Monday, June 19, 2017

ZIFAHAMU AINA KUMI NA MBILI(12) ZA MAUMIVU YA KICHWA NA TIBA ZAKE

AINA KUMI NA MBILI ZA KUUMWA NA KICHWA

Kuumwa na kichwa kumegawanyka sehemu kuu nyingi sana japo kuwa 1% yake ni hashirio la matatizo ya kiafya ambayo yameadvance. Kama vile concussion of brain,meningitis,encephaliti, na stroke. Kuumwa na kichwa pia inawezatokana na matatizo ya taya, meno au hata kula vitu vya baridi zaidi. Vyakula vyenye nitrite au monosodium glutamate.
Sehemu ambazo huuma ni kama ifuatavyo.mfumo wa fahamu ambao upo kwenye fuvu la kichwa.
Baadhi ya neva za fahamu zizlizoko usoni
Misuli ya kichwani
Mishipa inayopatikana kwenye fuvu la kichwana chini ya ubongo kuna mifumo ya fahamu yenye hisia. Kumbuka fuvu na tishuu za ubongo kwa zenyewe haziumi kwani hazna mifumo ya fahamu ambayo inahisia.
Mambo haya 12 nayo yanahusika sana.

1:Nervous tension headaches;

Ni maumivu ya kichwa endelevu upande mmoja au pande zote za misuli ya shingo na upande wa juu wa mgongo,kuumwa na kichwa pamoja na kusinzia. Tumia vitamin b2 na c , punguza au acha matumizi ya sukari,kahawa,chakula chenye kukusababishia mzio,misongo ya mawazo na ufanye mazoezi yakutosha.

2: Cluster headaches

Kichwa kuuma haswa upande mmoja wa kichwa kwa maumivu makali, machozi humtoka mtu na makamasi kwa mbali. Kitu cha kwanza ni kutumia chakula chenye protein ya kutosha, epukana na chakula chenye mzio kwako.

3: Hangover headaches;

Hii ni hali ya kichwa kuuma kwa sababu ya matumizi makubwa ya vinywaji vikali haswa pombe. Weka barafu chini ya kichwa yaani maeneo ya kichogoni au shingoni,kunywa maji mengi na juice ya matunda freshi na uache pombe.

4: Exertion headaches;

Hutokea pale ambapo mwili utatumika sana na haswa kwenye ngono. Weka barafu linalouma, kula mlo kamili na usifanye mazoezi.

5: Caffein headaches;

Hali hii hutokea pale ambapo umeacha matumizi makubwa sana ya kahawa kwa ghafla. Kunywa kiasi kidogo cha kahawa kuondoa maumivu na upunguze matumizi kidogokodogo mpaka utakapo acha kabisa.

6: Sinus headaches;

Maumivu haya huanzia upande wa kulia na kushoto wa pua na kupanda mpaka kichwani. Kula vitamini C kwa wingi na umuone mtaalamu wa afya maana saa zingine hii utkana na maambukizi.

7: Bilious headaches;

Kichwa na macho huuma haswa kipanda uso na husababishwa na kula sana, kula vibaya, kutofanya mazoezi na kukosa choo. Fanya mazoezi na kunywa maji yakutosha na kasha fanya enema.

8: Hunger headaches;

Maumivu ya kichwa ambaya husababishwa na kutokula kwa muda. Kula chochote ilimradi kiwe ni protein au carbohydrates .

9: Eyes ram headaches

Haya ni maumivu yanayotokea kwenye macho na wengi hudhani labda wameangalia vibaya japo saa zingine inaweza kuwa sababu. lakini chanzo chake haswa ni ubongo kufanya kazi kupita kiasi. Badili mtindo wa maisha na kama ni mtumiaji wa miwani ni vyema ukamuana mtaalamu aangalie kama lensi zimepotea nuru au la.

10: Menstrual headaches;

Hali hii hutokea kwa kina mama kipindi cha yai kupevuka. Hutokana na mabadiliko ya hormone, muone mtaalamu wa afya.

11: Arthritis headaches;

Haya ni maumivu ya kichwa yanayosikika mpaka shingoni na saa zingine mpaka mgongoni ambayo husababisha maumivu haswa unapozidisha mwendo au shughuli. Kitu kikubwa ni kutibu ugonjwa unaosababisha hali hiyo.

