Tuesday, June 13, 2017

JINSI YA KUONDOA CHUNUSI KWA NJIA YA ASILI

JINSI YA KUONDOA CHUNSI KWA NJIA YA ASILI

Magadi Soda:
Magadi soda ni mazuri sana kwa kusafishia uso na haswa ukiwa na chunusi. Changanya kiasi kidogo cha magadi soda na maji ya kutosha kuunda kidonge kidogo na kisha weka au kandika kidonge icho sehemu ilio athirika na chunusi. Kwa muda wa dakika 15-20 au mpaka ikauke, na kisha suuza kwa maji yasiwe ya moto. Unaweza kurudia rudia mara kadhaa kwa siku mpaka utakapo ona athari ya chunusi imepotea.

Matango:
Unaweza kutumia Tango kwa kuondoa chunusi na hata kuondoa mabaka mabaka katika ngozi na kuifanya ngozi yako kuonekana yenye afya na yenye kuvutia.
mazuri sana kwa kusafishia uso na haswa ukiwa na chunusi. Kata tango na kasha liponde ponde (unaweza kutumia blenda) kisha paka au kandika usoni. Wacha ikae kwa muda wa dakika 15-20  kisha suuza kwa maji baridi. Unaweza kurudia kwa siku mara mbili mpaka mara tatu kwa siku.

Kitunguu Thaumu:
Unaweza kutumia kitunguu thaumu. Kuondoa chunusi. Matumizi ya Kitunguu thaumu, uleta matokeo mazuri sana katika kuondoa chunusi usoni na hata kuuwa bacteria sababu ina kemikali (antiseptiki) inayozuia kukua kwa bakteria kwenye jeraha au ngozi iliyo athirika kwa chunusi au hata kwenye kidonda. Na pia ina viwango vya juu wa salfa (ni zuri kwa ajili kukausha mafuta kwenye ngozi ya mwili). Twanga kitungu thaumu, au unaweza kukata nusu na kubandika sehemu iliyo na chunusi shikilia kwa dakika 5-10, na kisha safisha na maji baridi. Waweza kufanya ivyo asubuhi na jioni.

Mnana (Peppermint):
Unaweza kutumia majani ya Mnanaa kuondoa chunusi usoni.
Majani ya manna utumika hata kwa wale wenye matatizo ya Mba kwenye kichwa. Twanga majani machache au saga kisha weka sehemu iliyo athirika. Wacha mpaka pakauke na kisha safisha kwa maji baridi. Unaweza kufanya hivyo mara kadhaa kwa siku.

Matumizi ya Limao:
Kata limao na kisha kwa kutumia kijiti chenye pamba kiloweke kwa maji ya limao, sugua sehemu yenye chunusi, kisha wacha pakauke, unaweza kurudia rudi kila baada ya masaa kadhaa. Usitumie maji ya limao ya kwenye chupa, kwa sababu yameweka vihifadhi kemikali zingine kiasi cha kuondoa ubora wa kemikali halisi za kwenye limao. Tumia limao alisi.

Kutumia Asali:
Matumizi ya asali ni ya asili na ufanya ngozi, iwe na afya na nyororo. Kwa sababu kwenye asali kuna virutubisho vingi vyenye kazi ya kuua vimelea (bacteria) na kuzuia uchafu na kusinyaa kwa ngozi.
Weka asali kidogo sehemu ilio athirika na iwache kwa muda mrefu kadri uwezavyo. Vilevile unaweza kupaka uso mzima au hata mwili mzima ukitaka. Sababu asali inarutubisha ngozi ya mwili na kuifanya iwe na afya na mwonekano mzuri. Ukisha ridhika na muda wa asali kwenye ngozi yako unaweza kusafisha kwa kutumia maji ya vuguvugu.

Kutumia Papai:
Unaweza kushangaa, lakini matumizi ya papai yameonyesha matokeo mazuri sana katika kuondoa chunusi usoni na kusafisha sehemu zingine za mwili.
Ponda ponda kiasi kidogo cha papai na kisha iwache kwa muda mrefu kadri uwezavyo. Ukisha ridhika na muda unaweza kusafisha kwa kutumia maji ya kawaida. Unaweza kurudia mara kadhaa kila siku kama unataka.

Dawa Ya Meno:
Unaweza kushangaa, lakini ushangazwi na matokeo mazuri ya meno yako kusafishika kwa dawa ya meno.
Kemikali zinazotumika kuuwa Bakteria wa kwenye meno, pia zina uwezo wa kupambana na bakteria wengine. Tumia dawa ya meno isiyo na gel (non-gel) paka kwenye chunusi. Ni vizuri ukatumia usiku wakati wa kwenda kulala, ila si vibaya ukipaka hata muda wa asubuhi au mchana mradi tu uwe na muda wa kutosha wa dawa kukauka ili iweze kufanyakazi vizuri.

Namna nyingine ni kuchanganya dawa ya meno na unga wa mahindi au nganoiuliosagwa na kuwa laini sana. Unaweza kupaka na kuiwacha ikauke kwa dakika tano mpaka 10.
Safisha kwa sabuni. Mchanganyiko huu unasaidia kukausha chunusi.

Matumizi ya Poda:
Unaweza kutumia baby powder kwa kupaka nyakati za usiku wakati wa kwenda kulala na na kuiwacha mpaka asubuhi.

