Friday, July 28, 2017

FAIDA 48 ZA JUISI YA TANGAWIZI AMBAZO WENGI HAMZIFAHAMU

FAIDA 48 ZA JUISI YA TANGAWIZI AMBAZO ULIKUWA HUZIJUI

1. Huondoa sumu mwilini haraka sana
2. Huua bakteria wa aina nyingi mwilini hata salmonella ndani ya mwili hata juu ya ngozi
3. Kuna viua vijisumu (antibiotics) vya asili viwili kwenye tangawizi
4. Huondoa uvimbe mwilini
5. Huondoa msongamano mapafuni
6. Tangawizi inayo ‘zingibain’ ambayo huua vimelea mbalimbali vya magonjwa na mayai yake
7. Huondoa maumivu ya koo
8. Huua virusi wa homa
9. Huondoa maumivu mbalimbali mwilini
10. Huondoa homa hata homa ya baridi (chills)
11. Hutibu saratani ya tezi dume. Tangawizi huua kimeng’enya ambacho ni chakula cha seli za kansa ya tezi dume kiitwacho ‘5-LO enzymes’ na seli hizo za kansa hufa ndani ya masaa mawili au manne bila hicho kimeng’enya.
12. Tangawizi ina kiinilishe muhimu sana ambacho huzuia kuongezeka kwa seli za kansa ya kongosho kiitwacho kwa kitaalamu kama ‘gingerol”
13. Hutibu kansa zinazoweza kusababishwa na kupata choo kigumu muda mrefu (constipation-r
elated cancer)
14. Ni dawa nzuri kwa kansa ya kwenye damu (leukemia)
15. Ni dawa nzuri dhidi ya kansa ya mapafu (lung cancer)
16. Huzuia kujizalisha kwa bakteria aitwaye ‘Helicobacter pylori’, bakteria huyu ndiye husababisha vidonda vya tumbo mwilini, pia hutibu kiungulia, na kansa mbalimbali za tumbo
17. Ni msaada sana katika kuzuia na kutibu kansa ya titi
18. Hutibu kansa za kwenye kizazi na kansa za kwenye mirija ya uzazi
19. Huongeza msukumo wa damu
20. Husaidia kuzuia shambulio la moyo
21. Huzuia damu kuganda
22. Hushusha kolestro
23. Husafisha damu
24. Husaidia watu wenye kukakamaa kwa mishipa
25. Hutibu shinikizo la juu la damu
26. Husafisha utumbo mpana
27. Hupunguza mishtuko kwenye utumbo mpana na tumbo kuunguruma
28. Huondoa GESI TUMBONI KIRAHISI ZAIDI
29. Husaidia mfumo wa mmeng’enyo wa chakula
30. Dawa nzuri ya kuondoa uchovu
31. Husaidia kuzuia kutapika. Husaidia hata wale wanaosafiri baharini wasipatwe na kichefuchefu
32. Husaidia kuondoa maumivu kutokana na mkao mmoja wa mrefu ama kusimama au kukaa
33. Husaidia uzalishwaji wa juisi vimeng’enya kwa ajili ya kumeng’enya chakula
34. Husaidia kuzuia kuharisha
35. Husaidia mfumo wa upumuaji na kutuliza dalili za pumu
36. Hutibu tatizo la miguu kuwaka moto
37. Hutibu homa ya kichwa
38. Hutibu maumivu ya tumbo wakati wa hedhi
39. Hutibu homa za asubuhi hata kwa mama mjamzito
40. Husaidia kupunguza homa ya baridi yabisi (helps reduce inflammation of arthritis)
41. Huimarisha afya ya figo
42. Husaidia kupunguza uchovu unaotokana na matibabu yaliyopita ya mionzi
43. Ina madini ya potassium ya kutosha
44. Ina madini ya manganese ambayo ni muhimu katika kuuongeza mfumo wa kinga ya mwili dhidi ya magonjwa mbalimbali, hulinda kuta za moyo, hulinda mishipa ya damu na mishipa ambako mikojo hupita
45. Ina kitu kinaitwa ‘silicon’ ambacho chenyewe kazi yake hasa ni kuongeza afya ya ngozi, nywele, meno na kucha
46. Husaidia umeng’enywaji wa madini ya calcium
47. Pia ina vitamini A, C, E, B-complex, chuma, zinki , magnesium, phosphorus, sodium, calcium, na beta-carotene
48. Hulinda kuta za moyo, hulinda mishipa ya damu na mishipa ambako mikojo hupita

BLEND KAMA UNAVYO TENGENEZA JUICE YA KAWAIDA  KISHA KUNYWA  GLASS MOJA KWA SIKU.

