Saturday, June 17, 2017

TATIZO LA UKOSEFU WA NGUVU ZA KIUME NA CHANZO CHAKE

...
LIFAHAMU TATIZO LA #UKOSEFU WA NGUVU ZA #KIUME NA CHANZO CHAKE.

Leo katika zama hizi za sayansi na teknolojia tatizo la kupungua nguvu za kiume limekuwa kubwa sana, siyo Tanzania tu, bali duniani kote. Jambo muhimu analopaswa mwanaume yeyote kufahamu ni kwamba, kupungua nguvu za kiume siyo ugonjwa, ni dalili ya ugonjwa. Hii ina maana kuna dosari au udhaifu wa kiutendaji ndani ya mwili wake. 

Kuna sababu nyingi mno zinazosababisha mwanaume apungue nguvu za kiume. Mtu aweza kujiuliza kwa nini kuwe na sababu nyingi namna hiyo?

Kwani nguvu za kiume ni nini?

Nguvu za kiume ni jina la jumla lenye vipengele vingi ndani yake ikiwa ni pamoja na hamu ya mapenzi; kusimama kwa uume barabara; kuchelewa kufika kileleni kiasi cha kufurahia tendo la ndoa; uwezo wa kurudia tendo la ndoa; pumzi, wepesi na uchangamfu wa mwili katika kutenda tendo  lenyewe.

Ni viungo gani vinavyohusika na nguvu za kiume?

Nguvu za kiume ni tukio pana sana lenye kuhusisha viungo na vitu vingi ndani ya mwili. Kuna zaidi ya viungo na vitu 50 ndani ya mwili wa mwanaume vinavyohusika na nguvu za kiume ambapo viungo hivi pia hufanya kazi zingine za mwili. Baadhi ya viungo hivyo ni ubongo, moyo, mishipa ya neva mishipa ya ateri, mirija iliyo ndani ya uume iitwayo corpora cavernosa.

Viungo vingine ni neva maalumu za parasympathetic, tezidume (prostate gland), ini, figo, homoni ya testestorone, kemikali za  acetylcholine, serotonin, na dopamine, uti wa mgongo, eneo la chini ya mgongo (kiuno), eneo la nyonga.

Viungo vingine ni misuli maalumu iitwayo pelvic floor, tezi pituitari (pituitary gland), utando maalumu wa uumeni uitwao tunica albuginea, misuli iitwayopubococcygeus [PC muscles], kemikali ya nitric oxide, kemikali ya prolactin n.k.
Nadhani unaona jinsi ilivyo vitu vingi.

Nini maana ya kupungua nguvu za kiume?

Unapopungua nguvu za kiume ina maana ndani ya mwili wako kuna baadhi ya vitu katika vitu nilivyovitaja hapo juu havifanyi kazi vizuri jinsi ipasavyo na inavyotakiwa. Yawezekana ni figo ndilo halifanyi kazi vizuri, au ini, au tezi dume, au neva ya parasympathetic, au moyo una tatizo au mishipa ya ateri, au misuli ya pelvic au homoni fulani iko juu sana au iko chini sana (hormonal imbalance), orodha ni ndefu sana.

Kitendo cha baadhi ya viungo hivyo kutofanya kazi vizuri basi hapo hutokea upungufu katika nguvu za kiume. Upungufu huo unaweza kuwa ni:

1. Kukosa hamu ya mapenzi; au

2. Uume kusimama kwa uregevu; au

3. Kuwahi kufika kileleni; au

4. Kuchelewa sana kufika kileleni (au kushindwa kufika kileleni kabisa); au

5. Kushindwa kurudia tendo la ndoa; au

6. Kuhisi maumivu wakati wa tendo la ndoa au baada ya tendo hilo; au

7. Kukosa pumzi na uchangamfu wa mwili katika utendaji; au

8. Kuchoka sana baada ya tendo la ndoa na hata kukinai kabisa au hata kusikia kichefuchefu;

Ili uelewe vizuri zaidi labda niseme kwamba, nguvu za kiume ni kama kiwanda; na ni zaidi ya kiwanda. Ndani ya kiwanda kuna umeme, maji, madawa, watu (wafanyakazi wa kila taaluma na fani), mashine, mitambo n.k.

Ikitokea kitu kimojawapo kukosekana, mathalani umeme, au wafanyakazi wakagoma, au kukakosekana madawa muhimu au maji na kadhaa wa kadha, basi bidhaa inayotarajiwa kupatikana sokoni, kwa hakika haitapatikana.

Vivyo hivyo nguvu za kiume, mathalani, ikitokea tezi dume kutofanya kazi vyema, basi hapo mwanaume hatoona nguvu za kiume, zitapungua au zitaisha kabisa!