12: Hypertension headaches;

Ni maumivu ya kichwa chote, mwendo mkubwa pia huongeza maumivu. Hali hii husababishwa na shinikizo la damu. Tibu au pambana kushusha shinikizo la damu na halii itaisha bila shaka.

@Swali lolote comment hapo chini nawe utajibiwa haraka kwa blog yetu

Saturday, June 17, 2017

TATIZO LA UKOSEFU WA NGUVU ZA KIUME NA CHANZO CHAKE

...
LIFAHAMU TATIZO LA #UKOSEFU WA NGUVU ZA #KIUME NA CHANZO CHAKE.

Leo katika zama hizi za sayansi na teknolojia tatizo la kupungua nguvu za kiume limekuwa kubwa sana, siyo Tanzania tu, bali duniani kote. Jambo muhimu analopaswa mwanaume yeyote kufahamu ni kwamba, kupungua nguvu za kiume siyo ugonjwa, ni dalili ya ugonjwa. Hii ina maana kuna dosari au udhaifu wa kiutendaji ndani ya mwili wake. 

Kuna sababu nyingi mno zinazosababisha mwanaume apungue nguvu za kiume. Mtu aweza kujiuliza kwa nini kuwe na sababu nyingi namna hiyo?

Kwani nguvu za kiume ni nini?

Nguvu za kiume ni jina la jumla lenye vipengele vingi ndani yake ikiwa ni pamoja na hamu ya mapenzi; kusimama kwa uume barabara; kuchelewa kufika kileleni kiasi cha kufurahia tendo la ndoa; uwezo wa kurudia tendo la ndoa; pumzi, wepesi na uchangamfu wa mwili katika kutenda tendo  lenyewe.

Ni viungo gani vinavyohusika na nguvu za kiume?

Nguvu za kiume ni tukio pana sana lenye kuhusisha viungo na vitu vingi ndani ya mwili. Kuna zaidi ya viungo na vitu 50 ndani ya mwili wa mwanaume vinavyohusika na nguvu za kiume ambapo viungo hivi pia hufanya kazi zingine za mwili. Baadhi ya viungo hivyo ni ubongo, moyo, mishipa ya neva mishipa ya ateri, mirija iliyo ndani ya uume iitwayo corpora cavernosa.

Viungo vingine ni neva maalumu za parasympathetic, tezidume (prostate gland), ini, figo, homoni ya testestorone, kemikali za  acetylcholine, serotonin, na dopamine, uti wa mgongo, eneo la chini ya mgongo (kiuno), eneo la nyonga.

Viungo vingine ni misuli maalumu iitwayo pelvic floor, tezi pituitari (pituitary gland), utando maalumu wa uumeni uitwao tunica albuginea, misuli iitwayopubococcygeus [PC muscles], kemikali ya nitric oxide, kemikali ya prolactin n.k.
Nadhani unaona jinsi ilivyo vitu vingi.

Nini maana ya kupungua nguvu za kiume?

Unapopungua nguvu za kiume ina maana ndani ya mwili wako kuna baadhi ya vitu katika vitu nilivyovitaja hapo juu havifanyi kazi vizuri jinsi ipasavyo na inavyotakiwa. Yawezekana ni figo ndilo halifanyi kazi vizuri, au ini, au tezi dume, au neva ya parasympathetic, au moyo una tatizo au mishipa ya ateri, au misuli ya pelvic au homoni fulani iko juu sana au iko chini sana (hormonal imbalance), orodha ni ndefu sana.

Kitendo cha baadhi ya viungo hivyo kutofanya kazi vizuri basi hapo hutokea upungufu katika nguvu za kiume. Upungufu huo unaweza kuwa ni:

1. Kukosa hamu ya mapenzi; au

2. Uume kusimama kwa uregevu; au

3. Kuwahi kufika kileleni; au

4. Kuchelewa sana kufika kileleni (au kushindwa kufika kileleni kabisa); au

5. Kushindwa kurudia tendo la ndoa; au

6. Kuhisi maumivu wakati wa tendo la ndoa au baada ya tendo hilo; au

7. Kukosa pumzi na uchangamfu wa mwili katika utendaji; au

8. Kuchoka sana baada ya tendo la ndoa na hata kukinai kabisa au hata kusikia kichefuchefu;

Ili uelewe vizuri zaidi labda niseme kwamba, nguvu za kiume ni kama kiwanda; na ni zaidi ya kiwanda. Ndani ya kiwanda kuna umeme, maji, madawa, watu (wafanyakazi wa kila taaluma na fani), mashine, mitambo n.k.

