na vinywaji tunavyotumia kila siku na hutumika kuupa mwili nguvu. Glukosi ni aina ya sukari ambayo huzipa chembe za mwili nishati. Hata hivyo ili glukosi iingie ndani ya chembe hizo inahitaji insulini. Insulini ni kemikali (Homoni) ambayo hutokezwa na kongosho (Pancrease).

NINI CHANZO HASA CHA KISUKARI?

Ili kuelewa vyema ugonjwa wa kisukari ni muhimu kwanza kuelewa namna chakula kinavyovunjwa vunjwa na kutumiwa na mwili ili kuzalisha nguvu. Wakati chakula kinapoyeyushwa matukio kadhaa hutokea. Moja ni sukari inayoitwa glucosi ambayo ni chanzo cha nishati/nguvu mwilini huingia katika damu. Tukio la pili ni kiungo kinachoitwa kongosho (Pancrease) kutengeneza kichocheo cha insulini. Kazi ya insulini ni kuondoa glucosi katika damu na kuingiza katika misuli, seli za mafuta na ini, ambako hutumika kama nishati.
Watu wenye kisukari huwa na kiwango kikubwa cha sukari kwenye damu kuliko inavyotakiwa kwa sababu miili yao haiwezi kupeleka sukari kwenye seli za mafuta, ini na misuli ili ihifadhiwe kwa ajili ya kuzalisha nguvu. Hii ni kutokana na moja ya sababu zifuatazo, huenda kongosho zao haziwezi kutengeneza insulini ya kutosha au seli za mwili wao haziathiriwi na insini kama inavyotakiwa au sababu zote hizo mbili.
DALILI ZA UGONJWA WA KISUKARI
Kama wewe ni mnene kupita kiasi, hufanyi mazoezi kwa ukawaida au una watu wa ukoo walio na kisukari, huenda tayari una kiwango cha juu cha sukari kwenye damu. Ongezeko la sukari kwenye damu mbali na kuwa kisababishi cha kisukari, hali hiyo inahusianishwa na hatari ya kupatwa na ugonjwa wa akili uitwao 'DEMENTIA'.

Kula sukari nyingi sio sababu ya ugonjwa wa kisukari. Lakini lazima tuseme kwamba kula sukari nyingi si nzuri kwa afya yako kwani utaongeza uzito wa kuweza kuathiri uwezo wa mwili wako kujikinga na maradhi tofauti. Ugonjwa wa kisukari umeitwa kwa kufaa "ugonjwa unaoathiri kiini cha nishati ya mwili". Mwili unaposhindwa kutumia glukosi, mifumo mbalimbali ya mwili inaweza kuacha kufanya kazi au hata kusababisha kifo
Ugonjwa wa Kisukari kitaalamu hujulikana kama 'DIABETES MELLITUS'. Jina 'Diabetes Mellitus' linatokana na neno la Kigiriki linalomaanisha 'kunyonya' na neno la Kilatini linalomaanisha 'tamu kama asali'. Maneno hayo yanafafanua vizuri sana ugonjwa huo, kwani maji hupita mwilini mwa mtu aliye na ugonjwa wa kisukari kana kwamba yananyonywa na mdomo na kupitia kwenye njia ya mkojo kisha kutoka nje ya mwili. Isitoshe mkojo huwa na ladha tamu kwa kuwa una sukari.
Nyingine ni ngozi kuwa kavu na kuwasha, mgonjwa kupoteza uzito bila sababu, kuwa na ukungu machoni, kuchoka kusiko kwa kawaida, hisia kupungua katika vidole na viganja
mikononi na miguuni na kuwa na ukungu katika fizi, ngozi na kibofu cha mkojo.
NI NANI ANAWEZA KUWA NA UGONJWA WA KISUKARI?
Watu walio katika makundi yafuatayo wana uwezekano mkubwa wa kupata ugonjwa wa kisukari:
 Wenye uzito uliozidi
 Wenye historia ya kuwa na wagonjwa wa kisukari katika familia zao,
  Wanawake waliozaa watoto wenye kilo 4 au zaidi,
 Watu wasiojishughirisha au wasiofanya mazoezi,
  Wenye shinikizo la damu,
  Wenye msongo wa mawazo na
  Wenye matumizi makubwa ya pombe na sigara
 Watu hawa wanashauriwa kupima sukari yao kila mwaka wakiwa na umri wa miaka 45 na kuendelea.
Kuna hatari kubwa ya kuugua ugonjwa huo ikiwa mtu ana mafuta mengi katika tumbo na kiuno chake kuliko katika mapaja yake. Mafuta katika kongosho na ini huvuruga uwezo wa mwili wa kudhibiti kiasi cha sukari kwenye damu.
Wavutaji wa sigara wanakabiliwa na hatari kubwa zaidi kwani zoea hilo hudhuru moyo na mfumo wa mzunguko wa damu na kubana mishipa ya damu. Kitabu kimoja kinasema kwamba asilimia 95 ya watu wanaougua kisukari ambao hulazimika kukatwa viungo ni wavutaji wa sigara.

DALILI ZA UGONJWA WA KISUKARI
  Kunywa maji mengi kuliko kawaida na kusikia kiu kila wakati
  Kwenda haja ndogo mara kwa mara. Watoto kukojoa kitandani
  Kuwa dhaifu, kukosa nguvu na kujisikia mchovu kila wakati.
  Kupungua uzito au kukonda licha ya kula vizuri.
  Kusikia njaa kila wakati na kula sana.
  Wanawake kuwashwa ukeni.
  Kutoona vizuri.
  Kupungua nguvu za kiume au hamu ya kujamiiana kwa wanawake.
  Ganzi, kuchomwachomwa au kutohisi unapoguswa sehemu za miguu, viganja na vidole
  Miguu kuoza na hata kupata gangrini.
  Kukaukwa na ngozi na pia kupata aina ya ganzi katika miguu.
  Vidonda au majeraha sehemu yoyote ya mwili kutopona haraka.
  Majipu mwilini.

Wenye dalili hizi wanashauriwa kupima sukari ili kubaini kama wana kisukari.
Watu wenye kisukari wanapaswa kubadili jinsi wanavyokula na kuishi.Ufuatao ni ushauri wa kuwasaidia kufanya mabadiliko:
• Anza na mabadiliko madogo madogo. Kwa mfano, badala ya kuacha utumiaji wa vinywaji vilivyokolezwa sukari mara moja, jaribu kupunguza matumizi ya vinywaji hivyo taratibu. Kupunguza taratibu kiasi cha sukari unayokula au kuongeza kiasi cha mazoezi ni rahisi kutekeleza na kuna uwezekano mkubwa utazoea na kuendelea na utaratibu huo.
• Amua mwenyewe unataka kubadili nini. Weka lengo kama vile kutembea zaidi, kupunguza uvutaji au kutovuta kabisa, au kuweza kucheza na wajukuu zako.
• Tafuta msaada. Familia, marafiki, au watu wengine wenye kisukari wanaweza kukusaidia kufanya mabadiliko.
• Tafuta msaada kwa matatizo ya kisaikolojia. Ni jambo la kawaida kwa watu wenye kisukari kuogopa maisha ya baadaye, kuhuzunika juu ya kuugua mara kwa mara, au kuwa na hasira juu ya mabadiliko yanayohitajika. Hisia za uchungu, huzuni, au kukosa matumaini vinaweza kumzuia mtu mwenye kisukari kufanya mabadiliko ambayo yanahitajika au ambayo anataka kufanya.
• Tafuta sababu zako za kutaka kuwa na afya bora zaidi. Unataka kufanya nini na unataka kujisikia vizuri namna gani? Kwa mfano, fikiria familia yako na kwa nini unataka kuendelea kuishi ukiwa mwenye afya ya kukuwezesha kuwasaidia wanafamilia kwa muda mrefu zaidi.
• Ugonjwa wa kisukari ni tatizo ambalo siku hizi husababishwa na mfumo wa maisha tunayoishi hasa vijana, tafiti zilizowahi kufanywa zinaonesha kuwa vijana wapo kwenye hatari kubwa ya kupata kisukari kwa sababu ya mfumo usio sahihi wa maisha wanayoishi vijana.
• Kutokufanya mazoezi, kukosa muda wa kupumzika na kutokula mlo sahihi,unywaji wa pombe na uvutaji sigara wa kupitiliza, hizi ni sababu chache zinazochangia vijana kuishi katika mfumo wa maisha hatarishi wa kupata maradhi ya kisukari.
Baadhi ya dawa za mitishamba zinaweza kusaidia kucontrol sukari mwilini
Waulize wataalam wa tiba za asili dawa gani za mitishamba zinapatikana katika eneo lako kwa ajili ya kupunguza sukari kwenye damu na kuwa kawaida, njia bora zaidi za kuzitumia, na kama ni salama kuzitumia sambamba na insulini na dawa zingine.
Duniani kote, wataalam wa tiba za asili wamegundua vyakula na dawa za mitishamba ambazo zinaweza kusaidia kupunguza sukari kwenye damu. Ifuatayo ni mifano kadhaa:
• Bitter melon , Mdalasin, Binzari ya manjano, Majani ya mlonge, Uwatu (Fenugreek), Forosadi (Mulberry) , Tangawizi , Nopal (cactus, Bitter leaf , Siki
SHARE UJUMBE HUU KWA NDGU NA MARAFIKI KWA MSAADA WA ELIMU JUU YA UGONJWA HUU

SARATANI YA TEZI DUME(VISABABISHI,DALILI PAMOJA NA JINSI YA KUIEPUKA)

HABARI ZENU WADAU WA MAKALA ZANGU..?

LEO NATAKA NIIZUNGUMZIE CHANGAMOTO YA SARATANI YA TEZI DUME.

SARATANI ya TEZI DUME inashika NAFASI YA TATU kwa kusababisha VIFO vinavyotokana na KANSA kwa WANAUME duniani.

UGONJWA huu ni chanzo kikuu cha VIFO vinavyosababishwa na SARATANI kwa WANAUME wenye UMRI wa kuanzia MIAKA 45 na kuendelea, hata hivyo, SARATANI ya TEZI DUME kwa sasa inawapata sana WANAUME kuanzia MIAKA 25.

Kwa ufahamisho tu ni kwamba NENO SARATANI ni JINA la UGONJWA ambalo hutokea wakati CHEMBE HAI au SELI katika sehemu fulani ya MWILI zinapoanza KUKUA bila kufuata UTARATIBU wa MFUMO WA MWILI na kutengeneza VIJIUVIMBE vidogo vidogo.
Kwa kawaida SELI huwa ZINAJIGAWA, KUPEVUKA na baadaye ZINAKUFA.

UTOKEAJI wa SARATANI ni pale ambapo SELI zilizotakiwa KUFA HAZIFI, zinaendelea KUISHI wakati HUOHUO zile MPYA zinazidi KUZALIWA.

UKWELI ni kwamba WANAUME wote WANAZALIWA na TEZI DUME lakini baada ya BALEHE, TEZI DUME huongezeka UKUBWA mara MBILI.
Na ikifika MIAKA 30 TEZI DUME huanza KUKUA haraka zaidi.Hii ni kwa sababu UKUAJI wa TEZI DUME huenda SAMBAMBA na UMRI.