Kwa hiyo upungufu wa nguvu za kiume ni upungufu au kasoro za kiutendaji wa viungo ndani ya mwili wa mwanaume. Mwanaume yoyote anapaswa kutambua jambo hili.

Lakini nini kinachopelekea viungo hivyo vishindwe kufanya kazi vizuri?

Kuna maradhi kadhaa, vyakula tunavyokula, tabia na mtindo wa maisha vinavyoweza kupelekea viungo hivyo kutofanya kazi vizuri. Baadhi ya maradhi hayo na tabia hizo ni kujichua/punyeto (masturbation) kwa muda mrefu; kisukari; presha ya kupanda; presha ya kushuka; uvutaji wa sigara; unywaji wa pombe; madawa ya kulevya; kufanya kazi kupita kiwango na kukosa muda wa kupumuzika; matatizo ya kukosa usingizi na kuchelewa kulala usiku.

Uume wako unatakiwa usimame kwenda juu siyo usimame kwenda mbele tu au kurudi chini. Na ukielekea juu uwe umenyooka kama rula usijikunje kama ndizi maana ukijikunja hilo ni tatizo la kitu kinachoitwa plaque kuganda kwenye uume. See? Ndo maana tunaelimishana rafiki. Tatizo la nguvu za kiume ni pana sana.

Hata hivyo kuna vitu unaweza kufanya ili kurejesha nguvu zako za kiume.

Usilee tatizo. Madhara ni makubwa mno likiendelea kwa muda mrefu!

Mawasiliano haya hapa.

#WhatsApp +255620204770

TATIZO LA KUTOPATA CHOO(CONSTIPATION)

#CONSTIPATION/TATIZO LA KUTOPATA CHOO.

#KAMA UNAPATA CHOO MARA 1 KWA SIKU NA UNAKULA MARA 3,UPO KWENYE HATARI YA KUPATA MAGONJWA YAFUATAYO....….…..

~Kansa ya Utumbo.
~Uzito uliozidi.
~Bawasiri(Vinyama sehemu ya haja kubwa).
~Kifo.
~Maumivu ya Kiuno,Mgongo,Mabega,Kichwa,Misuli.
~Kukosa usingizi(Insomnia)
~Kukosa hamu ya kula(Loss of appetite).
~Tumbo kuja gesi.
~Vidonda vya tumbo(Ulcers).
~Upungufu wa nguvu za kiume.
~Kushindwa kubeba mimba  au kuzaa.
~Kupasuka kwa utumbo.
~Ileocecal valve incompetence.
~Kutoa harufu mbaya mdomoni na unapojamba.

Soma zaidi hapa.............
Kati ya changamoto ya kiafya niliyokua nayo,ni kutopata choo na kupata choo kigumu kama cha mbuzi,na nilidhani ni kawaida kutopata choo kwa muda wa siku 3 hadi week,kumbe ni tatizo kubwa linaloweza kusababisha 90% ya magonjwa yasiyoambukizwa na hatimae vifo.

#WATU wengi wanasumbuliwa na tatizo hili ambalo huwafanya kuwa na uoga na aibu wa kuelezea na kushindwa hata kwenda hospital kupata tiba.

#CHANZO CHA TATIZO
Tatizo la kutopata choo linasababishwa na mfumo mbovu wa mmeng'enyo wa chakula.

Kwenye utumbo mdogo ambao una urefu wa takribani mara 10 mpaka 13 ya urefu wa mtu husika,kuna Villars, hivi ni kama vidole vinavyokua vinachezacheza ili kumeng'enya chakula,ila kutokana na sumu tunazoingiza mwilini kila siku kutoka kwenye vinywaji,chakula,dawa na hewa,pamoja na mafuta tunayokula kwenye vyakula,zinaenda kujipachika katikati ya Villars (vidole) na hivyo kusababisha vidole visimame(blocked) hivyo chakula hakimeng'enywi na kusababisha chakula unachokula kupitiliza moja kwa moja kwenye utumbo mkubwa,na hapo ndio tatizo linapoanzia.
Na tatizo hili ndio hupelekea kupata tatizo la bawasiri.

#JE, UNAJUA BAWASIRI/HEMORRHOIDS NI NINI????!!

~Ni ugonjwa unaotokana na kuathirika kwa mishipa ya damu ya ndani na Inje ya sehemu ya haja kubwa na wakati mwingine mishipa hiyo huweza kupasuka/kuteleza na kuvuja damu kwenye njia ya haja kubwa na kasababisha kutoka kinyama au uvimbe.