AU UNAWEZA KUJENGA MAZOEA YA KUTAFUNA VIPANDE KADHAA KILA SIKU ASUBUHI KABLA HUJALA KITU.

Tafadhari share kwa ajili ya wengine

Wednesday, July 26, 2017

FAHAMU VYAKULA VINAVYO ONGEZA HAMU YA TENDO LA NDOA

VYAKULA VINAVYOONGEZA HAMU YA TENDO LA NDOA

PILIPILI
Kama tunavyojua wote mara nyingi chakula ambacho kimeungwa pilipili hufanya hata mapigo ya moyo kuwa tofauti na wakati mwingine hata jasho kutoka au kamasi kutoka. Kwenye pilipili kuna kitu kinaitwa capsaicin ambacho hufanya pilipili iwe na hali ya ukali ambao huwezesha ubongo kutoa homoni ya endorphins ambayo katika hali ya juu huleta mguso wa hisia za raha.
Pia pilipili husisimua mfumo wa ufahamu (nerves) wa ubongo na katika kufanya hivyo huwezesha kumshwa haraka hisia za kimapenzi (kunyegeka) na pia ili ukiguswa au kubusiwa au kunyonywa au kupapaswa uweze kupata hisia kila sehemu.

NAFAKA
Nafaka zina nyuzinyuzi (fibre) na sukari ngumu (complex sugar) ambazo kusaidia kutunza uzito wa mwili.
Nafaka husaidia katika kuzalisha homoni za testosterone kwenye damu. Na pia nafaka huwezesha mtu kuwa na nguvu hatimaye kwenda masafa marefu wakati wa tendo. Kula nafaka nzima kama vile brown bread badala ya white bread, pia kula nafaka halisi badala ya cornflakes(zilizokobolewa) ni jambo zuri linalokuhakikisha afya njema na mahusiano mazuri ya ndoa yako

MATUNDA NA MBOGA ZA MAJANI.
Mlo wenye matunda na mboga za majani una matokeo makubwa sana katika hamu ya tendo la ndoa kwa njia nyingi. Kwanza; matunda na mboga za majani hupunguza kiwango cha mafuta na unene (cholesterol), kuongezeka kwa mafuta mwilini huzuia mzunguko wa damu kwa kubana mishipa ya damu. Pia kula matunda na mboga za majani huhakikisha balance ya uzito kwani unene (obesity) kwa wanaume kuna matokeo mabaya katika kuzalisha homoni za testosterone na hatimaye jogoo kushindwa kuwika na kuwa na hisia kidogo. Na pia wanandoa wanapozidi kunenepeana ndipo na hali ya kufurahia au kutaka au hamu ya tendo la ndoa huzidi kupungua.

TANGAWIZI
Tangawizi ni chakula ambacho husisimua sana mfumo wa mzunguko wa damu mwilini, na tangawizi zinajulikana sana kwa kusukuma damu kwenda sehemu za viungo vya uzazi yaani uke na uume. Inaweza kuliwa mbichi, au kupikwa au kuanikwa na kuwa kama unga.

ASALI
Asali ina madini yanayoitwa boron, ambayo husaidia mwili kutumia homoni ya estrogen ambayo ni homoni inayohusika na viungo ya uzazi na mapenzi kwa mwanamke. Pia kuna utafiti unaoonesha kwamba asali huongeza nguvu, kitendo ambacho kitapelekea mwanamke kuwa uwezo na hamu ya tendo la ndoa au libido.