Kuna VIHATARISHI vingi vinavyochangia MWANAUME kupata SARATANI ya TEZI dume.

Vifuatavyo ni baadhi yake:-

-UMRI. Nafasi ya kupata SARATANI ya TEZI DUME huongezeka sana hasa ukifikia UMRI wa karibu MIAKA 50 na kuendelea.

-NASABA ni kihatarishi kingine ambapo WANAUME wenye HISTORIA ya tatizo hili kwenye FAMILIA ZAO,wale ambao MMOJA WA NDUGU ZAO wamewahi kuugua UGONJWA huu, huwa katika HATARI ya kupata SARATANI hiyo kutokana na KURITHI JENI za UGONJWA huo.

-SUALA jingine ni LISHE ambapo WANAUME wanaopenda KULA NYAMA(red meat) na WALAJI wa CHAKULA chenye kiasi KIKUBWA cha MAFUTA hasa ya WANYAMA, huwa katika HATARI KUBWA ya kupata SARATANI ya TEZI DUME.

-Pia WATAALAM wanatumbia kuwa,WANAUME wasiopenda kufanya MAZOEZI,WANENE na WENYE UPUNGUFU wa VIRUTUBISHO vya VITAMIN E pia wako kwenye HATARI ZAIDI ya kupata SARATANI ya KIBOFU cha MKOJO.

-WANAUME wengine walio katika HATARI KUBWA ya kupata SARATANI ya TEZI DUME ni pamoja na wale wenye ASILI ya AFRIKA(Weusi), ikilinganishwa na WAZUNGU.

-WAKULIMA wanaotumia aina fulani ya MBOLEA za KEMIKALI, wanaofanya KAZI katika VIWANDA vya kutengeneza MATAIRI na WACHIMBAJI MADINI, hususani aina ya cadmium

DALILI ZA SARATANI YA TEZI DUME

Katika HATUA zake za AWALI, dalili za saratani ya TEZI DUME hazitofautiani na zile za KUVIMBA kwa TEZI DUME au BPH. Dalili hizo ni pamoja na:-

1.Kupata SHIDA wakati wa kuanza KUKOJOA.

2.Kutiririka kwa MKOJO baada ya KUMALIZA kukojoa.

3.Kukojoa MKOJO wenye mtiririko DHAIFU.

4.Kukojoa mara kwa mara hasa nyakati za USIKU.

5.KUJIKAKAMUA wakati wa kukojoa na KUSHINDWA kumaliza MKOJO wote.

6.Kutoa MKOJO uliochanganyika na DAMU.

KITAALAM imethibitika kuwa endapo MWANAUME HUYU hasa mwenye MIAKA kuanzia 30 atapata VIRUTUBISHO maalum vya VITAMINI na MADINI anaweza KUEPUKA CHANGAMOTO HII.

WANAUME waliopo HATARINI zaidi ni kuanzia MIAKA 45 na kuendelea. Kwani katika kila WANAUME 6 inakadiriwa kuwa MMOJA atakuwa na SARATANI HII.

Monday, June 19, 2017

ZIFAHAMU AINA KUMI NA MBILI(12) ZA MAUMIVU YA KICHWA NA TIBA ZAKE

AINA KUMI NA MBILI ZA KUUMWA NA KICHWA

Kuumwa na kichwa kumegawanyka sehemu kuu nyingi sana japo kuwa 1% yake ni hashirio la matatizo ya kiafya ambayo yameadvance. Kama vile concussion of brain,meningitis,encephaliti, na stroke. Kuumwa na kichwa pia inawezatokana na matatizo ya taya, meno au hata kula vitu vya baridi zaidi. Vyakula vyenye nitrite au monosodium glutamate.
Sehemu ambazo huuma ni kama ifuatavyo.mfumo wa fahamu ambao upo kwenye fuvu la kichwa.
Baadhi ya neva za fahamu zizlizoko usoni
Misuli ya kichwani
Mishipa inayopatikana kwenye fuvu la kichwana chini ya ubongo kuna mifumo ya fahamu yenye hisia. Kumbuka fuvu na tishuu za ubongo kwa zenyewe haziumi kwani hazna mifumo ya fahamu ambayo inahisia.
Mambo haya 12 nayo yanahusika sana.

1:Nervous tension headaches;

Ni maumivu ya kichwa endelevu upande mmoja au pande zote za misuli ya shingo na upande wa juu wa mgongo,kuumwa na kichwa pamoja na kusinzia. Tumia vitamin b2 na c , punguza au acha matumizi ya sukari,kahawa,chakula chenye kukusababishia mzio,misongo ya mawazo na ufanye mazoezi yakutosha.

2: Cluster headaches

Kichwa kuuma haswa upande mmoja wa kichwa kwa maumivu makali, machozi humtoka mtu na makamasi kwa mbali. Kitu cha kwanza ni kutumia chakula chenye protein ya kutosha, epukana na chakula chenye mzio kwako.

3: Hangover headaches;

Hii ni hali ya kichwa kuuma kwa sababu ya matumizi makubwa ya vinywaji vikali haswa pombe. Weka barafu chini ya kichwa yaani maeneo ya kichogoni au shingoni,kunywa maji mengi na juice ya matunda freshi na uache pombe.

4: Exertion headaches;

Hutokea pale ambapo mwili utatumika sana na haswa kwenye ngono. Weka barafu linalouma, kula mlo kamili na usifanye mazoezi.

5: Caffein headaches;

Hali hii hutokea pale ambapo umeacha matumizi makubwa sana ya kahawa kwa ghafla. Kunywa kiasi kidogo cha kahawa kuondoa maumivu na upunguze matumizi kidogokodogo mpaka utakapo acha kabisa.

6: Sinus headaches;

Maumivu haya huanzia upande wa kulia na kushoto wa pua na kupanda mpaka kichwani. Kula vitamini C kwa wingi na umuone mtaalamu wa afya maana saa zingine hii utkana na maambukizi.

7: Bilious headaches;

Kichwa na macho huuma haswa kipanda uso na husababishwa na kula sana, kula vibaya, kutofanya mazoezi na kukosa choo. Fanya mazoezi na kunywa maji yakutosha na kasha fanya enema.

8: Hunger headaches;

Maumivu ya kichwa ambaya husababishwa na kutokula kwa muda. Kula chochote ilimradi kiwe ni protein au carbohydrates .

9: Eyes ram headaches

Haya ni maumivu yanayotokea kwenye macho na wengi hudhani labda wameangalia vibaya japo saa zingine inaweza kuwa sababu. lakini chanzo chake haswa ni ubongo kufanya kazi kupita kiasi. Badili mtindo wa maisha na kama ni mtumiaji wa miwani ni vyema ukamuana mtaalamu aangalie kama lensi zimepotea nuru au la.

10: Menstrual headaches;

Hali hii hutokea kwa kina mama kipindi cha yai kupevuka. Hutokana na mabadiliko ya hormone, muone mtaalamu wa afya.

11: Arthritis headaches;

Haya ni maumivu ya kichwa yanayosikika mpaka shingoni na saa zingine mpaka mgongoni ambayo husababisha maumivu haswa unapozidisha mwendo au shughuli. Kitu kikubwa ni kutibu ugonjwa unaosababisha hali hiyo.

12: Hypertension headaches;

Ni maumivu ya kichwa chote, mwendo mkubwa pia huongeza maumivu. Hali hii husababishwa na shinikizo la damu. Tibu au pambana kushusha shinikizo la damu na halii itaisha bila shaka.

@Swali lolote comment hapo chini nawe utajibiwa haraka kwa blog yetu

Saturday, June 17, 2017

TATIZO LA UKOSEFU WA NGUVU ZA KIUME NA CHANZO CHAKE

...
LIFAHAMU TATIZO LA #UKOSEFU WA NGUVU ZA #KIUME NA CHANZO CHAKE.

Leo katika zama hizi za sayansi na teknolojia tatizo la kupungua nguvu za kiume limekuwa kubwa sana, siyo Tanzania tu, bali duniani kote. Jambo muhimu analopaswa mwanaume yeyote kufahamu ni kwamba, kupungua nguvu za kiume siyo ugonjwa, ni dalili ya ugonjwa. Hii ina maana kuna dosari au udhaifu wa kiutendaji ndani ya mwili wake. 

Kuna sababu nyingi mno zinazosababisha mwanaume apungue nguvu za kiume. Mtu aweza kujiuliza kwa nini kuwe na sababu nyingi namna hiyo?

Kwani nguvu za kiume ni nini?

Nguvu za kiume ni jina la jumla lenye vipengele vingi ndani yake ikiwa ni pamoja na hamu ya mapenzi; kusimama kwa uume barabara; kuchelewa kufika kileleni kiasi cha kufurahia tendo la ndoa; uwezo wa kurudia tendo la ndoa; pumzi, wepesi na uchangamfu wa mwili katika kutenda tendo  lenyewe.

Ni viungo gani vinavyohusika na nguvu za kiume?

Nguvu za kiume ni tukio pana sana lenye kuhusisha viungo na vitu vingi ndani ya mwili. Kuna zaidi ya viungo na vitu 50 ndani ya mwili wa mwanaume vinavyohusika na nguvu za kiume ambapo viungo hivi pia hufanya kazi zingine za mwili. Baadhi ya viungo hivyo ni ubongo, moyo, mishipa ya neva mishipa ya ateri, mirija iliyo ndani ya uume iitwayo corpora cavernosa.

Viungo vingine ni neva maalumu za parasympathetic, tezidume (prostate gland), ini, figo, homoni ya testestorone, kemikali za  acetylcholine, serotonin, na dopamine, uti wa mgongo, eneo la chini ya mgongo (kiuno), eneo la nyonga.

Viungo vingine ni misuli maalumu iitwayo pelvic floor, tezi pituitari (pituitary gland), utando maalumu wa uumeni uitwao tunica albuginea, misuli iitwayopubococcygeus [PC muscles], kemikali ya nitric oxide, kemikali ya prolactin n.k.
Nadhani unaona jinsi ilivyo vitu vingi.

Nini maana ya kupungua nguvu za kiume?

Unapopungua nguvu za kiume ina maana ndani ya mwili wako kuna baadhi ya vitu katika vitu nilivyovitaja hapo juu havifanyi kazi vizuri jinsi ipasavyo na inavyotakiwa. Yawezekana ni figo ndilo halifanyi kazi vizuri, au ini, au tezi dume, au neva ya parasympathetic, au moyo una tatizo au mishipa ya ateri, au misuli ya pelvic au homoni fulani iko juu sana au iko chini sana (hormonal imbalance), orodha ni ndefu sana.