Matumizi ya Mvuke:
Unaweza kutumia mvuke (Steam/vapour) kuondoa mafuta yaliozidi kwenye ngozi ya uso wako. Kwa kujifukisha. Kwa wale ambao hawana mashine wanaweza kujaza sufuria au bakuli kwa maji ya moto na kujifunika kwa taulo uku ukielekeza uso wao kwenye sufuria au bakuli lenye maji yanayotoa mvuke k wa dakika 5-10. Unaweza kufanya hivi pamoja na njia mojawapo nilizo zitaja hapo juu.

Tahadhari:
Njia hizi za Asili, uchukuwa muda kidogo mpaka kuona matokeo ya kuridhisha.
Njia zote hizi kama hazijaleta matokeo mazuri, tafadhali muone daktari wa ngozi au nenda hospitali ilio karibu kwa uchunguzi zaidi wa ngozi yako.

JINSI YA KUJIKINGA NA HOMA YA INI(HEPATITIS B)

HABARI ZENU WADAU WA MAKALA ZANGU?

Leo nimeona nikushirikishe kuhusu UGONJWA WA HOMA YA INI

HOMA YA INI ni UGONJWA unaoambukizwa kwa njia ya VIRUSI ambavyo vikishaingia MWILINI hushambulia INI kabla ya kugeuka kuwa MARADHI SUGU.VIRUSI ivyo vinaitwa HBV - HEPATITIS B VIRUSES.

VIRUSI hivi husambazwa kwa njia ya DAMU au MAJIMAJI mengine ya MWILINI mfano MATE au JASHO.

UGONJWA huu kama haujatibiwa hutengeneza UVIMBE katika INI na kusababisha KANSA ya INI na baadaye KIFO.

JINSI UNAVYOAMBUKIZWA.
Katika maeneo hatari zaidi DUNIANI,virusi vya HEPATITIS B ( HBV ) kwa kawaida husambazwa kutoka kwa MAMA kwenda kwa MTOTO wakati wa kuzaliwa au kutoka kwa MTU mmoja hadi mwingine hususani nyakati za UTOTONI.

Kama ilivyo kwa UKIMWI virusi vya HOMA ya INI navyo huambukizwa kwa njia ya KUJAMIIANA ,MATE,JASHO, na mwingiliano wowote wa DAMU.

NJIA KUU ZA MAAMBUKIZI :-
- Kujamiiana bila kinga.
- Kunyonyana NDIMI ( Denda )
- MAMA mwenye Ugonjwa kumwambikiza MTOTO wakati wa kujifungua.
- Kuchangia DAMU isiyo salama.
- Kuchangia vitu vya ncha kali kama SINDANO ,WEMBE n.k
- Kuchangia MISWAKI .
- Kuchangia TAULO na mwenye Ugonjwa huo.
- Kubadilishana nguo au kukumbatiana wakati mkiwa mnavuja JASHO .

Tafiti zinaonesha kuwa VIRUSI hivi ni HATARI kuliko hata vya UKIMWI kwa sababu vinaweza kuishi NJE ya MWILI wa BINADAMU  ( yaani nje ya mfumo wa damu ) kwa siku SABA.
VIRUSI vya UKIMWI  ( VVU ) havina UWEZO wa kuishi NJE ya mfumo wa DAMU hata kwa DAKIKA moja.

Kutokana na USUGU wa HBV maana yake ni kwamba kama kirusi kipo kwenye NGOZI,kitaendelea kuwa HAI kwa siku SABA na katika kipindi hicho MTU anaweza kuambukizwa kwa njia ya DAMU au JASHO. Kwa wastani kirusi cha HBV kikishaingia MWILINI hupevuka ndani ya SIKU 75.Hata hivyo upo uwezekano wa kupevuka kati ya SIKU 30 hadi SIKU 180.Ndani ya SIKU 30 mpaka SIKU 60, MTU mwenye HBV anaweza kugundulika ikiwa atapimwa.

MTU mwenye HOMA ya INI ana wastani mdogo wa KUISHI kuliko mwenye UKIMWI.

DALILI ZA UGONJWA HUU.
WATU wengi hawaonyeshi DALILI yoyote.
Kwa maana hiyo MTU anaweza kuishi na HBV na kusababisha MAAMBUKIZI kwa WENGINE bila kugundulika.
Hata hivyo WATU wengine husumbuliwa na HOMA KALI na DALILI ambazo hudumu kwa wiki kadhaa. DALILI hizo ni:-
- Uchovu
- Kichefuchefu
- Mwili kuwa dhaifu
- Homa kali
- Kupoteza hamu ya kula
- Kupungua uzito
- Maumivu makali ya tumbo upande wa INI.
- Macho na ngozi kuwa ya njano.
- Mkojo mweusi.
Kwa WAGONJWA wengine, VIRUSI vya HEPATITIS B hukua hadi kusababisha INI kuharibika kabisa ( Cirrhosis of the liver ) au SARATANI ya INI  ( liver cancer  ).

KINGA.
- Chanjo
- Kutumia kinga wakati wa Kujamiiana.
- Kuacha Kuchangia vitu vya ncha kali.
- Kutochangia miswaki.
- Kuwa na mpenzi mmoja mwaminifu.
- Kutochangia damu isiyo salama.

Featured Post

FAIZA ZA KULA PAPAI

 _*Siri usioijua kuhusu utajiri wa tunda la papai katika kukulinda na magonjwa hatarishi kutokana na faida zake lukuki*_  Hizi ndizo FAIDA 1...