KARANGA
Karanga huhusika moja kwa moja na kutunza mfumo wa mzunguko wa damu kuwa na afya (vascular system). Pia mfumo wenye afya (mzunguko wa damu) katika uke na uume huwezesha mwanaume' na mwanamke kupata msisimko wa mapenzi haraka hatimaye tendo la ndoa kuwa zuri. Pia karanga zina madini muhimu kama vile magnesium, asidi ya folic na zinc ambayo ni muhimu sana katika uzalishaji wa mbegu za mwanaume.

OYSTERS
Huwa na kiasi kikubwa sana cha madini ya zinc na haya madini ndiyo huhusika zaidi na uzalishaji wa homoni ya testosterone kwa wanaume. Pia imethibitika kwamba wanaume wenye ukosefu wa madini ya zinc huwa na matatizo ya nguvu za kiume na wakati huohuo kuwa na madini mengi ya zinc mwilini huongeza kiwango cha shahawa.

SOYA
Pamoja na kuwa na kiwango kidogo sana cha fat na pia kuwa na kiwango kizuri cha protein, soya zina phytoestrogens ambayo husaidia sana wanawake ambao wamefikia menopause kutengeneza homoni ya estrogen ya ziada. Husaidia uke kuwa laini (wet, lubricated) mwanamke akisisimliwa wakati wa tendo la ndoa.
KUMBUKA: SOYA NI NZURI KWA MWANAMKE TU.

CHOCOLATE
Chocolate ina phenylethylamine, kemikali ambayo husababisha hisia za furaha wakati wa mwanamke au mwanaume kufika kileleni (orgasm)

NOTE; kama wewe ni mnene tambua kuwa vyakula vya Wanga na Sukari kwako siyo rafiki kwani husababisha uzito usipungue au kuongezeka kabisa. Chagua vyakula sahihi vyenye Protin, Fat, Mboga zote za Majani na Matunda yasiyo matamu.

Unene ni adui wa tendo la ndoa, ni vyema kuwa na uzito wa kawaida ili kurahisisha hata homoni zako za uzazi kufanya kazi kwa usafiri.

Na endapo wewe siyo mnene basi unaweza kutumia vyakula vyote tulivyotaja katika somo hili, kumbuka kuwa tiba ya vyakula ni tiba ya taratibu hadi kufikia malengo.

Kama kuna makala utataka uandaliwe kuhusu ugonjwa wowote usisite kuacha comment yako chini nasi tutakuandalia au waweza tuandikia katika email na whatsapp hapo chini

Email:ephrakirumba8@gmail.com
Whatsapp:+255717064639

Tuesday, July 25, 2017

EAT TWO BANANAS A DAY AND YOU WILL NOTICE SEVEN CHANGES IN YOURSELF

1.The vitamins and minerals found in bananas keep your body in good condition and the potassium helps to prevent muscle cramps.

2.Your body transforms the amino acid tryptophan into serotonin and releases it in your brain. This so-called happiness hormone helps us to be content and more satisfied.

3.Bananas contain very little sodium and lots of potassium which makes them the perfect food for people with heart conditions.

4.Bananas are rich in iron which your body needs to create red blood cells and hemoglobin. This helps to boost your blood supply.

5.Bananas help to regulate your blood sugar level. They also contain Vitamin B which has a calming effect on your nerves.

6.When its hot out you can cool yourself down by eating a banana. They can even help to reduce your body temperature. If you have fever.

7.Bananas are natural acid reflux Inhibitors. Eating a banana can instantly relieve heartburn.

Friday, July 21, 2017

JINSI YA KUTAMBUA KAMA UZITO WAKO UNAENDANA NA UREFU WAKO

JINSI YA KUTAMBUA KAMA UZITO WAKO UNAENDANA NA UREFU WA MWILI WAKO(BODY MASS INDEX)

By: Ephraim Kirumba
whatsapp 0717064639
Email: ephrakirumba8@gmail.com

Watu wengi tumekuwa tukiishi kwa kutojua miili yetu kama ipo sawa, hii ni kutokana na kile kitendo pengine cha kutougua hutufanya tujisahau kabisa katika kujua undani wa Afya yetu.

