Saturday, June 17, 2017

TATIZO LA KUTOPATA CHOO(CONSTIPATION)

#CONSTIPATION/TATIZO LA KUTOPATA CHOO.

#KAMA UNAPATA CHOO MARA 1 KWA SIKU NA UNAKULA MARA 3,UPO KWENYE HATARI YA KUPATA MAGONJWA YAFUATAYO....….…..

~Kansa ya Utumbo.
~Uzito uliozidi.
~Bawasiri(Vinyama sehemu ya haja kubwa).
~Kifo.
~Maumivu ya Kiuno,Mgongo,Mabega,Kichwa,Misuli.
~Kukosa usingizi(Insomnia)
~Kukosa hamu ya kula(Loss of appetite).
~Tumbo kuja gesi.
~Vidonda vya tumbo(Ulcers).
~Upungufu wa nguvu za kiume.
~Kushindwa kubeba mimba  au kuzaa.
~Kupasuka kwa utumbo.
~Ileocecal valve incompetence.
~Kutoa harufu mbaya mdomoni na unapojamba.

Soma zaidi hapa.............
Kati ya changamoto ya kiafya niliyokua nayo,ni kutopata choo na kupata choo kigumu kama cha mbuzi,na nilidhani ni kawaida kutopata choo kwa muda wa siku 3 hadi week,kumbe ni tatizo kubwa linaloweza kusababisha 90% ya magonjwa yasiyoambukizwa na hatimae vifo.

#WATU wengi wanasumbuliwa na tatizo hili ambalo huwafanya kuwa na uoga na aibu wa kuelezea na kushindwa hata kwenda hospital kupata tiba.

#CHANZO CHA TATIZO
Tatizo la kutopata choo linasababishwa na mfumo mbovu wa mmeng'enyo wa chakula.

Kwenye utumbo mdogo ambao una urefu wa takribani mara 10 mpaka 13 ya urefu wa mtu husika,kuna Villars, hivi ni kama vidole vinavyokua vinachezacheza ili kumeng'enya chakula,ila kutokana na sumu tunazoingiza mwilini kila siku kutoka kwenye vinywaji,chakula,dawa na hewa,pamoja na mafuta tunayokula kwenye vyakula,zinaenda kujipachika katikati ya Villars (vidole) na hivyo kusababisha vidole visimame(blocked) hivyo chakula hakimeng'enywi na kusababisha chakula unachokula kupitiliza moja kwa moja kwenye utumbo mkubwa,na hapo ndio tatizo linapoanzia.
Na tatizo hili ndio hupelekea kupata tatizo la bawasiri.

#JE, UNAJUA BAWASIRI/HEMORRHOIDS NI NINI????!!

~Ni ugonjwa unaotokana na kuathirika kwa mishipa ya damu ya ndani na Inje ya sehemu ya haja kubwa na wakati mwingine mishipa hiyo huweza kupasuka/kuteleza na kuvuja damu kwenye njia ya haja kubwa na kasababisha kutoka kinyama au uvimbe.

~ugonjwa huu wa bawasiri kwa lugha ya kitaalamu tunauita HEMORRHOIDS ilhali kwa lugha ya kingereza unafahamika kama piles.

~tatizo hili huwaathiri watu wote ila zaidi huwaathiri watu wazima kuliko watoto na inakadiriwa kuwa karibu 50%ya watu wote wako katika hatari ya kupata tatizo hili katika umri wa miaka 30_50

#AINA ZA BAWASIRI

~Kuna Aina mbili za bawasiri

(A) BAWASIRI YA NDANI

~Aina hii ya bawasiri hutokea ndani ya mfereji wa haja kubwa huwa haiambatani na maumivu na wengi huwa hawajitambui kuwa Wana tatizo hili

~Aina hii hutokana na kuvimba na kuharibika kwa mshipa wa artery za ndani ya mfereji wa haja kubwa

