Saturday, October 26, 2024

FAIZA ZA KULA PAPAI


 _*Siri usioijua kuhusu utajiri wa tunda la papai katika kukulinda na magonjwa hatarishi kutokana na faida zake lukuki*_


 Hizi ndizo FAIDA 10 za kiafya za kula papai

1️⃣ Papai ni katika matunda yanayojenga afya sana kwenye mwili wa binadamu. Papai lina *vitamin C na vitamini A* kwa wingi pia kuna *potassium na folate.* Pia tafiti zinaonesha kuwa *antioxidant aina ya lycopene* iliyomo kwenye papai *husaidia katika kuzuia kupata saratani.* 


2. Tunda hili pia lina *vitamin B, vitamin E na vitamin K.* Pia lina *madini ya calsium (kashiam) potassium, mgnessium na copper.* Pia punje za papai ni *dawa kwa baadhi ya matatizo ya ini na figo.* Pia kwenye papai kuna *protelytic enzymes hii husaidia katika kuuwa bakteria na minyoo pamoja na wadudu wengine hatari ndani ya tumbo (mfumo wa kumeng’enya chakula).* 


3️⃣ Papai linatambulika kwa kuwa na *uwezo wa kuulinda mwili na maradhi ya uzee kama macho, misuli na kuzeeka kwa haraka.* Ndani ya papai kuna *Zeaxanthin hii ni anti oxidant ambayo inakazi ya kuchuja miale hatari ya jua.* Pa inaaminika kuwa *antioxidant hizi husaidia katika afya ya macho na husaidia katika kudhibiti kudhoofu kwa misuli.* 


4️⃣ Vilevile papai huaminika kusaidia kupunguza *hatari ya kuwa na ugonjwa wa pumu.* Hupunguza hatari ya kuugua pumu. Ndani ya papai kuna virutubisho vingi, lakini uwepo wa *beta-carotene ndani ya papai husaidia kwa wagonjwa wenye pumu.* 


5️⃣Ulaji wa antioxidanti zilizopo kwenye papai mfano *beta-carotene* *husaidia katika kupunguza athari za kupata maradhi ya saratani kwa vijana* . Ulaji wa tunda hili husaidia katika *kudhibiti upatikanaji wa saratani ya kwenye via vya uzazi hasa saratani ya korodani.* 

6. Pia papa Lina kiwango kikubwa Cha fibres (nyuzi na kambakamba) zinazosaidia kurahisisha mmeng'enyo wa chakula na kufanya mtumiaji kutopata choo kigumu (Constipation)

 *Hitimisho:* 

Nimalizie kwa kusema kuwa matunda ni dawa. Ni vyema kujitahidi kula matunda na mboga za majani mara kwa mara. Pia viungio vya mboga kama vitunguu, tangawizi, bamia na karoti viungio hivi ni muhimu sana.

No comments:

Post a Comment

Featured Post

FAIZA ZA KULA PAPAI

 _*Siri usioijua kuhusu utajiri wa tunda la papai katika kukulinda na magonjwa hatarishi kutokana na faida zake lukuki*_  Hizi ndizo FAIDA 1...