Leo napenda tujifunze namna ya kujua jinsi gani utatambua kuwa UZITO WAKO UNAENDANA NA UREFU WA MWILI WAKO(BODY MASS INDEX kwa kifupi BMI)

Kwa kifupi kitendo hiki huhusisha vitu viwili ambavyo ni uzito wako katika kilogram(kg) pamoja na urefu wako katika mita(m). Tutajifunza kwa kutumia mfano.

Uhusiano huo upo katika mpangilio kama ifuatavyo:
BMI ikiwa chini ya 18.50 hapa inakuwa mtu huyu uzito wake upo chini kuliko kawaida(UNDER WEIGHT)

BMI kuanzia 18.50 hadi 24.99 huyu mtu ni mwenye Afya njema na yuko vizuri kabisa(HEALTHY)

BMI kuanzia 25.00 hadi 29.99 huyu ni mtu ambaye amezidi uzito(OVER WEIGHT) hivyo uzito wake na urefu wake haviendani kabisa.

BMI kuanzia 30.00 na kuendelea basi huyu mtu ni yule aliyepitiliza kabisa kiwango cha uzito na anaingia katika kundi la Obesity.

Sasa unapata vipi uhusiano wa uzito na urefu wako(BMI)?

Angalia hapa chini
Kanuni(BMI)=uzito ÷ (urefu)kipeo cha pili
      
Tuangalie mfano mimi Ephraim nikiwa nina uzito wa kg 64 na urefu wa sentimeta 162 ambao ni sawa na mita 1.62

BMI ya Ephraim=64/1.62×1.62
BMI=64/2.6244
BMI=24.386

Kwa mfano huo basi Ephraim yupo kwenye kundi salama japo bado kidogo tu afikie 25 ambapo siyo pazuri.

Sasa tufanye ya kwamba Ephraim ana uzito wa kilo 74 na urefu uleule

BMI= 74/2.6244
BMI=28.196
Hapa anakuwa OVER WEIGHT

Na endapo Ephraim ana uzito wa kg 91;
BMI=91/2.6244
BMI=34.6745
Hapa ni OBESITY!!

Ndugu msomaji wa makala hii nadhani sasa umeshafahamu namna ya kujua kama una uzito unaoendana na urefu wako, hivyo unaweza kujifanyia tathimini wewe mwenyewe.
NOTE: Urefu wako uwe katika kipimo cha mita(metre)

YAFUATAYO NI BAADHI YA MADHARA YA KUWA NA UZITO ULIOZIDI(KUANZIA BMI 25 NA KUENDELEA)
-Magonjwa/matatizo ya Ini na Figo
-Magonjwa ya Kisukari, Shinikizo la damu, Kiharusi na matatizo ya Moyo
-Tatizo la kutopumua vizuri wakati wa usingizi
-Kiwanjo cha juu cha mafuta mabaya(cholesterols)
-Ugonjwa wa mifupa kama yabisi(osteoarthritis)
-Matatizo ya hedhi kwa akinamama na upungufu wa nguvu za kiume kwa wanaume

Unaweza ku-share zaidi makala hii kwa watu wengi kadri uwezavyo ili nao waweze kujifunza kama ulivyojifunza wewe.

Mawasiliano yetu yapo hapo mwanzo kabisa mwa makala hii.

Wednesday, July 19, 2017

ZIJUE TARATIBU ZA ULAJI WA MATUNDA

======*******USHAURI JUU YA ULAJI WA MATUNDA*******======
**************************************************************************************
    Matunda yana faida nyingi mwilini na ni miongoni mwa vyakula vinavyopaswa kupewa kipaumbele katika milo yetu ya kila siku. Lakini kwa bahati mbaya, siyo watu wote wanaelewa umuhimu wa matunda na jinsi ya kula ili kupata faida zake.