Kitendo cha baadhi ya viungo hivyo kutofanya kazi vizuri basi hapo hutokea upungufu katika nguvu za kiume. Upungufu huo unaweza kuwa ni:

1. Kukosa hamu ya mapenzi; au

2. Uume kusimama kwa uregevu; au

3. Kuwahi kufika kileleni; au

4. Kuchelewa sana kufika kileleni (au kushindwa kufika kileleni kabisa); au

5. Kushindwa kurudia tendo la ndoa; au

6. Kuhisi maumivu wakati wa tendo la ndoa au baada ya tendo hilo; au

7. Kukosa pumzi na uchangamfu wa mwili katika utendaji; au

8. Kuchoka sana baada ya tendo la ndoa na hata kukinai kabisa au hata kusikia kichefuchefu;

Ili uelewe vizuri zaidi labda niseme kwamba, nguvu za kiume ni kama kiwanda; na ni zaidi ya kiwanda. Ndani ya kiwanda kuna umeme, maji, madawa, watu (wafanyakazi wa kila taaluma na fani), mashine, mitambo n.k.

Ikitokea kitu kimojawapo kukosekana, mathalani umeme, au wafanyakazi wakagoma, au kukakosekana madawa muhimu au maji na kadhaa wa kadha, basi bidhaa inayotarajiwa kupatikana sokoni, kwa hakika haitapatikana.

Vivyo hivyo nguvu za kiume, mathalani, ikitokea tezi dume kutofanya kazi vyema, basi hapo mwanaume hatoona nguvu za kiume, zitapungua au zitaisha kabisa!

Kwa hiyo upungufu wa nguvu za kiume ni upungufu au kasoro za kiutendaji wa viungo ndani ya mwili wa mwanaume. Mwanaume yoyote anapaswa kutambua jambo hili.

Lakini nini kinachopelekea viungo hivyo vishindwe kufanya kazi vizuri?

Kuna maradhi kadhaa, vyakula tunavyokula, tabia na mtindo wa maisha vinavyoweza kupelekea viungo hivyo kutofanya kazi vizuri. Baadhi ya maradhi hayo na tabia hizo ni kujichua/punyeto (masturbation) kwa muda mrefu; kisukari; presha ya kupanda; presha ya kushuka; uvutaji wa sigara; unywaji wa pombe; madawa ya kulevya; kufanya kazi kupita kiwango na kukosa muda wa kupumuzika; matatizo ya kukosa usingizi na kuchelewa kulala usiku.

Uume wako unatakiwa usimame kwenda juu siyo usimame kwenda mbele tu au kurudi chini. Na ukielekea juu uwe umenyooka kama rula usijikunje kama ndizi maana ukijikunja hilo ni tatizo la kitu kinachoitwa plaque kuganda kwenye uume. See? Ndo maana tunaelimishana rafiki. Tatizo la nguvu za kiume ni pana sana.

Hata hivyo kuna vitu unaweza kufanya ili kurejesha nguvu zako za kiume.

Usilee tatizo. Madhara ni makubwa mno likiendelea kwa muda mrefu!

Mawasiliano haya hapa.

#WhatsApp +255620204770

TATIZO LA KUTOPATA CHOO(CONSTIPATION)

#CONSTIPATION/TATIZO LA KUTOPATA CHOO.

#KAMA UNAPATA CHOO MARA 1 KWA SIKU NA UNAKULA MARA 3,UPO KWENYE HATARI YA KUPATA MAGONJWA YAFUATAYO....….…..

~Kansa ya Utumbo.
~Uzito uliozidi.
~Bawasiri(Vinyama sehemu ya haja kubwa).
~Kifo.
~Maumivu ya Kiuno,Mgongo,Mabega,Kichwa,Misuli.
~Kukosa usingizi(Insomnia)
~Kukosa hamu ya kula(Loss of appetite).
~Tumbo kuja gesi.
~Vidonda vya tumbo(Ulcers).
~Upungufu wa nguvu za kiume.
~Kushindwa kubeba mimba  au kuzaa.
~Kupasuka kwa utumbo.
~Ileocecal valve incompetence.
~Kutoa harufu mbaya mdomoni na unapojamba.

Soma zaidi hapa.............
Kati ya changamoto ya kiafya niliyokua nayo,ni kutopata choo na kupata choo kigumu kama cha mbuzi,na nilidhani ni kawaida kutopata choo kwa muda wa siku 3 hadi week,kumbe ni tatizo kubwa linaloweza kusababisha 90% ya magonjwa yasiyoambukizwa na hatimae vifo.

#WATU wengi wanasumbuliwa na tatizo hili ambalo huwafanya kuwa na uoga na aibu wa kuelezea na kushindwa hata kwenda hospital kupata tiba.

#CHANZO CHA TATIZO
Tatizo la kutopata choo linasababishwa na mfumo mbovu wa mmeng'enyo wa chakula.

Kwenye utumbo mdogo ambao una urefu wa takribani mara 10 mpaka 13 ya urefu wa mtu husika,kuna Villars, hivi ni kama vidole vinavyokua vinachezacheza ili kumeng'enya chakula,ila kutokana na sumu tunazoingiza mwilini kila siku kutoka kwenye vinywaji,chakula,dawa na hewa,pamoja na mafuta tunayokula kwenye vyakula,zinaenda kujipachika katikati ya Villars (vidole) na hivyo kusababisha vidole visimame(blocked) hivyo chakula hakimeng'enywi na kusababisha chakula unachokula kupitiliza moja kwa moja kwenye utumbo mkubwa,na hapo ndio tatizo linapoanzia.
Na tatizo hili ndio hupelekea kupata tatizo la bawasiri.

#JE, UNAJUA BAWASIRI/HEMORRHOIDS NI NINI????!!

~Ni ugonjwa unaotokana na kuathirika kwa mishipa ya damu ya ndani na Inje ya sehemu ya haja kubwa na wakati mwingine mishipa hiyo huweza kupasuka/kuteleza na kuvuja damu kwenye njia ya haja kubwa na kasababisha kutoka kinyama au uvimbe.

~ugonjwa huu wa bawasiri kwa lugha ya kitaalamu tunauita HEMORRHOIDS ilhali kwa lugha ya kingereza unafahamika kama piles.

~tatizo hili huwaathiri watu wote ila zaidi huwaathiri watu wazima kuliko watoto na inakadiriwa kuwa karibu 50%ya watu wote wako katika hatari ya kupata tatizo hili katika umri wa miaka 30_50

#AINA ZA BAWASIRI

~Kuna Aina mbili za bawasiri

(A) BAWASIRI YA NDANI

~Aina hii ya bawasiri hutokea ndani ya mfereji wa haja kubwa huwa haiambatani na maumivu na wengi huwa hawajitambui kuwa Wana tatizo hili

~Aina hii hutokana na kuvimba na kuharibika kwa mshipa wa artery za ndani ya mfereji wa haja kubwa

(B)BAWASIRI YA NNJE

~Aina hii ya bawasiri hutokea katika eneo la mwisho kabisa la mfereji wa haja kubwa na huambatana na maumivu makali na kuwashwa kwa ngozi katika eneo la tundu Hilo pia husababisha mishipa ya damu (vena) kupasuka na damu kuganda na kasababisha Aina ya bawasiri iitwayo THROMBOSED HEMORRHOIDS

#CHANZO CHA TATIZO

~chanzo halisi cha ugonjwa huu hakijapatikana ila Kuna vitu ambavyo huwa chanzo cha kupata ugonjwa wa bawasiri ambayo ni

°Kufanya mapenzi kinyume na maumbile.
°Kuharisha kwa muda mrefu.
°Tatizo la kutopata choo.
°Matatizo ya umri.
°Shughuri ya kukaa kwa muda mrefu sana.
°Uzito kupita kiasi.
°Matumizi ya vyoo vya kukaa kwa muda mrefu.
°Vyakula vyenye mafuta kwa wingi.
°Vinywaji vikali kama pombe,kahawa,viroba.
°Kutokula vyakula vya nyuzi nyuzi.
°Kutokunywa maji ya kutosha.
°Vyakula vya ngano,wanga na vilivyokobolewa.
°Kutofanya shughuli yoyote baada ya kula.
°Kulala kabla ya masaa 4 baada ya kula usiku.

#DALILI ZA KUTOPATA CHOO NA BAWASIRI.

√ Ngozi kuwasha katika eneo la tundu la haja kubwa.
√ kupata maumivu makali wakati wa kujisaidia.
√ kutokea uvimbe/kinyama katika eneo la tundu la haja kubwa.
√kinyesi kuwa na damu na kunuka harufu mbaya sana.
√ Kinyesi cha makundi makundi kama cha mbuzi.
√ Kuhisi moto wakati wa kujisaidia.
√ Kutopata choo kwa siku 2 na kuendelea.
√ Tumbo kujaa gesi na kujisaidia hewa.
√ Kuhisi maumivu ukikaa.
√ Kusinzia baada tu ya kula
√ Tumbo kuunguruma.
√ Kujamba kila wakati.
√ Kukosa hamu ya kula.
√ Mkojo wenye rangi(ambao sio mweupe kama maji)

#MATIBABU NA JINSI YA KUEPUKA TATIZO LA BAWASIRI NA KUTOKUPATA CHOO.

~matibabu ya bawasiri hutegemea na Aina ya bawasiri pia tiba iliyozoeleka ni kukatwa kinyama na kuendelea na lishe ya chakula,kama kula matunda,mboga za majani,maji kwa wingi, hata hvyo tiba hii si nzuri kwasababu huwa haitibu chanzo cha tatizo hivyo huwa rahisi kujirudia.

#MADHARA YA TATIZO LA KUTOPATA CHOO NA BAWASIRI.

-kupata upungufu wa damu (anemia).
-Kupata tatizo la kutokuweza kuhimili choo.
-hupunguza nguvu za kiume na kuondoa hamu ya tendo la ndoa kwa wanawake.
-kuathirika kisaikolojia
- kukosa moral ya kufanya Kazi kutokana na maumivu makali.
- Kupasuka kwa utumbo na kusababisha kifo.
- Kitambi na uzito uliopindukia.
- Kansa ya Utumbo.
- Kukosa uwezo wa kubeba mimba.
- Na mengine yoote niliyoyataja mwanzo wa post.

Na Kwa ushauri zaidi juu ya nini ufanye kama una tatizo hilo,na kwa lengo la kujikinga,usikose makala ijayo

Friday, June 16, 2017

UGONJWA WA KIDOLE TUMBO(APPENDICITIS) NA TIBA YAKE

TAMBUA UGONJWA WA KIDOLE TUMBO
(APPENDICITIS) NA TIBA YAKE

Kidole tumbo au Apendeksi hupatikana katika utumbo mkubwa, urefu wake ni kama kidole cha mwisho cha mkono, huwa hakina kazi yoyote mwilini. Sehemu hii hupitisha myeyuko wa chakula na endapo katika chakula hicho kuna michanga au vitu vidogovidogo vigumu, hujikita humo na kushindwa kutoka.

Kidole tumbo pia kinapatikana upande wa kulia wa tumbo kutoka usawa wa kitovu na nyonga ya kulia.
Taka ngumu hizo zikishajikita kwenye kidole  tumbo na kushindwa kutoka ndipo kinapoanza kuvimba, hali hii kitaalam huitwa ‘Inflammation’. Hapa kidole tumbo kinavimba na kuwa na maumivu na pia hupata maambukizi ya bakteria.