Ikitokea kitu kimojawapo kukosekana, mathalani umeme, au wafanyakazi wakagoma, au kukakosekana madawa muhimu au maji na kadhaa wa kadha, basi bidhaa inayotarajiwa kupatikana sokoni, kwa hakika haitapatikana.

Vivyo hivyo nguvu za kiume, mathalani, ikitokea tezi dume kutofanya kazi vyema, basi hapo mwanaume hatoona nguvu za kiume, zitapungua au zitaisha kabisa!

Kwa hiyo upungufu wa nguvu za kiume ni upungufu au kasoro za kiutendaji wa viungo ndani ya mwili wa mwanaume. Mwanaume yoyote anapaswa kutambua jambo hili.

Lakini nini kinachopelekea viungo hivyo vishindwe kufanya kazi vizuri?

Kuna maradhi kadhaa, vyakula tunavyokula, tabia na mtindo wa maisha vinavyoweza kupelekea viungo hivyo kutofanya kazi vizuri. Baadhi ya maradhi hayo na tabia hizo ni kujichua/punyeto (masturbation) kwa muda mrefu; kisukari; presha ya kupanda; presha ya kushuka; uvutaji wa sigara; unywaji wa pombe; madawa ya kulevya; kufanya kazi kupita kiwango na kukosa muda wa kupumuzika; matatizo ya kukosa usingizi na kuchelewa kulala usiku.

Uume wako unatakiwa usimame kwenda juu siyo usimame kwenda mbele tu au kurudi chini. Na ukielekea juu uwe umenyooka kama rula usijikunje kama ndizi maana ukijikunja hilo ni tatizo la kitu kinachoitwa plaque kuganda kwenye uume. See? Ndo maana tunaelimishana rafiki. Tatizo la nguvu za kiume ni pana sana.

Hata hivyo kuna vitu unaweza kufanya ili kurejesha nguvu zako za kiume.

Usilee tatizo. Madhara ni makubwa mno likiendelea kwa muda mrefu!

Mawasiliano haya hapa.

#WhatsApp +255620204770

TATIZO LA KUTOPATA CHOO(CONSTIPATION)

#CONSTIPATION/TATIZO LA KUTOPATA CHOO.

#KAMA UNAPATA CHOO MARA 1 KWA SIKU NA UNAKULA MARA 3,UPO KWENYE HATARI YA KUPATA MAGONJWA YAFUATAYO....….…..

~Kansa ya Utumbo.
~Uzito uliozidi.
~Bawasiri(Vinyama sehemu ya haja kubwa).
~Kifo.
~Maumivu ya Kiuno,Mgongo,Mabega,Kichwa,Misuli.
~Kukosa usingizi(Insomnia)
~Kukosa hamu ya kula(Loss of appetite).
~Tumbo kuja gesi.
~Vidonda vya tumbo(Ulcers).
~Upungufu wa nguvu za kiume.
~Kushindwa kubeba mimba  au kuzaa.
~Kupasuka kwa utumbo.
~Ileocecal valve incompetence.
~Kutoa harufu mbaya mdomoni na unapojamba.

Soma zaidi hapa.............
Kati ya changamoto ya kiafya niliyokua nayo,ni kutopata choo na kupata choo kigumu kama cha mbuzi,na nilidhani ni kawaida kutopata choo kwa muda wa siku 3 hadi week,kumbe ni tatizo kubwa linaloweza kusababisha 90% ya magonjwa yasiyoambukizwa na hatimae vifo.

#WATU wengi wanasumbuliwa na tatizo hili ambalo huwafanya kuwa na uoga na aibu wa kuelezea na kushindwa hata kwenda hospital kupata tiba.

#CHANZO CHA TATIZO
Tatizo la kutopata choo linasababishwa na mfumo mbovu wa mmeng'enyo wa chakula.

Kwenye utumbo mdogo ambao una urefu wa takribani mara 10 mpaka 13 ya urefu wa mtu husika,kuna Villars, hivi ni kama vidole vinavyokua vinachezacheza ili kumeng'enya chakula,ila kutokana na sumu tunazoingiza mwilini kila siku kutoka kwenye vinywaji,chakula,dawa na hewa,pamoja na mafuta tunayokula kwenye vyakula,zinaenda kujipachika katikati ya Villars (vidole) na hivyo kusababisha vidole visimame(blocked) hivyo chakula hakimeng'enywi na kusababisha chakula unachokula kupitiliza moja kwa moja kwenye utumbo mkubwa,na hapo ndio tatizo linapoanzia.
Na tatizo hili ndio hupelekea kupata tatizo la bawasiri.