    Kutokana na kula matunda kinyume na utaratibu, watu wengi huyachukia matunda baada ya kujikuta wakiumwa tumbo au kujisikia kichefuchefu na kutapika mara baada ya kula. Wengine husikia tumbo kujaa gesi na kusikia kiungulia.
    Halikadhalika, watu wengi wamefundishwa na kuzoeshwa kulishwa matunda baada ya mlo, mazoea ambayo ni kinyume kabisa na kanuni za ulaji sahihi wa matunda. Katika makala haya, utaelewa njia sahihi ya kula matunda ili kupata faida zake.

KULA MATUNDA TUMBO LIKIWA TUPU
===============================
-- Ili kunufaika na matunda, kula matunda wakati ukiwa na njaa na tumbo likiwa tupu. Unapokula matunda katika hali hii, matunda husagika haraka na virutubisho vyake husambaa mwilini kwa urahisi. Baada ya saa moja au zaidi, unaruhusiwa kula mlo wako mwingine kama kawaida.

USILE BAADA YA KULA
===================
-- Imezoeleka na watu wengi kula matunda baada ya mlo kamili. Hata kwenye hafla na tafrija kubwa mbalimbali, utaona matunda huliwa mwishoni baada ya chakula. HII SIYO SAHIHI na hayo ni makosa miongoni mwa makosa mengi yanayofanyika kwa sababu ya mazoea tu.

-- Inaelezwa kuwa ulaji wa matunda baada ya mlo siyo sahihi kwa sababu matunda huyeyuka haraka kuliko chakula cha kawaida. Tunda linapokuwa tayari kupita tumboni kuelekea kwenye utumbo mwembamba, huzuiwa na chakula. Baada ya muda tunda linachanganyika na chakula na kuoza na hatimaye kuzalisha asidi  ambayo humfanya mtu kuumwa tumbo baada ya kula matunda. Lakini pia virutubisho vyake hupotea.

-- Ili kuepukana na hali hiyo ya msongamano kwenye tumbo, kula matunda saa moja kabla au kama utakula baada ya mlo, angalau kula baada ya masaa mawili. Ukila baada ya muda huo, utakuwa umetoa nafasi ya chakula kusagika na bila kuzuia uyayukaji wa matunda.

ZINGATIA KIWANGO CHA SUKARI KWENYE MATUNDA
===========================================
--> Baadhi ya matunda, kama vile papai, ndizi mbivu, yana kiwango kingi cha sukari, karibu matunda yote yana sukari, lakini mengine huwa na kiwango kingi zaidi. Hivyo inashauriwa kula matunda kwa kiwango cha wastani kila siku bila kuzidisha kiwango cha sukari cha gramu 25 kinachohitajika kwa siku.

--> Aidha, unapokula tunda, hakikisha unakula tunda kwa ukamilifu wake ili kupata virutubisho vyote. Kwa mfano unapokula chungwa, ni vizuri pia ukala pamoja na nyama zake ili kupata virutubisho vyote muhimu vilivyomo.

--> Jiwekee tabia ya kula matunda ya aina mbalimbali kwa nyakati tofauti ili kupata vitamini na madini tofauti tofauti kulingana na mahitaji ya mwili. Kwa kuwa matunda ndiyo yanayojenga na kuimarisha kinga ya mwili, ulaji wa matunda ya aina mbalimbali kutakuhakikishia mwili wako kinga imara dhidi ya maradhi na kamwe hutasumbuliwa na magonjwa mara kwa mara.

SHARE KM WEWE SIO MCHOYO,WAKUMBUSHE NA WENZIO,,SUBSCRIBE BLOG YETU PIA KUPATA VITU ADIMU KM IVI KILA SIKU

Sunday, July 16, 2017

PID(PELVIC INFLAMMATORY DISEASE AU MAAMBUKIZI KATIKA VIA VYA UZAZI)

FAHAMU UGONJWA WA PID (PELVIC INFLAMMATORY DISEASE AU MAAMBUKIZI KATIKA VIA VYA UZAZI)

PID ni kifupi cha Pelvic Inflammatory Disease ambayo ni maambukizi ya vijududu vya bakteria katika mfumo wa ndani wa uzazi wa mwanamke. Maambukizi yanaweza kuwa katika mji wa uzazi, mirija ya uzazi, ovari au shingo ya uzazi.