DALILI ZA UGONJWA

Mgonjwa huanza kuhisi maumivu ya tumbo  kuanzia usawa wa kitovu ambayo huwa makali na kuacha kisha kusambaa taratibu kuelekea upande wa kulia.

Baada ya muda mgonjwa huanza kutapika  kisha kupata homa. Dalili hizi huwa haziji pamoja, huanza moja na kufuata nyingine lakini mgonjwa akiwahi kupata tiba dalili nyingine haziendelei. Baada ya hapo mgonjwa hupata homa.

Dalili za ugonjwa zinatofautiana kufuatana na aina ya ugonjwa huu ambapo kawaida umegawanyika katika hali ya ukali ‘Acute’ na hali ya usugu ‘chronic’. Maumivu makali yanayoambatana na homa na kutapika tunaita ni ‘Acute’

Maumivu ya ugonjwa huu ukifikia hatua mbaya husambaa hadi katika uti wa mgongo usawa wa kitovu au ‘Belly button’.

Pamoja na kwamba maumivu huanzia usawa wa kitovu, lakini dalili za awali kabisa huanzia juu ya kitovu ambayo huja na kupotea na mgonjwa anaweza kujihisi ana ugonjwa wa vidonda vya tumbo, baadaye ndipo hushuka chini taratibu na kusambaa.

Dalili hizi ni tofauti na watoto ambao hulalamika tumbo linauma sehemu zote kukiwa hakuna eneo maalam na baadaye maumivu huwa makali sana kwa tumbo lote hata akiguswa linauma sana.

Hali ya tumbo kuuma huambatana na kujaa gesi kwa wote yaani wanaume, wanawake na watoto.

CHANZO CHA TATIZO

Kama tulivyoona hapo awali chanzo cha tatizo, maumivu makali ‘Acute’ hapa hutokana na vile vitu vigumu vilivyoingia katika kidole tumbo kushindwa kutoka hivyo huziba kwa juu na zile taka ngumu huganda humo na kidole tumbo kuzidi kuvimba.

Hali ya usugu wa maumivu hutokana na taka ngumu hizo kukaa humo kwa muda fulani na baadaye hutoka huku ukiacha hali ya kidole tumbo kuwa na uvimbe.

Hali ya uvimbe ikikaa muda mrefu husababisha mzunguko wa damu kuzuiliwa sehemu hiyo hivyo kidole tumbo huvimba zaidi na husababisha kuta za Apendeksi kuharibika ‘Necrtotic’ na kukusanya majimaji kama usaha.

Hali hii husababisha tatizo liitwalo ‘Peritonitis’ yaani tumbo lote huathirika na kuuma. Mgonjwa akichelewa kupata tiba, usaha huu husambaa katika mfumo wa damu na kusababisha kifo.

UCHUNGUZI

Huzingatia historia ya mgonjwa, dalili na ishara zitajitokeza, vipimo vya damu vitafanyika, vipimo vingine ni vya Ultrasound na CT Scan ya tumbo vitasaidia kujua tatizo kwa undani zaidi.

Zipo pia njia mbalimbali za uchunguzi ambazo daktari anaweza kuzitumia mfano ‘Rovsing’s sign’ na  sitokovkty’s sign na nyinginezo.
Matibabu

Tatizo hili katika hatua za awali mgonjwa anaweza kutibiwa kwa dawa lakini tatizo linapoendelea inabidi afanyiwe upasuaji kuondoa Apendeksi.

Tatizo likiwa kubwa, upasuaji wa dharura hufanyika. Ni vema uwahi hospitali kwa uchunguzi na tiba.

Thursday, June 15, 2017

VIDONDA VYA TUMBO NA SABABU ZAKE

HABARI ZENU WADAU WA MAKALA ZANGU..?

LEO NIMEONA NIZUNGUMZIE VIDONDA VYA TUMBO NA SABABU ZAKE.

UGONJWA wa VIDONDA vya TUMBO hutokea iwapo KIDONDA cha UKUBWA wa angalau NUSU sentimita kitatokea kwenye sehemu yeyote ya UKUTA wa TUMBO au UTUMBO wa BINADAMU.

Kwa kawaida TATIZO hili huleta MAUMIVU MAKALI sana ya TUMBO ingawa si lazima kila MAUMIVU ayapatayo MGONJWA husababishwa na VIDONDA vya TUMBO .

Tafiti zimeonesha kwamba karibu ASILIMIA 70% mpaka ASILIMIA 90% ya VIDONDA vya TUMBO husababishwa na aina ya VIMELEA vya BAKTERIA wajulikanao kama Helicobacter pylori.

Aidha MATUMIZI ya baadhi ya DAWA za kutuliza MAUMIVU za JAMII ya Non Steroid Anti-inflamatory Drugs(NSAIDs), kama Aspirin au Diclofenac HUWEZA kusababisha au KUONGEZA uwezekano wa kupata UGONJWA huu.

Kuna DHANA iliyozoeleka kuwa VIDONDA vya TUMBO huathiri zaidi MFUKO wa kuhifadhia CHAKULA yaani TUMBO (stomach). DHANA hii SI KWELI kwani sehemu INAYOATHIRIWA ZAIDI na TATIZO hili ni SEHEMU ya KWANZA ya UTUMBO MDOGO ijulikanayo kama DUODENUM .

Kuna MAKUNDI MAKUU yafuatayo ya UGONJWA huu:-

1.VIDONDA vinavyotokea kwenye MFUKO wa kuhifadhia CHAKULA yaani TUMBO (Gastric ulcers)

2. VIDONDA vinavyotokea kwenye SEHEMU ya KWANZA ya UTUMBO MDOGO (Duodenal Ulcers)

3. VIDONDA vinavyotokea kwenye KOO (Oesophageal ulcers)

4. VIDONDA vijulikanavyo kama Merckel’sDiverticulum ulcers.

VISABABISHI:-

VIDONDA vya TUMBO husababishwa na MAAMBUKIZI ya BAKTERIA aina ya Helicobacter pylori.

Imeonekana kuwa zaidi ya ASILIMIA 50% ya WATU duniani wana VIMELEA hivi katika UTUMBO .

Aidha, MIONGONI mwao, karibu ASILIMIA 80% huwa hawaoneshi DALILI yeyote ya KUUGUA UGONJWA huu.

AINA hii ya VIMELEA vya BACTERIA husababisha karibu ASILIMIA 60% ya VIDONDA vinavyotokea kwenye TUMBO (gastric ulcers) na zaidi ya ASILIMIA 90% ya duodenal ulcers.

HALI hii husababishwa ZAIDI na KUSHINDWA kwa MFUMO wa KINGA MWILINI KUWAUA na KUWAONDOA kabisa VIMELEA hawa NDANI ya MWILI .

MATOKEO ya kushindwa huku HUSABABISHA kuwepo UAMBUKIZI wa KUDUMU katika KUTA za TUMBO (chronic active gastritis), UAMBUKIZI ambao huharibu MFUMO na UWEZO wa KUTA za TUMBO kutunza HOMONI ya GASTRIN, ambayo ni MUHIMU katika kuhakikisha MAZINGIRA ya TUMBO yanakuwa na KIWANGO salama cha TINDIKALI.

Kwa KAWAIDA, KAZI ya GASTRIN ni KUCHOCHEA utolewaji wa TINDIKALI (gastric acid) kutoka kwenye SELI za UKUTA wa TUMBO zijulikanazo kama Parietal cells.

Iwapo BACTERIA hawa WATASHAMBULIA na kuharibu UKUTA wa TUMBO , MFUMO wa GASTRIN pia UHARIBIKA, na hivyo kusababisha GASTRIN kuzalishwa kwa WINGI hali ambayo pia huchochea UZALISHAJI wa GASTRIC ACID kwa WINGI.

MATOKEO ya KUZALISHWA kwa WINGI kwa TINDIKALI hii hupelekea KUCHUBUKA kwa UKUTA wa TUMBO na hivyo kusababisha VIDONDA vya TUMBO .

MATUMIZI ya MUDA MREFU ya DAWA za kuondoa MAUMIVU za kundi la NSAIDs:-

UKUTA wa UTUMBO hujilinda na MADHARA yatokanayo na TINDIKALI ya UTUMBO (gastric acid) kwa kuwa na UTANDO LAINI (mucus) ambao hutolewa na VICHOCHEO vijulikavyo kama Prostaglandins.

DAWA hizi za KUNDI la NSAIDs huharibu MFUMO wa kutengeza VICHOCHEO hivi yaani prostaglandins na hivyo kufanya KUTA za TUMBO kukosa UTANDO wa KUZILINDA na MASHAMBULIZI ya TINDIKALI hali ambayo hupelekea KUTOKEA kwa VIDONDA vya TUMBO.

UVUTAJI wa SIGARA :-

Uvutaji SIGARA sambamba na MAAMBUKIZI ya BAKTERIA aina ya Helicobacter pylori huongeza MADHARA ya UGONJWA wa VIDONDA vya TUMBO.Ifahamike tu kuwa UVUTAJI SIGARA pekee hausababishi VIDONDA vya TUMBO.

VYAKULA au VIUNGO vya CHAKULA vyenye UCHACHU :-

KINYUME na DHANA iliyozoeleka miongoni mwa WATU wengi, baadhi ya VYAKULA vyenye UCHACHU na UPILIPILI kama vile PILIPILI, NDIMU, LIMAO na MASALA, HAVINA UHUSIANO na UWEZEKANO wa kupata VIDONDA vya TUMBO .

WATU walio katika KUNDI la DAMU la O :-

IMEONEKANA pia kwamba KUNDI la DAMU lijulikanalo kama BLOOD GROUP O, HALINA uhusiano wa kusababisha VIDONDA vya TUMBO.

UNYWAJI wa POMBE :-

UNYWAJI wa POMBE pekee hausababishi VIDONDA vya TUMBO. Hata hivyo, UNYWAJI wa POMBE sambamba na MAAMBUKIZI ya VIMELEA vya Helicobacter pylori huongeza MADHARA ya UGONJWA wa VIDONDA vya TUMBO.

VITU vingine:-

VITU vinavyohusishwa na UONGEZAJI wa MADHARA ya VIDONDA vya TUMBO ni pamoja na UPASUAJI wa TUMBO (major abdominal surgeries), KUUNGUA kwa MOTO (burns), UGONJWA wa FIGO ,na KUBADILISHWA kwa VIUNGO vya MWILI kama FIGO au INI .

DALILI au VIASHIRIA vya VIDONDA VYA TUMBO:-

# MAUMIVU MAKALI au KIUNGULIA maeneo ya CHEMBE MOYO (epigastic pains).

# MAUMIVU juu KIDOGO ya TUMBO mara nyingi HUENDANA na MUDA wa KULA CHAKULA . MTU mwenye VIDONDA kwenye TUMBO (gastric ulcers) hupata MAUMIVU MAKALI sana kipindi ANAPOKULA au mara tu BAADA ya KUMALIZA KULA wakati aliye na VIDONDA kwenye SEHEMU ya kwanza ya UTUMBO MDOGO (duodenal ulcers) hupata MAUMIVU MAKALI anapokuwa na NJAA na hupata NAFUU pindi ANAPOKULA .