(B)BAWASIRI YA NNJE

~Aina hii ya bawasiri hutokea katika eneo la mwisho kabisa la mfereji wa haja kubwa na huambatana na maumivu makali na kuwashwa kwa ngozi katika eneo la tundu Hilo pia husababisha mishipa ya damu (vena) kupasuka na damu kuganda na kasababisha Aina ya bawasiri iitwayo THROMBOSED HEMORRHOIDS

#CHANZO CHA TATIZO

~chanzo halisi cha ugonjwa huu hakijapatikana ila Kuna vitu ambavyo huwa chanzo cha kupata ugonjwa wa bawasiri ambayo ni

°Kufanya mapenzi kinyume na maumbile.
°Kuharisha kwa muda mrefu.
°Tatizo la kutopata choo.
°Matatizo ya umri.
°Shughuri ya kukaa kwa muda mrefu sana.
°Uzito kupita kiasi.
°Matumizi ya vyoo vya kukaa kwa muda mrefu.
°Vyakula vyenye mafuta kwa wingi.
°Vinywaji vikali kama pombe,kahawa,viroba.
°Kutokula vyakula vya nyuzi nyuzi.
°Kutokunywa maji ya kutosha.
°Vyakula vya ngano,wanga na vilivyokobolewa.
°Kutofanya shughuli yoyote baada ya kula.
°Kulala kabla ya masaa 4 baada ya kula usiku.

#DALILI ZA KUTOPATA CHOO NA BAWASIRI.

√ Ngozi kuwasha katika eneo la tundu la haja kubwa.
√ kupata maumivu makali wakati wa kujisaidia.
√ kutokea uvimbe/kinyama katika eneo la tundu la haja kubwa.
√kinyesi kuwa na damu na kunuka harufu mbaya sana.
√ Kinyesi cha makundi makundi kama cha mbuzi.
√ Kuhisi moto wakati wa kujisaidia.
√ Kutopata choo kwa siku 2 na kuendelea.
√ Tumbo kujaa gesi na kujisaidia hewa.
√ Kuhisi maumivu ukikaa.
√ Kusinzia baada tu ya kula
√ Tumbo kuunguruma.
√ Kujamba kila wakati.
√ Kukosa hamu ya kula.
√ Mkojo wenye rangi(ambao sio mweupe kama maji)

#MATIBABU NA JINSI YA KUEPUKA TATIZO LA BAWASIRI NA KUTOKUPATA CHOO.

~matibabu ya bawasiri hutegemea na Aina ya bawasiri pia tiba iliyozoeleka ni kukatwa kinyama na kuendelea na lishe ya chakula,kama kula matunda,mboga za majani,maji kwa wingi, hata hvyo tiba hii si nzuri kwasababu huwa haitibu chanzo cha tatizo hivyo huwa rahisi kujirudia.

#MADHARA YA TATIZO LA KUTOPATA CHOO NA BAWASIRI.

-kupata upungufu wa damu (anemia).
-Kupata tatizo la kutokuweza kuhimili choo.
-hupunguza nguvu za kiume na kuondoa hamu ya tendo la ndoa kwa wanawake.
-kuathirika kisaikolojia
- kukosa moral ya kufanya Kazi kutokana na maumivu makali.
- Kupasuka kwa utumbo na kusababisha kifo.
- Kitambi na uzito uliopindukia.
- Kansa ya Utumbo.
- Kukosa uwezo wa kubeba mimba.
- Na mengine yoote niliyoyataja mwanzo wa post.

Na Kwa ushauri zaidi juu ya nini ufanye kama una tatizo hilo,na kwa lengo la kujikinga,usikose makala ijayo

No comments:

Post a Comment

Featured Post

FAIZA ZA KULA PAPAI

 _*Siri usioijua kuhusu utajiri wa tunda la papai katika kukulinda na magonjwa hatarishi kutokana na faida zake lukuki*_  Hizi ndizo FAIDA 1...