PID husababishwa na vijidudu vya bakteria kuingia kwenye mji wa mimba kupitia mlango wa shingo ya uzazi. Vijidudu hivi hutokana na magonjwa ya zinaa yasiyotibiwa kama kisonono au klamidia. Huingia kwenye mji wa uzazi na kisha kuweza kushambulia ovari,mirija au mji wa mimba wenyewe.

Dalili

P.I.D huleta dalili zifuatazo. Mgonjwa anaweza kupata zote au baadhi ya dalili hizi;

=>Maumivu ya kiuno
=>Kutokwa na uchafu ukeni
=>Maumivu wakati wa kufanya ngono
=>Kutokwa damu baada ya kufanya ngono
=>Maumivu chini ya kitovu baaada ya kufanya ngono
=>Maumivu wakati wa kukojoa
Mara nyingi dalili huwa sio kali na wakati mwingine zinaweza kutokea kwa kipindi cha muda mrefu. Wakati mwingine mwanamke anaweza kupatwa na dalili ghafla na kali hasa maumivu ya tumbo.

Vipimo
Vipimo hivi vinaweza kufanyika kujua kama kuna ugonjwa wa PID.

=>Kipimo cha ultrasound
=>Kipimo cha magonjwa ya zinaa (VDRL)
=>Kuotesha uchafu wa kwenye uke (Cervical/vaginal swab for culture)

Matibabu
Mara nyingi tatizo hili hutibiwa kwa njia ya dawa za antibiotics kwa muda wa siku 14 ni muhimu kuzingatia matumizi na kukamilisha dozi ya dawa ili kuhakikisha umepona kabisa.

Madhara
PID isipotibiwa huleta madhara kwa mgonjwa hasa ikiwa ni hali ya ugumba na hata utasa.

Kujikinga
Kujikinga na PID, ni muhimu kujikinga na magonjwa ya zinaa kwa;

kuwa na mpenzi mmoja uliyepima nae afya na magonjwa ya zinaa.
kutumia kondomu kila mara unapofanya ngono.
kuacha tabia ya kuwa na wapenzi wengi.
Unaposhisi dalili za magonjwa ya zinaa, wahi hospitali kupata matibabu sahihi na hakikisha umepona.

Friday, July 14, 2017

JINSI YA KUREKEBISHA MZUNGUKO WA HEDHI

Jinsi ya kurekebisha mzunguko wa hedhi

Tatizo la kuvurugika kwa mzunguko wa hedhi huanza ghafla au polepole ambapo mwanzo mwanamke alikuwa akipata siku zake katika utaratibu unaoeleweka lakini mara haelewi au hajielewi namna mzunguko wake unavyoenda.

Kuvurugika kwa hedhi ni kitendo cha mwanamke kuanza kuona siku zake bila tarehe au mzunguko maalumu na matokeo yake ni kuwa mwanamke atashindwa kutimiza malengo yake kwa kutumia mzunguko huo sababu ni haueleweki.

Unaweza kutokewa ghafla tu unapata hedhi mahali usipotarajia jambo linakufanya ubaki na woga na huelewi nini cha kufanya kwani hukuwa umejiandaa kwa tukio hilo kama matokeo ya siku zako kutokuwa mzunguko maalumu. Wakati mwingine unaweza kupitiliza mwezi hata miezi kadhaa bila kuona kabisa siku zako na hata ukipima ujauzito unakutwa huna ujauzito wala dalili huna.

Madhara ya kuvurugika kwa mzunguko ni pamoja na;  kushindwa kupata ujauzito, maambukizi katika kizazi na kuziba kwa mirija ya uzazi.

Kwanini unahitaji mzunguko wa hedhi ulio sawa?

Faida za kuwa na mzunguko wa hedhi ulio sawa:

Utakusaidia kupata ujaouzito ulioupangilia
Utakuepusha kupata ujauzito ambao hukuupangilia
Utaweza kuamua jinsia ya mtoto unayemtaka
Nini husababisha kuvurugika kwa mzunguko wa hedhi

Ni rahisi kugundua kama mzunguko wako umevurugika ikiwa tu unauafahamu vizuri mzunguko wako ulio sahihi. Kufahamu mzunguko unahitaji uifahamu siku ambayo ulianza kuona damu hadi siku utakapoona tena katika mzunguko unaofuata. Karibu kila mwanamke huwa na mzunguko wake usiofanana na wa mwingine.