(i) KUVIMBIWA au TUMBO kujaa GESI. HALI hii pia yaweza KUENDANA na KUBEUA au KUJAMBA mara kwa mara.

(ii) KUCHEUA na KUONGEZEKA kwa MATE yanayoshuka TUMBONI baada ya KUCHEUA .

(iii) KICHEFUCHEFU na KUTAPIKA

(iii) Kupoteza HAMU ya KULA na KUPUNGUA UZITO

(iv) Kutapika DAMU

(v) Kupata HAJA KUBWA cha RANGI NYEUSI au KAHAWIA chenye HARUFU MBAYA SANA.

HII humaanisha MGONJWA anapata HAJA KUBWA au CHOO kilichochanganyika na DAMU kwa mbali

UWEPI wa DALILI kama KIUNGULIA cha MUDA MREFU, KUCHEUA na KUTAPIKA baada ya KULA na HISTORIA ya KUTUMIA DAWA za KUPUNGUZA MAUMIVU (NSAIDs) kwa MUDA MREFU bila KUFUATA ushauri wa DAKTARI ni ISHARA tosha ya kumfanya MGONJWA kumuona DAKTARI kumpima na kumfanyia UCHUNGUZI ili KUJIRIDHISHA kuwa HANA TATIZO la VIDONDA vya TUMBO .

KAMA UNAZO DALILI HIZO USISITE KUFIKA HOSPITALI [KITUO CHA AFYA] KILICHO KARIBU NAWE KWA MSAADA ZAIDI

FAIDA ZA KUNYWA MAJI ASUBUHI(KABLA YA KIFUNGUA KINYWA)

KUNYWA MAJI KABLA YA KIFUNGUA KINYWA ASUBUHI -YANATIBU MARADHI MENGI.

Kiafya binadamu utunatakiwa kunywa glasi 7-8 kwa siku ni muhimu kwa afya zetu.Watu wengi hawajui kama kunywa maji asubuhi pale uamkapo ni kinga moja kubwa mwilini.image.Tiba hii huu inaitwa Ayurvedic treatment inafaida nyingi ya kukuepusha na maradhi.

sehemu kubwa ya mwili wa mwanadamu ni  maji  kwa asilimia 70% ambayo ndio inasaidia mwili Wake ufanye kazi kiufasaha,wakati cell ya ubongo wa binadamu una maji kwa asilimia 85%,damu inakiasi cha maji kwa asilimia 82%,muscles inatumia maji asilimia 75% wakati mifupa inamaji asilimia 25%.Mpaka hapo inaonyesha maji ni muhimu sana kwa mwili wa binadamu .

Umuhimu wa kunywa maji asubuhi kabla ujaingiza chochote tumboni.

Unatakiwa kunywa maji pale uamkapo ukiwa ujakula chochote,itakusaidia kusafisha mfumo wako wa mmeng’enyo (internal system) kwa urahisi. Itatoa uchafu  na sumu kwenye Colon ulizozila kupitia  vyakula tofauti tofauti .Faida nyinginezo ni

Kungarisha ngozi.

Renew cells.

Kusafishwa kwa colon na kufanya unyonywaji wa virutubisho kuwa rahisi.

Inatibu magongwa na maradhi .Unywaji wa maji asubuhi pale uamkapo inakusaidia kutibu maradhi kama matatizo ya ini,TB,kuhara,cancer,matatizo ya macho,maumivu ya kichwa,stress,uti wa mgongo.

Hupunguza uzito.

Kunywa maji pale uamkapo liters 1.5 ( glas 5-6),epuka kunywa kinywaji kingine chochote au kula kabla na baaya ya kunywa maji ,usinywe pombe baada ya siku 2 ndio uendelee na kunywa maji yako kila asubuhi .Mwanzo itakuwa ngumu sana kunywa glas 6 kwa pamoja unachotakiwa kunywa 4 pumzika kidogo kunywa izo 2 zilizobakia.Utafanya hivyo baada ya siku 3 utumbo utaozoea na utakunywa kwa urahisi.

Hii water therapy ilizinduliwa na wajapan baada ya kuifanyia utafiti wa mda mrefu na kubaini inatibu maradhi  mengi iwapo mgonjwa atafatisha sheria zake kama

Uamkapo kunywa maji moja kwa moja bila kupiga mswaki au kula chochote.

Piga mswaki na usile chochote sababu yale maji yanahitaji kutoa uchafu kabla ujaweka chakula au  kinywa tumboni.

Bada ya dakika 45 unaweza kunywa breakfast.

Baada ya breakfast usile kitu chochote baada ya masaa 2.

       Kipimo cha maji kulingana na maradhi.

Constipation-wenye matatizo ya kuapa haya kubwa watafata hii kinga ya maji  kwa siku 10

TB-siku 90

Kisukari siku 30

Gastric -kuwa na gesi nyingi tumboni -siku 10

Pressure (high blood pressure) siku 30.

Unatakiwa kunywa maji kwa wingi haswa wale wanaoishi sehemu za joto .Epuka kuwa dehydrated kwani utakaribisha maradhi kwa urahisi...Endelea kuwa nami kwa makala nyingi za afya

Wednesday, June 14, 2017

FAIDA TISA(9) ZA KULA NANASI

FAIDA ZA KULA NANASI KWA AFYA YAKO

Hapa tuta angalia faida kuu za kula nanasi na Wote tunajua kuwa kula matunda mazuri inasaidia mwili kupata vitamin na madini mbalimbali na kuwa mtu mwenye afya njema, na sasa tunda la nanasi ni tunda moja wapo ambalo ni muhimu sana hasa katika msimu huu wa mananasi.

1: Mmeng’enyo wa chakula.

Nanasi linasaidia kurahisisha mmeng’enyo wa chakula kwa kiasi kikubwa sana. Hii inatokana na kuwa nanasi linatoa aina protini katika mwili wako ambayo inarahisisha kazi hii ya kumeng’enya chakula.

2: Nanasi Lina Vitamin na Madini

Tunda la nanasi limejaa madini na protini nyingi ambazo zinafaa kwa mwili wako. Nanasi lina vitamin A Vitamini C calcium, fiber na pia potassium.

3: Kuzuia Kikohozi na Baridi.

Tangu nanasi lina utajiri wa vitamin C linaweza kupigana na virusi amabavyo vinaweza kusababisha kikohozi na ubaridi. Hata kama umeshakuwa na kikohozi nanasi kwa kiasi flan linaweza kukusaidia kupunguza makali. Tunda hili lina madini ya Bromelain ambayo yanauwezo wa kudhoofisha virusi vya kikohozi. Wakati unaumwa kula tunda la nanasi hata wakati unakuwa kwenye dozi ya dawa ambazo umepewa na daktari linaweza kukusaidia sana kuharakisha kupona haraka.

4: Kuimarisha Mifupa.

Je unahisi mifupa yako sio imara? Basi anza kula nanasi. Nanasi pia lina uwezo wa kuimarisha mifupa nakuifanya kuwa yenye nguvu. Hii ni kwa sababu nanasi lina madini ya manganese ambayo mwili wako unahitaji madini haya ili kwa ajili ya kuimarisha mifupa yako. Tena kama ukinywa kikombe kimoja tu cha juice ya nanasi unakua umeongeza asilimia 73% ya madini ya manganese ambayo ni hata zaidi ya mwili unavyoihitaji kitu ambacho ni kizuri kwa afya ya mifupa ya mwili wako. Unakua na mifupa iliyokomaa.

5: Huimarisha Meno yako.

Watu kila mara huwa wanajali sana meno yao, na mara nyingine huwa wanashindwa kuyapa kipaumbele kwa saaana. Kama una matatizo ya meno basi unashauriwa kula nanasi kwa sababu nanasi linasaidia kuimarisha magego ambayo yanashikiria meno. Kula tunda la nanasi linakufanya kuimarisha magego yanayoshikiria meno na pia meno yenyewe yanaimarika.

6: Huzuia Ugonjwa wa Asthma.

Ukila nanasi unajiweka katika hali nzuri ya kuto pata ugonjwa wa asthma. Watu wanaokula nanasi wanakua katika hali nzuri kwa sababu nanasi lina vitamin aina ya Beta Carotene ambayo linausaidia mwili kukabiliana na magonjwa mbali mbali ikiwemo asthma.

7: Blood Pressure.
Unapokula nanasi unaongeza potassium na pia kula matunda mengine yenye madini ya potassium yanaweza kukusaidia kupunguza uwezekano wa kupata blood pressure.

8. Kansa.
Kama kawaida nanasi lina utajili mkubwa wa vitamin C. Hii vitamin C inauwezo wa kuzuia virusi ambavyo vinaweza kukusababishia magonjwa mabali mabli ya kansa.

9. Huimarisha Afya ya Moyo.

Utajiri wa madini ya fiber, potassium na vitamin C ni mojawapo ya faida za tunda hili ambazo pia zina uwezo wa kuimarisha afya ya moyo wako na kuzuia maradhi yanayoweza kuuadhiri moyo wako.

Sasa jamani tuanze kula tunda la nanasi ili tuweze kufaidi madini ya na vitamin zilizojaa katika tunda hili. ili kuepuka magonjwa ya baadaee. 

Endelea ku subscribe blog hii kwa Habari zaidi. >>>>>>>>

FAHAMU MWANAMKE ANAVOPATA MIMBA

FAHAMU JINSI MWANAMKEE ANAVYO PATA MIMBA

Wengi hasa wanawake wamekuwa wakiuliza maswali mengi sana kuhusuana na jinsi ya mwanamke kupata mimba au kuzuia kutopata mimba.
Naamini maelezo yafuatayo ukisoma kwa makini unaweza kupata ufahamu na kujibiwa maswali yako yote ambayo yamekuwa yanakutatiza.
Pia ni vizuri kuzingatia na kutochanganya Kalenda ya menstrual cycle tunayoongelea hapa na ile 'kalenda ya mwaka' inayohusu tarehe za miezi 12 ya mwaka ambayo huwa tunaitundika ukutani huko nyumbani na maofisini kwetu!

Wanawake wamegawanyika katika makundi makubwa 4 linapokuja suala la siku za hedhi

Mzunguko mfupi yaani siku 22
Mzunguko wa kati yaani siku 28
Mzunguko mrefu yaani siku 35
Na mzunguko abnormal siku 15

Kama mwanamke ana menstruation cycle ya siku 22 inabidi afanye kama ifuatavo:

Kwanza itabidi atengeneze kalenda yake mwenyewe ya siku zake zote za menstruation cycle kama hapa chini:
1st, 2nd, 3rd, 4th, 5th, 6th, 7th, 8th, 9th, 10th, 11th, 12th, 13th, 14th, 15th, 16th, 17th, 18th, 19th, 20th, 21st, 22nd.

Kisha ahesabu kuanzia ile 22nd day kurudi nyuma mpaka afikishe siku 15.
Ataona kuwa siku ya kumi na tano inaangukia kwenye 8th day ya kalenda yake.
Hivyo 8th day ndiyo siku ya mimba kwa mwanamke yeyote ambaye ana menstration cycle ya siku 22.
Akumbuke kwamba 1st day ndiyo siku anayoanza ku-bleed!