#JE, UNAJUA BAWASIRI/HEMORRHOIDS NI NINI????!!

~Ni ugonjwa unaotokana na kuathirika kwa mishipa ya damu ya ndani na Inje ya sehemu ya haja kubwa na wakati mwingine mishipa hiyo huweza kupasuka/kuteleza na kuvuja damu kwenye njia ya haja kubwa na kasababisha kutoka kinyama au uvimbe.

~ugonjwa huu wa bawasiri kwa lugha ya kitaalamu tunauita HEMORRHOIDS ilhali kwa lugha ya kingereza unafahamika kama piles.

~tatizo hili huwaathiri watu wote ila zaidi huwaathiri watu wazima kuliko watoto na inakadiriwa kuwa karibu 50%ya watu wote wako katika hatari ya kupata tatizo hili katika umri wa miaka 30_50

#AINA ZA BAWASIRI

~Kuna Aina mbili za bawasiri

(A) BAWASIRI YA NDANI

~Aina hii ya bawasiri hutokea ndani ya mfereji wa haja kubwa huwa haiambatani na maumivu na wengi huwa hawajitambui kuwa Wana tatizo hili

~Aina hii hutokana na kuvimba na kuharibika kwa mshipa wa artery za ndani ya mfereji wa haja kubwa

(B)BAWASIRI YA NNJE

~Aina hii ya bawasiri hutokea katika eneo la mwisho kabisa la mfereji wa haja kubwa na huambatana na maumivu makali na kuwashwa kwa ngozi katika eneo la tundu Hilo pia husababisha mishipa ya damu (vena) kupasuka na damu kuganda na kasababisha Aina ya bawasiri iitwayo THROMBOSED HEMORRHOIDS

#CHANZO CHA TATIZO

~chanzo halisi cha ugonjwa huu hakijapatikana ila Kuna vitu ambavyo huwa chanzo cha kupata ugonjwa wa bawasiri ambayo ni

°Kufanya mapenzi kinyume na maumbile.
°Kuharisha kwa muda mrefu.
°Tatizo la kutopata choo.
°Matatizo ya umri.
°Shughuri ya kukaa kwa muda mrefu sana.
°Uzito kupita kiasi.
°Matumizi ya vyoo vya kukaa kwa muda mrefu.
°Vyakula vyenye mafuta kwa wingi.
°Vinywaji vikali kama pombe,kahawa,viroba.
°Kutokula vyakula vya nyuzi nyuzi.
°Kutokunywa maji ya kutosha.
°Vyakula vya ngano,wanga na vilivyokobolewa.
°Kutofanya shughuli yoyote baada ya kula.
°Kulala kabla ya masaa 4 baada ya kula usiku.

#DALILI ZA KUTOPATA CHOO NA BAWASIRI.

√ Ngozi kuwasha katika eneo la tundu la haja kubwa.
√ kupata maumivu makali wakati wa kujisaidia.
√ kutokea uvimbe/kinyama katika eneo la tundu la haja kubwa.
√kinyesi kuwa na damu na kunuka harufu mbaya sana.
√ Kinyesi cha makundi makundi kama cha mbuzi.
√ Kuhisi moto wakati wa kujisaidia.
√ Kutopata choo kwa siku 2 na kuendelea.
√ Tumbo kujaa gesi na kujisaidia hewa.
√ Kuhisi maumivu ukikaa.
√ Kusinzia baada tu ya kula
√ Tumbo kuunguruma.
√ Kujamba kila wakati.
√ Kukosa hamu ya kula.
√ Mkojo wenye rangi(ambao sio mweupe kama maji)

#MATIBABU NA JINSI YA KUEPUKA TATIZO LA BAWASIRI NA KUTOKUPATA CHOO.

~matibabu ya bawasiri hutegemea na Aina ya bawasiri pia tiba iliyozoeleka ni kukatwa kinyama na kuendelea na lishe ya chakula,kama kula matunda,mboga za majani,maji kwa wingi, hata hvyo tiba hii si nzuri kwasababu huwa haitibu chanzo cha tatizo hivyo huwa rahisi kujirudia.