Tatizo linaweza kuanza kwa kurukaruka siku, mwanamke pia anaweza kupoteza siku yaani mwezi mwingine anaona na mwezi mwingine haoni, au anaingia mara mbili kwa mwezi au anaona damu ya hedhi kwa siku nyingi hata zaidi ya siku arobaini mfululizo. Damu yake inaweza kutokea kidogo kidogo kila siku au nyingi huku ikiambatana na mabongemabonge na maumivu pia. Maumivu haya ya wakati wa hedhi huenea chini ya tumbo mpaka miguuni na kiunoni.

Kuvurugika kwa hedhi kunaweza kutokea kutokana na sababu zifuatazo:

Mabadiliko ya mazingira ambayo hupelekea mfumo wa mwili hubadilika pia hasa mwanamke akitoka sehemu ya joto kwenda mikoa ya baridi au toka mikoa ya baridi kwenda mikoa ya joto.

1.Msongo wa mawazo (stress)
2.Hofu
3.Woga
4.Mabadiliko ya kisikolojia
5.Uvimbe kwenye kizazi
6.Matatizo kwenye mfumo wa homoni
7.Matatizo kwenye vifuko vya mayai
8.Mimba kuharibika
9.Maambukizi sugu ya kizazi pia ni mojawapo ya sababu.
Maumivu ya tumbo chini ya kitovu ya mara kwa mara na kila ukipima unaambiwa ni ugonjwa wa U.T.I kumbe siyo yutiai
Kutokwa na uchafu ukeni
Maumivu wakati wa tendo la ndoa.

Jinsi ya kurekebisha mzunguko wa hedhi

Kabla ya yote unapopatwa na tatizo hili kwa muda mrefu ni vizuri ukaonana na daktari uweze kupata uchunguzi wa kutosha kubaini nini hasa inaweza kuwa ndiyo sababu hasa ya tatizo kwa upande wako.

Zifuatazo ni dawa mbadala 6 unazoweza kuzitumia ukiwa nyumbani ili kurekebisha tatizo hili

1. Papai

Papai ni moja ya dawa nzuri sana katika kutibu tatizo la kuvurugika kwa hedhi. Ina viinilishe mhimu kama carotene, chuma ( iron), Kalsiamu (calcium) na vitamini A na C ambavyo husaidia kulainisha na kunywea kirahisi kwa kuta za mji wa uzazi.
Siku 2 au 3 kabla ya kuanza kula papai kila siku nusu papai papai zima kutegemea na ukubwa wake au uwezo wako.

Kwa mtu mwelevu sababu ameshagundua papai laweza kumsaidia hivyo basi atalifanya papai kuwa sehemu ya chakula chake kila siku na si mpaka aumwe tu.

2. Mdalasini

Mdalasini unayo sifa ya kuondoa tatizo la damu kuganda sifa inayoweza kusaidia kuondoa tatizo la maumivu wakati wa hedhi.
Mdalasini ni chanzo kizuri cha nyuzinyuzi (fiber), kalsiamu (calcium), chuma (iron) manganizi (manganese).

• Tengeneza chai ya tangawizi kwa kutumia kijiko kidogo cha mdalasini ya unga na maji kikombe kimoja (robo lita), ipua na uache ipowe kidogo, ongeza asali kijiko kikubwa kimoja ndani yake na unywe. Fanya zoezi hili mara 2 mpaka mara tatu siku 2 au 3 kabla ya kuanza siku zako.

• Au changanya kijiko kidogo kimoja cha mdalasini ya unga na kijiko kidogo kimoja cha asali katika glasi moja ya maji ya uvuguvugu na unywe kutwa mara 2 siku za mwanzoni unapoanza au kukaribia kuingia katika siku zako.