Kama mwanamke ana menstruation cycle ya siku 28 inabidi afanye kama ifuatavo:
Kwanza itabidi atengeneze kalenda yake mwenyewe ya siku zake zote za menstration cycle kama hapa chini:
1st, 2nd, 3rd, 4th, 5th, 6th, 7th, 8th, 9th, 10th, 11th, 12th, 13th, 14th, 15th, 16th, 17th, 18th, 19th, 20th, 21st, 22nd, 23rd, 24th, 25th, 26th, 27th, 28th.

Kisha ahesabu kuanzia ile 28th day kurudi nyuma mpaka afikishe siku 15.
Ataona kuwa siku ya kumi na tano inaangukia kwenye 14th day.
Inamaana kwamba 14th day ndiyo siku ya mimba kwa mwanamke yeyote ambaye ana menstruation cycle ya siku 28.
Akumbuke kwamba 1st day ndiyo siku anayoanza ku-bleed!
Kama mwanamke ana menstruation cycle ya siku 35 inabidi afanye kama ifuatavo:
Kwanza itabidi atengeneze kalenda yake mwenyewe ya siku zake zote za menstruation cycle kama hapa chini:
1st, 2nd, 3rd, 4th, 5th, 6th, 7th, 8th, 9th, 10th, 11th, 12th, 13th, 14th, 15th, 16th, 17th, 18th, 19th, 20th, 21st, 22nd, 23rd, 24th, 25th, 26th, 27th, 28th, 29th, 30th, 31st, 32nd, 33rd, 34th, 35th.

Kisha ahesabu kuanzia ile 35th day kurudi nyuma mpaka afikishe siku 15.
Ataona kuwa siku ya kumi na tano inaangukia kwenye 21st day.
Inamaana kwamba 21st day ndiyo siku ya mimba kwa mwanamke yeyote ambaye ana menstruation cycle ya siku 35.
Akumbuke kwamba 1st day ndiyo siku anayoanza ku-bleed!
Kama mwanamke ana abnormal menstruation cycle ya siku 15

BASI KUNAUWEZEKANO WA KUTOPATA MIMBA KABISA KAMA INAVYOONEKANA HAPA CHINI:

Kwanza itabidi atengeneze kalenda yake mwenyewe ya siku zake zote za menstruation cycle kama kawaida:
1st, 2nd, 3rd, 4th, 5th, 6th, 7th, 8th, 9th, 10th, 11th, 12th, 13th, 14th, 15th.
Kisha ahesabu kuanzia ile 15th day kurudi nyuma mpaka afikishe siku 15.
Ataona kuwa siku ya kumi na tano inaangukia kwenye 1st day.
Inamaana kwamba, the 1st day of her bleeding ndiyo siku ya mimba kwa mwanamke yeyote ambaye ana menstruation cycle ya siku 15.
Akumbuke kwamba 1st day ndiyo siku anayoanza ku-bleed, na ndiyo hiyo hiyo siku ambayo mwanamke wa kundi hili anaweza kupata mimba!
Hii inamaana kwamba, siku ambayo linaharibika lile yai la upande mmoja ndiyo siku hiyo hiyo ambayo yai la upande wa pili linapevuka tayari kwa kurutubishwa.
Mwanamke wa aina hii anaweza kupata mimba tu kama atakutana na mwanaume siku ile anayoanza kubleed, kwani siku ambayo yai moja linaanza kuharibika ndio siku hiyo hiyo ambayo yai la upande wa pili linakuwa tayari kurutubishwa
Na wanawake wa kundi hili la nne ukiwauliza vizuri watakiri kwamba hawajawahi kuona au ku-feel ule ute mweupe ambao wenzao huwa wanaupata siku ile yai linapokuwa tayari kwa kurutubishwa, kwani ute wa wanawake wa kundi hili la nne huwa unachanganyikana na damu kwa vile unatoka siku ile ile wanapoanza ku-bleed.Pia wanawake wa kundi hili huwa wanatokwa na kiasi kidogo sana cha damu na bleed hukatika ndani ya siku moja au mbili tu!

Endelea kuwa pamoja nami na unaweza share na wenzako walitambue hili...

Tuesday, June 13, 2017

JINSI YA KUONDOA CHUNUSI KWA NJIA YA ASILI

JINSI YA KUONDOA CHUNSI KWA NJIA YA ASILI

Magadi Soda:
Magadi soda ni mazuri sana kwa kusafishia uso na haswa ukiwa na chunusi. Changanya kiasi kidogo cha magadi soda na maji ya kutosha kuunda kidonge kidogo na kisha weka au kandika kidonge icho sehemu ilio athirika na chunusi. Kwa muda wa dakika 15-20 au mpaka ikauke, na kisha suuza kwa maji yasiwe ya moto. Unaweza kurudia rudia mara kadhaa kwa siku mpaka utakapo ona athari ya chunusi imepotea.

Matango:
Unaweza kutumia Tango kwa kuondoa chunusi na hata kuondoa mabaka mabaka katika ngozi na kuifanya ngozi yako kuonekana yenye afya na yenye kuvutia.
mazuri sana kwa kusafishia uso na haswa ukiwa na chunusi. Kata tango na kasha liponde ponde (unaweza kutumia blenda) kisha paka au kandika usoni. Wacha ikae kwa muda wa dakika 15-20  kisha suuza kwa maji baridi. Unaweza kurudia kwa siku mara mbili mpaka mara tatu kwa siku.

Kitunguu Thaumu:
Unaweza kutumia kitunguu thaumu. Kuondoa chunusi. Matumizi ya Kitunguu thaumu, uleta matokeo mazuri sana katika kuondoa chunusi usoni na hata kuuwa bacteria sababu ina kemikali (antiseptiki) inayozuia kukua kwa bakteria kwenye jeraha au ngozi iliyo athirika kwa chunusi au hata kwenye kidonda. Na pia ina viwango vya juu wa salfa (ni zuri kwa ajili kukausha mafuta kwenye ngozi ya mwili). Twanga kitungu thaumu, au unaweza kukata nusu na kubandika sehemu iliyo na chunusi shikilia kwa dakika 5-10, na kisha safisha na maji baridi. Waweza kufanya ivyo asubuhi na jioni.

Mnana (Peppermint):
Unaweza kutumia majani ya Mnanaa kuondoa chunusi usoni.
Majani ya manna utumika hata kwa wale wenye matatizo ya Mba kwenye kichwa. Twanga majani machache au saga kisha weka sehemu iliyo athirika. Wacha mpaka pakauke na kisha safisha kwa maji baridi. Unaweza kufanya hivyo mara kadhaa kwa siku.

Matumizi ya Limao:
Kata limao na kisha kwa kutumia kijiti chenye pamba kiloweke kwa maji ya limao, sugua sehemu yenye chunusi, kisha wacha pakauke, unaweza kurudia rudi kila baada ya masaa kadhaa. Usitumie maji ya limao ya kwenye chupa, kwa sababu yameweka vihifadhi kemikali zingine kiasi cha kuondoa ubora wa kemikali halisi za kwenye limao. Tumia limao alisi.

Kutumia Asali:
Matumizi ya asali ni ya asili na ufanya ngozi, iwe na afya na nyororo. Kwa sababu kwenye asali kuna virutubisho vingi vyenye kazi ya kuua vimelea (bacteria) na kuzuia uchafu na kusinyaa kwa ngozi.
Weka asali kidogo sehemu ilio athirika na iwache kwa muda mrefu kadri uwezavyo. Vilevile unaweza kupaka uso mzima au hata mwili mzima ukitaka. Sababu asali inarutubisha ngozi ya mwili na kuifanya iwe na afya na mwonekano mzuri. Ukisha ridhika na muda wa asali kwenye ngozi yako unaweza kusafisha kwa kutumia maji ya vuguvugu.

Kutumia Papai:
Unaweza kushangaa, lakini matumizi ya papai yameonyesha matokeo mazuri sana katika kuondoa chunusi usoni na kusafisha sehemu zingine za mwili.
Ponda ponda kiasi kidogo cha papai na kisha iwache kwa muda mrefu kadri uwezavyo. Ukisha ridhika na muda unaweza kusafisha kwa kutumia maji ya kawaida. Unaweza kurudia mara kadhaa kila siku kama unataka.

Dawa Ya Meno:
Unaweza kushangaa, lakini ushangazwi na matokeo mazuri ya meno yako kusafishika kwa dawa ya meno.
Kemikali zinazotumika kuuwa Bakteria wa kwenye meno, pia zina uwezo wa kupambana na bakteria wengine. Tumia dawa ya meno isiyo na gel (non-gel) paka kwenye chunusi. Ni vizuri ukatumia usiku wakati wa kwenda kulala, ila si vibaya ukipaka hata muda wa asubuhi au mchana mradi tu uwe na muda wa kutosha wa dawa kukauka ili iweze kufanyakazi vizuri.

Namna nyingine ni kuchanganya dawa ya meno na unga wa mahindi au nganoiuliosagwa na kuwa laini sana. Unaweza kupaka na kuiwacha ikauke kwa dakika tano mpaka 10.
Safisha kwa sabuni. Mchanganyiko huu unasaidia kukausha chunusi.

Matumizi ya Poda:
Unaweza kutumia baby powder kwa kupaka nyakati za usiku wakati wa kwenda kulala na na kuiwacha mpaka asubuhi.

Matumizi ya Mvuke:
Unaweza kutumia mvuke (Steam/vapour) kuondoa mafuta yaliozidi kwenye ngozi ya uso wako. Kwa kujifukisha. Kwa wale ambao hawana mashine wanaweza kujaza sufuria au bakuli kwa maji ya moto na kujifunika kwa taulo uku ukielekeza uso wao kwenye sufuria au bakuli lenye maji yanayotoa mvuke k wa dakika 5-10. Unaweza kufanya hivi pamoja na njia mojawapo nilizo zitaja hapo juu.

Tahadhari:
Njia hizi za Asili, uchukuwa muda kidogo mpaka kuona matokeo ya kuridhisha.
Njia zote hizi kama hazijaleta matokeo mazuri, tafadhali muone daktari wa ngozi au nenda hospitali ilio karibu kwa uchunguzi zaidi wa ngozi yako.

JINSI YA KUJIKINGA NA HOMA YA INI(HEPATITIS B)

HABARI ZENU WADAU WA MAKALA ZANGU?

Leo nimeona nikushirikishe kuhusu UGONJWA WA HOMA YA INI

HOMA YA INI ni UGONJWA unaoambukizwa kwa njia ya VIRUSI ambavyo vikishaingia MWILINI hushambulia INI kabla ya kugeuka kuwa MARADHI SUGU.VIRUSI ivyo vinaitwa HBV - HEPATITIS B VIRUSES.

VIRUSI hivi husambazwa kwa njia ya DAMU au MAJIMAJI mengine ya MWILINI mfano MATE au JASHO.

UGONJWA huu kama haujatibiwa hutengeneza UVIMBE katika INI na kusababisha KANSA ya INI na baadaye KIFO.