~ugonjwa huu wa bawasiri kwa lugha ya kitaalamu tunauita HEMORRHOIDS ilhali kwa lugha ya kingereza unafahamika kama piles.

~tatizo hili huwaathiri watu wote ila zaidi huwaathiri watu wazima kuliko watoto na inakadiriwa kuwa karibu 50%ya watu wote wako katika hatari ya kupata tatizo hili katika umri wa miaka 30_50

#AINA ZA BAWASIRI

~Kuna Aina mbili za bawasiri

(A) BAWASIRI YA NDANI

~Aina hii ya bawasiri hutokea ndani ya mfereji wa haja kubwa huwa haiambatani na maumivu na wengi huwa hawajitambui kuwa Wana tatizo hili

~Aina hii hutokana na kuvimba na kuharibika kwa mshipa wa artery za ndani ya mfereji wa haja kubwa

(B)BAWASIRI YA NNJE

~Aina hii ya bawasiri hutokea katika eneo la mwisho kabisa la mfereji wa haja kubwa na huambatana na maumivu makali na kuwashwa kwa ngozi katika eneo la tundu Hilo pia husababisha mishipa ya damu (vena) kupasuka na damu kuganda na kasababisha Aina ya bawasiri iitwayo THROMBOSED HEMORRHOIDS

#CHANZO CHA TATIZO

~chanzo halisi cha ugonjwa huu hakijapatikana ila Kuna vitu ambavyo huwa chanzo cha kupata ugonjwa wa bawasiri ambayo ni

°Kufanya mapenzi kinyume na maumbile.
°Kuharisha kwa muda mrefu.
°Tatizo la kutopata choo.
°Matatizo ya umri.
°Shughuri ya kukaa kwa muda mrefu sana.
°Uzito kupita kiasi.
°Matumizi ya vyoo vya kukaa kwa muda mrefu.
°Vyakula vyenye mafuta kwa wingi.
°Vinywaji vikali kama pombe,kahawa,viroba.
°Kutokula vyakula vya nyuzi nyuzi.
°Kutokunywa maji ya kutosha.
°Vyakula vya ngano,wanga na vilivyokobolewa.
°Kutofanya shughuli yoyote baada ya kula.
°Kulala kabla ya masaa 4 baada ya kula usiku.

#DALILI ZA KUTOPATA CHOO NA BAWASIRI.

√ Ngozi kuwasha katika eneo la tundu la haja kubwa.
√ kupata maumivu makali wakati wa kujisaidia.
√ kutokea uvimbe/kinyama katika eneo la tundu la haja kubwa.
√kinyesi kuwa na damu na kunuka harufu mbaya sana.
√ Kinyesi cha makundi makundi kama cha mbuzi.
√ Kuhisi moto wakati wa kujisaidia.
√ Kutopata choo kwa siku 2 na kuendelea.
√ Tumbo kujaa gesi na kujisaidia hewa.
√ Kuhisi maumivu ukikaa.
√ Kusinzia baada tu ya kula
√ Tumbo kuunguruma.
√ Kujamba kila wakati.
√ Kukosa hamu ya kula.
√ Mkojo wenye rangi(ambao sio mweupe kama maji)

#MATIBABU NA JINSI YA KUEPUKA TATIZO LA BAWASIRI NA KUTOKUPATA CHOO.

~matibabu ya bawasiri hutegemea na Aina ya bawasiri pia tiba iliyozoeleka ni kukatwa kinyama na kuendelea na lishe ya chakula,kama kula matunda,mboga za majani,maji kwa wingi, hata hvyo tiba hii si nzuri kwasababu huwa haitibu chanzo cha tatizo hivyo huwa rahisi kujirudia.

#MADHARA YA TATIZO LA KUTOPATA CHOO NA BAWASIRI.

-kupata upungufu wa damu (anemia).
-Kupata tatizo la kutokuweza kuhimili choo.
-hupunguza nguvu za kiume na kuondoa hamu ya tendo la ndoa kwa wanawake.
-kuathirika kisaikolojia
- kukosa moral ya kufanya Kazi kutokana na maumivu makali.
- Kupasuka kwa utumbo na kusababisha kifo.
- Kitambi na uzito uliopindukia.
- Kansa ya Utumbo.
- Kukosa uwezo wa kubeba mimba.
- Na mengine yoote niliyoyataja mwanzo wa post.

Na Kwa ushauri zaidi juu ya nini ufanye kama una tatizo hilo,na kwa lengo la kujikinga,usikose makala ijayo

Featured Post

FAIZA ZA KULA PAPAI

 _*Siri usioijua kuhusu utajiri wa tunda la papai katika kukulinda na magonjwa hatarishi kutokana na faida zake lukuki*_  Hizi ndizo FAIDA 1...