3. Tangawizi

Tangawizi ni dawa ya asili yenye maajabu katika kutibu tatizo la mvurugiko wa hedhi. Tangawizi hufanya kazi mhimu kabisa katika kushusha kiwango cha homoni inayosababisha maumivu ijulikanayo kwa kitaalamu kama ‘prostaglandins’. Tangawizi husaidia pia katika kupigana na uchovu uletwao na mzunguko wa hedhi katika siku zile za mwanzo au siku 2 hivi kabla ya kuanza siku zako na huweza pia kufanya mzunguko usio sawa wa hedhi kuwa sawa

• Tengeneza chai ya tangawizi ukitumia tangawizi mbichi, kunywa kikombe kimoja kutwa mara 3 wakati wa siku zako au siku yoyote tu kama kinga. Kamulia ndimu kidogo ndani yake na utumie asali kupata radha badala ya sukari.

• Unaweza pia kuongeza tangawizi kwenye vyakula na mboga mboga nyingi unazopika kila siku.

4. KOTIMIRI (Parsley):

Tengeneza juisi ya kotimiri, viazi pori (Beet Root), karoti au matango. Tumia asali mbichi ukitengeneza juisi hii. Hii kotimiri inapatikana kirahisi Dar na Zanzibar ni mboga mboga inayotumika zaidi kwenye mahoteli ya kitalii. Mboga hii inacho kitu mhimu sana kijulikanacho kama ‘Apiol’ amabcho kazi yake kuu ni kurekebisha na kuweka sawa homoni za kike.

Changanya kwa ujazo sawa yaani kama juisi ya kotimiri ni kikombe kimoja basi ya kiazi pori nayo kikombe kimoja kadharika kwa matango. Juisi hii ni dawa tosha ya maumivu wakati wa siku za hedhi, hurekebisha mzunguko wa hedhi na imethibitika kuwa bora kuliko dawa nyingi za kizungu.

Kunywa glasi moja ya juisi hii kutwa mara 2.

5. MREHANI

Mrehani au Basil kwa Kiingereza ni mmea mwingine mzuri sana katika kuondoa maumivu wakati wa hedhi na kurekebisha mzunguko wa hedhi kwa ujumla. Mmea huu unatumika sana jikoni kwenye mahotel ya kitalii Dar na Zanzibar. Unao sifa kuu ya kuzuia au kuondoa maumivu mwilini.

• Ongeza kijiko kikubwa kimoja cha majani freshi ya mrehani yaliyokatwakatwa na kisu (chop) kwenye kikombe kimoja cha maji ya moto, funika vizuri na usubiri ipowe. Kunywa yote ikishapoa na ufanye zoezi hili kutwa mara 3 kwa wiki 3 mpaka 4 au mpaka tatizo lako limeisha.

• Au tengeneza juisi ya majani haya. Yatwange kwenye kinu au kwenye blenda ya umee kupata majimaji yake kisha chota vijiko vya chai viwili uweke ndani ya kikombe kimoja cha maji ya moto na unywe yote. Fanya zoezi hili kutwa mara 3.

• Unaweza pia kuongeza majani freshi ya mrehani kwenye vyakula vingi unavyokula kila siku.

6. MAJI YA KUNYWA

Matatizo karibu yote mwilini chanzo chake ni mwili kutokuwa na maji ya kutosha. Maji ni uhai. Unachohitaji hapa ni kutokusubiri kiu. Kiu ni ishara ya mwili iliyochelewa kuhitaji maji.

Matatizo mengi ya kiafya tumeyaona kwa watu wasiopenda kunywa maji ya kutosha kila siku.

Jitahidi hata iweje iwe unaumwa au huumwi chochote unywe maji lita mbili mpaka tatu kila siku iendayo kwa Mungu na utaniletea mrejesho hapa hapa.

Kama una swali au unahitaji ushauri wowote liulize hapo kwenye comment nitakujibu.

Featured Post

FAIZA ZA KULA PAPAI

 _*Siri usioijua kuhusu utajiri wa tunda la papai katika kukulinda na magonjwa hatarishi kutokana na faida zake lukuki*_  Hizi ndizo FAIDA 1...