JINSI UNAVYOAMBUKIZWA.
Katika maeneo hatari zaidi DUNIANI,virusi vya HEPATITIS B ( HBV ) kwa kawaida husambazwa kutoka kwa MAMA kwenda kwa MTOTO wakati wa kuzaliwa au kutoka kwa MTU mmoja hadi mwingine hususani nyakati za UTOTONI.

Kama ilivyo kwa UKIMWI virusi vya HOMA ya INI navyo huambukizwa kwa njia ya KUJAMIIANA ,MATE,JASHO, na mwingiliano wowote wa DAMU.

NJIA KUU ZA MAAMBUKIZI :-
- Kujamiiana bila kinga.
- Kunyonyana NDIMI ( Denda )
- MAMA mwenye Ugonjwa kumwambikiza MTOTO wakati wa kujifungua.
- Kuchangia DAMU isiyo salama.
- Kuchangia vitu vya ncha kali kama SINDANO ,WEMBE n.k
- Kuchangia MISWAKI .
- Kuchangia TAULO na mwenye Ugonjwa huo.
- Kubadilishana nguo au kukumbatiana wakati mkiwa mnavuja JASHO .

Tafiti zinaonesha kuwa VIRUSI hivi ni HATARI kuliko hata vya UKIMWI kwa sababu vinaweza kuishi NJE ya MWILI wa BINADAMU  ( yaani nje ya mfumo wa damu ) kwa siku SABA.
VIRUSI vya UKIMWI  ( VVU ) havina UWEZO wa kuishi NJE ya mfumo wa DAMU hata kwa DAKIKA moja.

Kutokana na USUGU wa HBV maana yake ni kwamba kama kirusi kipo kwenye NGOZI,kitaendelea kuwa HAI kwa siku SABA na katika kipindi hicho MTU anaweza kuambukizwa kwa njia ya DAMU au JASHO. Kwa wastani kirusi cha HBV kikishaingia MWILINI hupevuka ndani ya SIKU 75.Hata hivyo upo uwezekano wa kupevuka kati ya SIKU 30 hadi SIKU 180.Ndani ya SIKU 30 mpaka SIKU 60, MTU mwenye HBV anaweza kugundulika ikiwa atapimwa.

MTU mwenye HOMA ya INI ana wastani mdogo wa KUISHI kuliko mwenye UKIMWI.

DALILI ZA UGONJWA HUU.
WATU wengi hawaonyeshi DALILI yoyote.
Kwa maana hiyo MTU anaweza kuishi na HBV na kusababisha MAAMBUKIZI kwa WENGINE bila kugundulika.
Hata hivyo WATU wengine husumbuliwa na HOMA KALI na DALILI ambazo hudumu kwa wiki kadhaa. DALILI hizo ni:-
- Uchovu
- Kichefuchefu
- Mwili kuwa dhaifu
- Homa kali
- Kupoteza hamu ya kula
- Kupungua uzito
- Maumivu makali ya tumbo upande wa INI.
- Macho na ngozi kuwa ya njano.
- Mkojo mweusi.
Kwa WAGONJWA wengine, VIRUSI vya HEPATITIS B hukua hadi kusababisha INI kuharibika kabisa ( Cirrhosis of the liver ) au SARATANI ya INI  ( liver cancer  ).

KINGA.
- Chanjo
- Kutumia kinga wakati wa Kujamiiana.
- Kuacha Kuchangia vitu vya ncha kali.
- Kutochangia miswaki.
- Kuwa na mpenzi mmoja mwaminifu.
- Kutochangia damu isiyo salama.

Monday, June 12, 2017

JINSI YA KUPUNGUZA NA KUONDOA MAFUTA TUMBONI KWA WANAWAKE

JINSI YA KUONDOA AU KUPUNGUZA MAFUTA TUMBONI KWA WANAWAKE

Wanawake wengi miaka ya karibuni wanakabiliwa na tatizo linalofanana na kitambi kwa upande wa wanaume. Hivyo ingekuwa ni wanaume tungesema ni kitambi ambalo nalo ni tatizo kubwa miongoni mwa wanaume wengi nyakati za sasa.

Kinachowasumbuwa wanawake siyo kitambi tunasema ni mlundikano wa mafuta sehemu ya chini ya tumbo na tumbo kwa ujumla kufikia hali kuonekana kama ana tumbo kubwa au kuhisi labda ni ujauzito kumbe ni mafuta tu mengi.

Kwa ujumla ni vigumu sana kupunguza tumbo la namna hii, hivyo kwenye post hii pamoja na mengine tutaona pia visababishi vya tatizo lenyewe, dawa za asili zinazoweza kuondoa tatizo hilo na aina ya maisha unayotakiwa kuishi ili ufanikiwe kirahisi zaidi bila kukuachia madhara mengine yoyote.

Nini kinasababisha tumbo kwa kina mama:

*Vyakula feki (Junk food)
*Kutumia vyakula vya wanga kupita kiasi
*Kutokunywa maji ya kutosha kila siku
*Kula chakula kizito muda mchache kabla ya kwenda kulala
*Kukaa masaa mengi kwenye kiti
*Kutokujishughulisha na mazoezi
*Mfadhaiko (stress)
*Kula wali kila siku
*Ugali wa sembe
*Kula vyakula vinavyopikwa katikati ya mafuta mengi (chipsi, maandazi, nk)

Vyakula 25 vinavyoondoa mafuta kwenye tumbo kwa wanawake

1. ASALI NA LIMAU

Chukua asali kijiko kikubwa kimoja cha chakula na majimaji ya limau vijiko vikubwa viwili, changanya hivi viwili ndani ya glasi moja (robo lita) ya maji ya uvuguvugu na unywe yote mara tu ukiamka asubuhi.

Tumia kwa wiki 3 hivi mpaka mwezi mmoja na hutachelewa kuona tofauti.

2. MAJI YA UVUGUVUGU

Kunywa maji ya uvuguvugu kama lita 1 hivi wakati tumbo likiwa tupu hasa asubuhi ukiamka tu. Hii inasaidia kusafisha mwili na kuondoa mafuta yasiyohitajika.

3. NYANYA

Kula nyanya ambazo hazijapikwa pia inasaidia kupunguza tumbo kwa kina mama, hivyo kula kachumbali ya kutosha kila siku ya nyanya peke yake na utaona mabadiliko.

4. TANGAWIZI

Chemsha chai ya tangawizi, ipua na usubiri ipowe kidogo, ongeza asali mbichi kidogo na pilipili manga kidogo ya unga. Pata kikombe kimoja cha chai hii kila siku asubuhi mapema ukiamka tu. Asali inasaidia kuyeyusha mafuta wakati pilipili itauongezea nguvu mfumo wa mmeng'enyo wa chakula.

5. SIKI YA TUFAA

Siki ya tufaa (apple cider vinegar) inasaidia kupunguza njaa na kukufanya ujisikie umeshiba kwa kipindi kirefu. Kunywa kijiko kikubwa kimoja cha siki ya tufaa mara 1 kwa siku kila siku wakati unakula chakula cha usiku. Kazi nyingine ya hii siki ni kuweka sawa damu sukari mwilini hivyo ni nzuri pia kwa wenye kisukari.

6. MAJANI YA BIZARI

Majani ya bizari husaidia kuondoa sumu na takatka nyingine mwilini kitu ambacho moja kwa moja hupelekea mlundikano mdogo wa mafuta katika tumbo. Kunywa chai ya majani ya bizari kila siku asubuhi, ukikosa majani unaweza kutumia hata unga wake.

8. ILIKI

Iliki hufanya kazi ya kuongeza nguvu katika mfumo wa mmeng'enyo wa chakula na ni dawa nzuri sana ya kuondoa sumu na takataka nyingine mwilini. Iliki pia hutumika katika kupunguza uzito. Tengeneza chai yenye iliki kila siku ndani yake, pia ni kiungo karibu kwa vyakula vingi hivyo hakikisha unaiweka katika kila chakula unachopika kwa matokeo mazuri zaidi.

9. MDALASINI

Mdalasini hufanya kazi ya kuchoma mafuta mwilini. Chukua kijiko kidogo kimoja cha mdalasini ya unga na uweke ndani ya glasi 1 ya maji ya moto na uache kwa dakika 5 hivi. Ongeza kijiko kidogo kimoja cha asali mbichi ndani yake na ukoroge vizuri, kisha unywe huo mchanganyiko wote asubuhi ukiamka tu.

10. JUISI YA LIMAU

Kunywa maji ya limau au juisi ya limau kila mara kutakusaidia kuondoa mafuta tumboni kwa haraka sana. Ongeza majimaji ya limau vijiko vikubwa viwili ndani ya glasi 1 ya maji na uongeze punje 1 ya chumvi ya mawe, koroga vizuri na unywe asubuhi ukiamka tu kila siku.

11. KITUNGUU SWAUMU

Ili kupunguza mafuta tumboni katakata vipande vidogo vidogo (chop) punje 3 mpaka 4 za kitunguu swaumu na unywe na maji vikombe viwili asubuhi tu na kisha shushia na glasi moja ya maji yenye limau kidogo kwa mbali. Hii ndiyo njia nzuri kabisa ya asili ya kuondoa mafuta tumboni kwa haraka zaidi.

12. TIKITI MAJI

Tikiti maji lina asilimia 82 za maji kitu kinachofanya tumbo lako kutokuwa na njaa ya kuhitaji chakula. Tikiti maji lina vitamini C ambayo ni mhimu kwa afya bora. Kula tikiti kila siku.

13. MAHARAGE

Kula maharage kila mara kunasaidia kupunguza mafuta katika tumbo. Maharage yana kiasi kingi cha nyuzinyuzi (faiba) kitu kinachosaidia tumbo lako kutojisikia njaa na hivyo itakuwezesha kula chakula kiasi kidogo. Kadri unavyokula chakula kichache ndivyo unavyokuwa mbali na uwezekano wa kuzalisha mafuta mengi tumboni.

Basi kula maharage kila siku.

14. TANGO

Tango lina asilimia 96 za maji na asilimia zinazobaki ni nishati. Tumia kachumbali yenye tango ndani yake kila siku au kula tu tango moja kila siku ili kupunguza mafuta tumboni kwa haraka.

15. PARACHICHI

Parachichi ni tunda lingine zuri sana kwa ajili ya kuchoma mafuta yaliyozidi mwilini. Parachichi ni chanzo kizuri cha nyuzinyuzi (faiba). Parachichi huikimbiza mbali njaa na wewe. Parachichi lina mafuta lakini ni mafuta mazuri (monounsaturated fatty acids) ambayo yenyewe husaidia kuchoma mafuta na hivyo kuondoa mafuta mabaya tumboni kirahisi zaidi.

Kula parachichi 1 kila siku.

16. TUFAA

Kula tufaa maarufu sana kama 'apple' (epo) kunaweza kusaidia kupigana na magonjwa mengi sana mwilini na inaweza pia kusaidia kuondoa mafuta kwenye tumbo lako. Tufaa hukufanya ujisikie umeshiba sana kwa masaa mengi sababu lina potasiamu na vitamini nyingi sana ndani yake.

Hivyo kula tunda hili 1 kila siku asubuhi kupunguza shauku yako ya kutaka kula zaidi ndani ya hiyo siku nzima.

