Wednesday, June 14, 2017

FAIDA TISA(9) ZA KULA NANASI

FAIDA ZA KULA NANASI KWA AFYA YAKO

Hapa tuta angalia faida kuu za kula nanasi na Wote tunajua kuwa kula matunda mazuri inasaidia mwili kupata vitamin na madini mbalimbali na kuwa mtu mwenye afya njema, na sasa tunda la nanasi ni tunda moja wapo ambalo ni muhimu sana hasa katika msimu huu wa mananasi.

1: Mmeng’enyo wa chakula.

Nanasi linasaidia kurahisisha mmeng’enyo wa chakula kwa kiasi kikubwa sana. Hii inatokana na kuwa nanasi linatoa aina protini katika mwili wako ambayo inarahisisha kazi hii ya kumeng’enya chakula.

2: Nanasi Lina Vitamin na Madini

Tunda la nanasi limejaa madini na protini nyingi ambazo zinafaa kwa mwili wako. Nanasi lina vitamin A Vitamini C calcium, fiber na pia potassium.

3: Kuzuia Kikohozi na Baridi.

Tangu nanasi lina utajiri wa vitamin C linaweza kupigana na virusi amabavyo vinaweza kusababisha kikohozi na ubaridi. Hata kama umeshakuwa na kikohozi nanasi kwa kiasi flan linaweza kukusaidia kupunguza makali. Tunda hili lina madini ya Bromelain ambayo yanauwezo wa kudhoofisha virusi vya kikohozi. Wakati unaumwa kula tunda la nanasi hata wakati unakuwa kwenye dozi ya dawa ambazo umepewa na daktari linaweza kukusaidia sana kuharakisha kupona haraka.

4: Kuimarisha Mifupa.

Je unahisi mifupa yako sio imara? Basi anza kula nanasi. Nanasi pia lina uwezo wa kuimarisha mifupa nakuifanya kuwa yenye nguvu. Hii ni kwa sababu nanasi lina madini ya manganese ambayo mwili wako unahitaji madini haya ili kwa ajili ya kuimarisha mifupa yako. Tena kama ukinywa kikombe kimoja tu cha juice ya nanasi unakua umeongeza asilimia 73% ya madini ya manganese ambayo ni hata zaidi ya mwili unavyoihitaji kitu ambacho ni kizuri kwa afya ya mifupa ya mwili wako. Unakua na mifupa iliyokomaa.

5: Huimarisha Meno yako.

Watu kila mara huwa wanajali sana meno yao, na mara nyingine huwa wanashindwa kuyapa kipaumbele kwa saaana. Kama una matatizo ya meno basi unashauriwa kula nanasi kwa sababu nanasi linasaidia kuimarisha magego ambayo yanashikiria meno. Kula tunda la nanasi linakufanya kuimarisha magego yanayoshikiria meno na pia meno yenyewe yanaimarika.

6: Huzuia Ugonjwa wa Asthma.

Ukila nanasi unajiweka katika hali nzuri ya kuto pata ugonjwa wa asthma. Watu wanaokula nanasi wanakua katika hali nzuri kwa sababu nanasi lina vitamin aina ya Beta Carotene ambayo linausaidia mwili kukabiliana na magonjwa mbali mbali ikiwemo asthma.

7: Blood Pressure.
Unapokula nanasi unaongeza potassium na pia kula matunda mengine yenye madini ya potassium yanaweza kukusaidia kupunguza uwezekano wa kupata blood pressure.

8. Kansa.
Kama kawaida nanasi lina utajili mkubwa wa vitamin C. Hii vitamin C inauwezo wa kuzuia virusi ambavyo vinaweza kukusababishia magonjwa mabali mabli ya kansa.

9. Huimarisha Afya ya Moyo.

Utajiri wa madini ya fiber, potassium na vitamin C ni mojawapo ya faida za tunda hili ambazo pia zina uwezo wa kuimarisha afya ya moyo wako na kuzuia maradhi yanayoweza kuuadhiri moyo wako.

Sasa jamani tuanze kula tunda la nanasi ili tuweze kufaidi madini ya na vitamin zilizojaa katika tunda hili. ili kuepuka magonjwa ya baadaee. 

Endelea ku subscribe blog hii kwa Habari zaidi. >>>>>>>>

FAHAMU MWANAMKE ANAVOPATA MIMBA

FAHAMU JINSI MWANAMKEE ANAVYO PATA MIMBA

Wengi hasa wanawake wamekuwa wakiuliza maswali mengi sana kuhusuana na jinsi ya mwanamke kupata mimba au kuzuia kutopata mimba.
Naamini maelezo yafuatayo ukisoma kwa makini unaweza kupata ufahamu na kujibiwa maswali yako yote ambayo yamekuwa yanakutatiza.
Pia ni vizuri kuzingatia na kutochanganya Kalenda ya menstrual cycle tunayoongelea hapa na ile 'kalenda ya mwaka' inayohusu tarehe za miezi 12 ya mwaka ambayo huwa tunaitundika ukutani huko nyumbani na maofisini kwetu!