#MADHARA YA TATIZO LA KUTOPATA CHOO NA BAWASIRI.

-kupata upungufu wa damu (anemia).
-Kupata tatizo la kutokuweza kuhimili choo.
-hupunguza nguvu za kiume na kuondoa hamu ya tendo la ndoa kwa wanawake.
-kuathirika kisaikolojia
- kukosa moral ya kufanya Kazi kutokana na maumivu makali.
- Kupasuka kwa utumbo na kusababisha kifo.
- Kitambi na uzito uliopindukia.
- Kansa ya Utumbo.
- Kukosa uwezo wa kubeba mimba.
- Na mengine yoote niliyoyataja mwanzo wa post.

Na Kwa ushauri zaidi juu ya nini ufanye kama una tatizo hilo,na kwa lengo la kujikinga,usikose makala ijayo

Friday, June 16, 2017

UGONJWA WA KIDOLE TUMBO(APPENDICITIS) NA TIBA YAKE

TAMBUA UGONJWA WA KIDOLE TUMBO
(APPENDICITIS) NA TIBA YAKE

Kidole tumbo au Apendeksi hupatikana katika utumbo mkubwa, urefu wake ni kama kidole cha mwisho cha mkono, huwa hakina kazi yoyote mwilini. Sehemu hii hupitisha myeyuko wa chakula na endapo katika chakula hicho kuna michanga au vitu vidogovidogo vigumu, hujikita humo na kushindwa kutoka.

Kidole tumbo pia kinapatikana upande wa kulia wa tumbo kutoka usawa wa kitovu na nyonga ya kulia.
Taka ngumu hizo zikishajikita kwenye kidole  tumbo na kushindwa kutoka ndipo kinapoanza kuvimba, hali hii kitaalam huitwa ‘Inflammation’. Hapa kidole tumbo kinavimba na kuwa na maumivu na pia hupata maambukizi ya bakteria.

DALILI ZA UGONJWA

Mgonjwa huanza kuhisi maumivu ya tumbo  kuanzia usawa wa kitovu ambayo huwa makali na kuacha kisha kusambaa taratibu kuelekea upande wa kulia.

Baada ya muda mgonjwa huanza kutapika  kisha kupata homa. Dalili hizi huwa haziji pamoja, huanza moja na kufuata nyingine lakini mgonjwa akiwahi kupata tiba dalili nyingine haziendelei. Baada ya hapo mgonjwa hupata homa.

Dalili za ugonjwa zinatofautiana kufuatana na aina ya ugonjwa huu ambapo kawaida umegawanyika katika hali ya ukali ‘Acute’ na hali ya usugu ‘chronic’. Maumivu makali yanayoambatana na homa na kutapika tunaita ni ‘Acute’

Maumivu ya ugonjwa huu ukifikia hatua mbaya husambaa hadi katika uti wa mgongo usawa wa kitovu au ‘Belly button’.

Pamoja na kwamba maumivu huanzia usawa wa kitovu, lakini dalili za awali kabisa huanzia juu ya kitovu ambayo huja na kupotea na mgonjwa anaweza kujihisi ana ugonjwa wa vidonda vya tumbo, baadaye ndipo hushuka chini taratibu na kusambaa.

Dalili hizi ni tofauti na watoto ambao hulalamika tumbo linauma sehemu zote kukiwa hakuna eneo maalam na baadaye maumivu huwa makali sana kwa tumbo lote hata akiguswa linauma sana.

Hali ya tumbo kuuma huambatana na kujaa gesi kwa wote yaani wanaume, wanawake na watoto.

CHANZO CHA TATIZO

Kama tulivyoona hapo awali chanzo cha tatizo, maumivu makali ‘Acute’ hapa hutokana na vile vitu vigumu vilivyoingia katika kidole tumbo kushindwa kutoka hivyo huziba kwa juu na zile taka ngumu huganda humo na kidole tumbo kuzidi kuvimba.

Hali ya usugu wa maumivu hutokana na taka ngumu hizo kukaa humo kwa muda fulani na baadaye hutoka huku ukiacha hali ya kidole tumbo kuwa na uvimbe.

Hali ya uvimbe ikikaa muda mrefu husababisha mzunguko wa damu kuzuiliwa sehemu hiyo hivyo kidole tumbo huvimba zaidi na husababisha kuta za Apendeksi kuharibika ‘Necrtotic’ na kukusanya majimaji kama usaha.