17. MAFUTA YA SAMAKI

Mafuta ya samaki ni mbadala mzuri kabisa katika kuchoma mafuta ya tumboni. Mafuta ya samaki yenyewe hulenga kuyachoma moja kwa moja mafuta yanayozidi tumboni. Ukiweza unaweza kuamua yawe ndiyo mafuta yako ya kupikia, pia unaweza kunywa mafuta haya kijiko kikubwa kimoja kila siku unapoenda kulala.

18. SIAGI YA KARANGA

Siagi ya karanga hupunguza njaa na kuongeza nguvu katika mfumo wa mmeng'enyo wa chakula. Siagi ya karanga ina kiinilishe kijulikanacho kama 'niacin' ambacho chenyewe huzuia mafuta kujilundika tumboni. Hivyo kwenye mkate wako asubuhi ningekushauri utumie hii siagi ya karanga badala ya mafuta mengine ambayo si salama, pia unaweza kutumia hii siagi ya karanga kama mafuta yako ya kuunga katika mboga nyingi unazopika hata katika wali unaweza kutumia kama mafuta yako mbadala.

19. MAYAI

Mayai yana vitamini nyingi sana ndani yake (mayai ya kienyeji lakini) na yana madini pia kama kalsiamu, zinki, chuma, omega -3 nk. Viinilishe vyote hivyo katika mayai husaidia kuchoma mafuta yanayozidi tumboni. Hivyo kula mayai asubuhi kila siku ili kuondoa na kupunguza mafuta mwilini. Mayai pia ni moja ya vyakula vinavyomfanya mtu ajisikie kushiba kwa muda mrefu bila kuhitaji kula kula tena.

20. CHAI YA KIJANI

Chai ya kijani maarufu kama 'Green tea' hufanya kazi ya kuondoa sumu mwilini jambo linalosaidia pia kuchoma mafuta yaliyozidi mwilini. Kunywa chai hii ya kijani kila siku kutafanya ngozi yako kukua vivyo hivyo kufanya tumbo lako kukaa sawa bila kuwa na mafuta mengi.

21. MTINDI

Ingawa mtindi unaweza kupelekea kuongeza uzito zaidi, hata hivyo mtindi mtupu kabisa ule ambao haujaongezwa kingine chochote ndani yake unaweza kukusaidia kupunguza mafuta tumboni. Matumizi yake kwa siku yasizidi kikombe kimoja (robo lita). Pia mtindi ni moja ya vyakula vinavyoweza kukufanya ujisikie umeshiba na hivyo kukuondolea njaa ya kutaka kula.

22. JUISI YA KOTIMIRI

Juisi ya kotimiri (Parsley juice) huondoa sumu na takataka nyingine zozote mwilini, pia huchoma mafuta na nishati. Kotimiri ni dawa nzuri kwa matatizo mbalimbali ya figo pia kwa kuchoma mafuta mwilini.

Pata kikombe kimoja cha juisi hii kila siku unapoenda kulala.

23. NDIZI

Kama lilivyo tufaa, ndizi pia zina kiasi kingi cha potasiamu na vitamini za aina mbalimbali ndani yake. Ukipenda kula ndizi kila mara zinachofanya mwilini mwako ni kuondoa ile hamu ya kutaka kula vyakula feki (fast food). Zaidi sana ndizi huuongezea nguvu mfumo wa mmeng'enyo wa chakula na hivyo kupelekea mafuta ya tumboni kuyeyuka kirahisi zaidi. Kula ndizi kila siku ukiweza ukiamka tu kula ndizi zilizoiva 3 mpaka 5 kila siku.

24. MAJI YA KUNYWA

Kunywa maji ya kutosha kila siku kunasaidia pia kupunguza uzito. Kunywa maji lita 2 mpaka 3 kila siku iendayo kwa Mungu. Kunywa maji kidogo kidogo kutwa nzima. Hili halitafanya kazi ya kusafisha mwili tu bali pia litafanya ngozi yako kung'aa na kukuwa. Nywele zako pia zitaonekana ni zenye afya na mwili mzima utakuwa ni wenye kuvutia.

Kitu cha kwanza ukiamka tu ni kunywa maji glasi 2 na uendelee hivyo hivyo glasi moja moja kila baada ya lisaa limoja au mawili kutwa nzima. Maji ni uhai, bila kunywa maji kila siku ni sawa na kwenda dukani bila hela mfukoni.

Asilimia 94 ya damu yako ni maji, asilimia 85 ya ubongo wako ni maji, asilimia 27 ya mifupa yako ni maji, asilimia 75 ya mwili wako ni maji. Sehemu kubwa ya dunia hii imefunikwa na maji na sehemu yenye ardhi ni kipande kidogo sana. Haijalishi unaishi kwenye baridi au kwenye joto hakikisha unakunywa maji ya kutosha kila siku, huhitaji kusikia kiu au hamu ndipo unywe maji, hapana maji ni lazima uyanywe tu hata iweje.

25. MAZOEZI YA KUTEMBEA

Shida kubwa kwa kina mama wengi wa kiTanzania ni kuwa hawajishughulishi na mazoezi. Hapa Tanzania mazoezi inaonekana ni jambo la wanaume tu. Mazoezi ni jambo la lazima kwa mtu yeyote iwe unaumwa au huumwi.

Ili kuchoma mafuta mwilini kwa haraka zaidi tembea kwa miguu mwendo kasi kidogo lisaa limoja kila siku. Kumbuka nimesema lisaa limoja yaani dakika 60 bila kupumzika (none stop) kila siku. Kutembea kwa miguu lisaa limoja huamsha mwilini kimeng'enya kijulikanacho kama 'lipase' ambacho chenyewe huamka tu ikiwa utatembea bila kusimama kwa dakika 60 na kikishaamshwa (when it is activated) huendelea kuchoma mafuta mwilini kwa masaa 12 mfulululizo.

Usiseme nikitoka sehemu fulani kwenda sehemu fulani nitakuwa nimetembea vya kutosha, hapana, unahitaji uwe na saa mkononi kuhakikisha kweli dakika 60 zimeisha ukiendelea kutembea bila kusimama. Kama utaweza kukimbia kidogo kidogo (jogging) basi utachoma mafuta ya tumbo kwa haraka zaidi.

Ufanye zoezi hili kila siku kwa mwezi mmoja mpaka miwili mfululizo na mafuta kwenye tumbo lako yatapotea yenyewe bila kupenda.


Tafadhari SHARE post hii kwa ajili ya wengine uwapendao.

Faida na Madhara ya kula pilipili manga

Pilipili manga ni mbegu ndogondogo zenye umbo la mviringo zenye rangi nyeusi.mbegu hizi hutoa ladha ya muwasho mfano kama pilipili na kutumika sana majumbani hasa upande wa jikoni, wapo wanaotumia kiungo hiki kikiwa kizima au kimesagwa inategemea na mtumiaji anavyopendelea. Wanawake wengi wa pwani hutumika pilipili manga katika vyakula ili kunogesha na kukipa ladha iliyo nzuri chakula, kitoweo hata kinywaji. Pia wapo wanaotumia pilipili manga kuramba endapo watahisi kifua kinawabana. Licha ya kuwa pilipili manga si dawa ya kifua ila kwa mazoea tumeipa nafasi pilipili manga kuwa ina uwezo wa kutibu kifua kama ifanyavyo tangawizi. Faida ya matumizi ya pilipili manga kwa wanawake. Pilipili manga ina faida kubwa kwa mwanamke ambaye ameshajifungua, hivyo ni vema uji anaokunywa uwekwe unga wa pilipili manga kwani humsaidia kutoa uchafu utakaokuwa upo kwenye kizazi ambao umebakia. Humuondolea maumivu ya mwili pamoja na tumbo, humsaidia kutoshika mimba katika kipindi hicho ambacho analea mtoto wake mchanga. Wapo baadhi ya watu wakila chakula au mchuzi rosti wa biriani ambayo inakuwa haijachanganywa na kiungo hiki hupata ugonjwa wa kuharisha au kupata maumivu makali ya tumbo. Lakini endapo utaweka pilipili manga kiasi kidogo basi mtu huyo hatoweza kuharisha wala kuumwa na tumbo hivyo kwa upande mwingine kiungo hiki huisaidia kutibu tumbo kwa mlaji. Katika matumizi ya watu wengi inashauriwa itumike pilipili manga ambayo ni nzima ili mtu ambaye inamdhuru akiwa anakula chakula ni lazima ataona vitumba vya pilipili manga na kuviondoa. Madhara ya matumizi ya pilipili manga; Kwa mwanamke anayehitaji kupata mtoto haruhusiwi kutunmia kiungo hicho kwa wingi kwani kinaweza kumsababishia kushindwa kushika ujauzito na hivyo kuhangaika kwa muda mrefu licha ya kutumia dawa za kila aina. Mwanamke yeyote ambaye anahitaji kupata mtoto anatakiwa ajichunge sana na vyakula anavyokula kwani viko vyakula vingine vina uwezo wa kumsababishia kushindwa kushika ujauzito kwa urahisi. Usitumie pilipili manga kutibu kifua. Kiungo hiki kinapoliwa na mgonjwa wa kifua humsababishia kukohoa mara mbili zaidi ya hapo awali. Kutokana na muwasho, kiungo hiki kuingia moja kwa moja kwenye mapafu na kusababisha mkwanguo ambao unaweza kuleta madhara ya mgonjwa kukohoa damu. Wapo wanaotumia maji ya limao na pilipili manga pindi wanapokohoa. Ni vema waache mara moja. hii ni hatari sana. Pia kiungo cha pilipili manga husababisha ugonjwa wa vidonda vya tumbo hasa kwa ambao hupenda kunywa uji uliotiwa pilipili manga kwa wingi wakitumia kama ndio kifungua kinywa. Elewa kuwa utumbo ni laini sana hivyo ni vizuri kujijali hasa katika matumizi ya vyakula vyenye pilipili chache na nyingi kabla ya kula chakula chochote. Hukatazwi kunywa uji wenye pilipili manga ila unatakiwa kuweka kiasi kidogo sana cha kiungo hicho ili kukuepusha na madhara ya vidonda vya tumbo. Angalizo: Wanawake waliokuwa ndani ya ndoa punguzeni matumizi ya pilipili manga na hatimaye ongezeni matumizi ya mdalasini. Mdalasini unaweza kutumiwa kwa jinsi zote ukiwa mapande mapande au umesagwa na kuwa unga. Unga wa mdalasini huchanganywa na asali kisha watumiaji wale kijiko kimoja cha chakula asubuhi, mchana na jioni. Hii itamsaidia sana katika suala la kupata mtoto, watu waliogundua matumizi ya pilipili manga katika kipindi cha kujifungua hawakuwa wajinga kwani kiungo hiki kilikuwa kinatumika enzi na enzi za babu na bibi zetu.

Featured Post

FAIZA ZA KULA PAPAI

 _*Siri usioijua kuhusu utajiri wa tunda la papai katika kukulinda na magonjwa hatarishi kutokana na faida zake lukuki*_  Hizi ndizo FAIDA 1...