Wanawake wamegawanyika katika makundi makubwa 4 linapokuja suala la siku za hedhi

Mzunguko mfupi yaani siku 22
Mzunguko wa kati yaani siku 28
Mzunguko mrefu yaani siku 35
Na mzunguko abnormal siku 15

Kama mwanamke ana menstruation cycle ya siku 22 inabidi afanye kama ifuatavo:

Kwanza itabidi atengeneze kalenda yake mwenyewe ya siku zake zote za menstruation cycle kama hapa chini:
1st, 2nd, 3rd, 4th, 5th, 6th, 7th, 8th, 9th, 10th, 11th, 12th, 13th, 14th, 15th, 16th, 17th, 18th, 19th, 20th, 21st, 22nd.

Kisha ahesabu kuanzia ile 22nd day kurudi nyuma mpaka afikishe siku 15.
Ataona kuwa siku ya kumi na tano inaangukia kwenye 8th day ya kalenda yake.
Hivyo 8th day ndiyo siku ya mimba kwa mwanamke yeyote ambaye ana menstration cycle ya siku 22.
Akumbuke kwamba 1st day ndiyo siku anayoanza ku-bleed!

Kama mwanamke ana menstruation cycle ya siku 28 inabidi afanye kama ifuatavo:
Kwanza itabidi atengeneze kalenda yake mwenyewe ya siku zake zote za menstration cycle kama hapa chini:
1st, 2nd, 3rd, 4th, 5th, 6th, 7th, 8th, 9th, 10th, 11th, 12th, 13th, 14th, 15th, 16th, 17th, 18th, 19th, 20th, 21st, 22nd, 23rd, 24th, 25th, 26th, 27th, 28th.

Kisha ahesabu kuanzia ile 28th day kurudi nyuma mpaka afikishe siku 15.
Ataona kuwa siku ya kumi na tano inaangukia kwenye 14th day.
Inamaana kwamba 14th day ndiyo siku ya mimba kwa mwanamke yeyote ambaye ana menstruation cycle ya siku 28.
Akumbuke kwamba 1st day ndiyo siku anayoanza ku-bleed!
Kama mwanamke ana menstruation cycle ya siku 35 inabidi afanye kama ifuatavo:
Kwanza itabidi atengeneze kalenda yake mwenyewe ya siku zake zote za menstruation cycle kama hapa chini:
1st, 2nd, 3rd, 4th, 5th, 6th, 7th, 8th, 9th, 10th, 11th, 12th, 13th, 14th, 15th, 16th, 17th, 18th, 19th, 20th, 21st, 22nd, 23rd, 24th, 25th, 26th, 27th, 28th, 29th, 30th, 31st, 32nd, 33rd, 34th, 35th.

Kisha ahesabu kuanzia ile 35th day kurudi nyuma mpaka afikishe siku 15.
Ataona kuwa siku ya kumi na tano inaangukia kwenye 21st day.
Inamaana kwamba 21st day ndiyo siku ya mimba kwa mwanamke yeyote ambaye ana menstruation cycle ya siku 35.
Akumbuke kwamba 1st day ndiyo siku anayoanza ku-bleed!
Kama mwanamke ana abnormal menstruation cycle ya siku 15

BASI KUNAUWEZEKANO WA KUTOPATA MIMBA KABISA KAMA INAVYOONEKANA HAPA CHINI:

Kwanza itabidi atengeneze kalenda yake mwenyewe ya siku zake zote za menstruation cycle kama kawaida:
1st, 2nd, 3rd, 4th, 5th, 6th, 7th, 8th, 9th, 10th, 11th, 12th, 13th, 14th, 15th.
Kisha ahesabu kuanzia ile 15th day kurudi nyuma mpaka afikishe siku 15.
Ataona kuwa siku ya kumi na tano inaangukia kwenye 1st day.
Inamaana kwamba, the 1st day of her bleeding ndiyo siku ya mimba kwa mwanamke yeyote ambaye ana menstruation cycle ya siku 15.
Akumbuke kwamba 1st day ndiyo siku anayoanza ku-bleed, na ndiyo hiyo hiyo siku ambayo mwanamke wa kundi hili anaweza kupata mimba!
Hii inamaana kwamba, siku ambayo linaharibika lile yai la upande mmoja ndiyo siku hiyo hiyo ambayo yai la upande wa pili linapevuka tayari kwa kurutubishwa.
Mwanamke wa aina hii anaweza kupata mimba tu kama atakutana na mwanaume siku ile anayoanza kubleed, kwani siku ambayo yai moja linaanza kuharibika ndio siku hiyo hiyo ambayo yai la upande wa pili linakuwa tayari kurutubishwa
Na wanawake wa kundi hili la nne ukiwauliza vizuri watakiri kwamba hawajawahi kuona au ku-feel ule ute mweupe ambao wenzao huwa wanaupata siku ile yai linapokuwa tayari kwa kurutubishwa, kwani ute wa wanawake wa kundi hili la nne huwa unachanganyikana na damu kwa vile unatoka siku ile ile wanapoanza ku-bleed.Pia wanawake wa kundi hili huwa wanatokwa na kiasi kidogo sana cha damu na bleed hukatika ndani ya siku moja au mbili tu!

Endelea kuwa pamoja nami na unaweza share na wenzako walitambue hili...

Featured Post

FAIZA ZA KULA PAPAI

 _*Siri usioijua kuhusu utajiri wa tunda la papai katika kukulinda na magonjwa hatarishi kutokana na faida zake lukuki*_  Hizi ndizo FAIDA 1...