Hali hii husababisha tatizo liitwalo ‘Peritonitis’ yaani tumbo lote huathirika na kuuma. Mgonjwa akichelewa kupata tiba, usaha huu husambaa katika mfumo wa damu na kusababisha kifo.

UCHUNGUZI

Huzingatia historia ya mgonjwa, dalili na ishara zitajitokeza, vipimo vya damu vitafanyika, vipimo vingine ni vya Ultrasound na CT Scan ya tumbo vitasaidia kujua tatizo kwa undani zaidi.

Zipo pia njia mbalimbali za uchunguzi ambazo daktari anaweza kuzitumia mfano ‘Rovsing’s sign’ na  sitokovkty’s sign na nyinginezo.
Matibabu

Tatizo hili katika hatua za awali mgonjwa anaweza kutibiwa kwa dawa lakini tatizo linapoendelea inabidi afanyiwe upasuaji kuondoa Apendeksi.

Tatizo likiwa kubwa, upasuaji wa dharura hufanyika. Ni vema uwahi hospitali kwa uchunguzi na tiba.

Thursday, June 15, 2017

VIDONDA VYA TUMBO NA SABABU ZAKE

HABARI ZENU WADAU WA MAKALA ZANGU..?

LEO NIMEONA NIZUNGUMZIE VIDONDA VYA TUMBO NA SABABU ZAKE.

UGONJWA wa VIDONDA vya TUMBO hutokea iwapo KIDONDA cha UKUBWA wa angalau NUSU sentimita kitatokea kwenye sehemu yeyote ya UKUTA wa TUMBO au UTUMBO wa BINADAMU.

Kwa kawaida TATIZO hili huleta MAUMIVU MAKALI sana ya TUMBO ingawa si lazima kila MAUMIVU ayapatayo MGONJWA husababishwa na VIDONDA vya TUMBO .

Tafiti zimeonesha kwamba karibu ASILIMIA 70% mpaka ASILIMIA 90% ya VIDONDA vya TUMBO husababishwa na aina ya VIMELEA vya BAKTERIA wajulikanao kama Helicobacter pylori.

Aidha MATUMIZI ya baadhi ya DAWA za kutuliza MAUMIVU za JAMII ya Non Steroid Anti-inflamatory Drugs(NSAIDs), kama Aspirin au Diclofenac HUWEZA kusababisha au KUONGEZA uwezekano wa kupata UGONJWA huu.

Kuna DHANA iliyozoeleka kuwa VIDONDA vya TUMBO huathiri zaidi MFUKO wa kuhifadhia CHAKULA yaani TUMBO (stomach). DHANA hii SI KWELI kwani sehemu INAYOATHIRIWA ZAIDI na TATIZO hili ni SEHEMU ya KWANZA ya UTUMBO MDOGO ijulikanayo kama DUODENUM .

Kuna MAKUNDI MAKUU yafuatayo ya UGONJWA huu:-

1.VIDONDA vinavyotokea kwenye MFUKO wa kuhifadhia CHAKULA yaani TUMBO (Gastric ulcers)

2. VIDONDA vinavyotokea kwenye SEHEMU ya KWANZA ya UTUMBO MDOGO (Duodenal Ulcers)

3. VIDONDA vinavyotokea kwenye KOO (Oesophageal ulcers)

4. VIDONDA vijulikanavyo kama Merckel’sDiverticulum ulcers.

VISABABISHI:-

VIDONDA vya TUMBO husababishwa na MAAMBUKIZI ya BAKTERIA aina ya Helicobacter pylori.

Imeonekana kuwa zaidi ya ASILIMIA 50% ya WATU duniani wana VIMELEA hivi katika UTUMBO .

Aidha, MIONGONI mwao, karibu ASILIMIA 80% huwa hawaoneshi DALILI yeyote ya KUUGUA UGONJWA huu.

AINA hii ya VIMELEA vya BACTERIA husababisha karibu ASILIMIA 60% ya VIDONDA vinavyotokea kwenye TUMBO (gastric ulcers) na zaidi ya ASILIMIA 90% ya duodenal ulcers.

HALI hii husababishwa ZAIDI na KUSHINDWA kwa MFUMO wa KINGA MWILINI KUWAUA na KUWAONDOA kabisa VIMELEA hawa NDANI ya MWILI .

MATOKEO ya kushindwa huku HUSABABISHA kuwepo UAMBUKIZI wa KUDUMU katika KUTA za TUMBO (chronic active gastritis), UAMBUKIZI ambao huharibu MFUMO na UWEZO wa KUTA za TUMBO kutunza HOMONI ya GASTRIN, ambayo ni MUHIMU katika kuhakikisha MAZINGIRA ya TUMBO yanakuwa na KIWANGO salama cha TINDIKALI.

Kwa KAWAIDA, KAZI ya GASTRIN ni KUCHOCHEA utolewaji wa TINDIKALI (gastric acid) kutoka kwenye SELI za UKUTA wa TUMBO zijulikanazo kama Parietal cells.

Iwapo BACTERIA hawa WATASHAMBULIA na kuharibu UKUTA wa TUMBO , MFUMO wa GASTRIN pia UHARIBIKA, na hivyo kusababisha GASTRIN kuzalishwa kwa WINGI hali ambayo pia huchochea UZALISHAJI wa GASTRIC ACID kwa WINGI.

MATOKEO ya KUZALISHWA kwa WINGI kwa TINDIKALI hii hupelekea KUCHUBUKA kwa UKUTA wa TUMBO na hivyo kusababisha VIDONDA vya TUMBO .

MATUMIZI ya MUDA MREFU ya DAWA za kuondoa MAUMIVU za kundi la NSAIDs:-

UKUTA wa UTUMBO hujilinda na MADHARA yatokanayo na TINDIKALI ya UTUMBO (gastric acid) kwa kuwa na UTANDO LAINI (mucus) ambao hutolewa na VICHOCHEO vijulikavyo kama Prostaglandins.

DAWA hizi za KUNDI la NSAIDs huharibu MFUMO wa kutengeza VICHOCHEO hivi yaani prostaglandins na hivyo kufanya KUTA za TUMBO kukosa UTANDO wa KUZILINDA na MASHAMBULIZI ya TINDIKALI hali ambayo hupelekea KUTOKEA kwa VIDONDA vya TUMBO.

UVUTAJI wa SIGARA :-

Uvutaji SIGARA sambamba na MAAMBUKIZI ya BAKTERIA aina ya Helicobacter pylori huongeza MADHARA ya UGONJWA wa VIDONDA vya TUMBO.Ifahamike tu kuwa UVUTAJI SIGARA pekee hausababishi VIDONDA vya TUMBO.

VYAKULA au VIUNGO vya CHAKULA vyenye UCHACHU :-

KINYUME na DHANA iliyozoeleka miongoni mwa WATU wengi, baadhi ya VYAKULA vyenye UCHACHU na UPILIPILI kama vile PILIPILI, NDIMU, LIMAO na MASALA, HAVINA UHUSIANO na UWEZEKANO wa kupata VIDONDA vya TUMBO .

WATU walio katika KUNDI la DAMU la O :-

IMEONEKANA pia kwamba KUNDI la DAMU lijulikanalo kama BLOOD GROUP O, HALINA uhusiano wa kusababisha VIDONDA vya TUMBO.

UNYWAJI wa POMBE :-

UNYWAJI wa POMBE pekee hausababishi VIDONDA vya TUMBO. Hata hivyo, UNYWAJI wa POMBE sambamba na MAAMBUKIZI ya VIMELEA vya Helicobacter pylori huongeza MADHARA ya UGONJWA wa VIDONDA vya TUMBO.

VITU vingine:-

VITU vinavyohusishwa na UONGEZAJI wa MADHARA ya VIDONDA vya TUMBO ni pamoja na UPASUAJI wa TUMBO (major abdominal surgeries), KUUNGUA kwa MOTO (burns), UGONJWA wa FIGO ,na KUBADILISHWA kwa VIUNGO vya MWILI kama FIGO au INI .

DALILI au VIASHIRIA vya VIDONDA VYA TUMBO:-

# MAUMIVU MAKALI au KIUNGULIA maeneo ya CHEMBE MOYO (epigastic pains).

# MAUMIVU juu KIDOGO ya TUMBO mara nyingi HUENDANA na MUDA wa KULA CHAKULA . MTU mwenye VIDONDA kwenye TUMBO (gastric ulcers) hupata MAUMIVU MAKALI sana kipindi ANAPOKULA au mara tu BAADA ya KUMALIZA KULA wakati aliye na VIDONDA kwenye SEHEMU ya kwanza ya UTUMBO MDOGO (duodenal ulcers) hupata MAUMIVU MAKALI anapokuwa na NJAA na hupata NAFUU pindi ANAPOKULA .

(i) KUVIMBIWA au TUMBO kujaa GESI. HALI hii pia yaweza KUENDANA na KUBEUA au KUJAMBA mara kwa mara.

(ii) KUCHEUA na KUONGEZEKA kwa MATE yanayoshuka TUMBONI baada ya KUCHEUA .

(iii) KICHEFUCHEFU na KUTAPIKA

(iii) Kupoteza HAMU ya KULA na KUPUNGUA UZITO

(iv) Kutapika DAMU

(v) Kupata HAJA KUBWA cha RANGI NYEUSI au KAHAWIA chenye HARUFU MBAYA SANA.

HII humaanisha MGONJWA anapata HAJA KUBWA au CHOO kilichochanganyika na DAMU kwa mbali

UWEPI wa DALILI kama KIUNGULIA cha MUDA MREFU, KUCHEUA na KUTAPIKA baada ya KULA na HISTORIA ya KUTUMIA DAWA za KUPUNGUZA MAUMIVU (NSAIDs) kwa MUDA MREFU bila KUFUATA ushauri wa DAKTARI ni ISHARA tosha ya kumfanya MGONJWA kumuona DAKTARI kumpima na kumfanyia UCHUNGUZI ili KUJIRIDHISHA kuwa HANA TATIZO la VIDONDA vya TUMBO .

KAMA UNAZO DALILI HIZO USISITE KUFIKA HOSPITALI [KITUO CHA AFYA] KILICHO KARIBU NAWE KWA MSAADA ZAIDI

FAIDA ZA KUNYWA MAJI ASUBUHI(KABLA YA KIFUNGUA KINYWA)

KUNYWA MAJI KABLA YA KIFUNGUA KINYWA ASUBUHI -YANATIBU MARADHI MENGI.

Kiafya binadamu utunatakiwa kunywa glasi 7-8 kwa siku ni muhimu kwa afya zetu.Watu wengi hawajui kama kunywa maji asubuhi pale uamkapo ni kinga moja kubwa mwilini.image.Tiba hii huu inaitwa Ayurvedic treatment inafaida nyingi ya kukuepusha na maradhi.

sehemu kubwa ya mwili wa mwanadamu ni  maji  kwa asilimia 70% ambayo ndio inasaidia mwili Wake ufanye kazi kiufasaha,wakati cell ya ubongo wa binadamu una maji kwa asilimia 85%,damu inakiasi cha maji kwa asilimia 82%,muscles inatumia maji asilimia 75% wakati mifupa inamaji asilimia 25%.Mpaka hapo inaonyesha maji ni muhimu sana kwa mwili wa binadamu .

Umuhimu wa kunywa maji asubuhi kabla ujaingiza chochote tumboni.

Unatakiwa kunywa maji pale uamkapo ukiwa ujakula chochote,itakusaidia kusafisha mfumo wako wa mmeng’enyo (internal system) kwa urahisi. Itatoa uchafu  na sumu kwenye Colon ulizozila kupitia  vyakula tofauti tofauti .Faida nyinginezo ni

Kungarisha ngozi.

Renew cells.

Kusafishwa kwa colon na kufanya unyonywaji wa virutubisho kuwa rahisi.

Inatibu magongwa na maradhi .Unywaji wa maji asubuhi pale uamkapo inakusaidia kutibu maradhi kama matatizo ya ini,TB,kuhara,cancer,matatizo ya macho,maumivu ya kichwa,stress,uti wa mgongo.

Hupunguza uzito.

Kunywa maji pale uamkapo liters 1.5 ( glas 5-6),epuka kunywa kinywaji kingine chochote au kula kabla na baaya ya kunywa maji ,usinywe pombe baada ya siku 2 ndio uendelee na kunywa maji yako kila asubuhi .Mwanzo itakuwa ngumu sana kunywa glas 6 kwa pamoja unachotakiwa kunywa 4 pumzika kidogo kunywa izo 2 zilizobakia.Utafanya hivyo baada ya siku 3 utumbo utaozoea na utakunywa kwa urahisi.

Hii water therapy ilizinduliwa na wajapan baada ya kuifanyia utafiti wa mda mrefu na kubaini inatibu maradhi  mengi iwapo mgonjwa atafatisha sheria zake kama

Uamkapo kunywa maji moja kwa moja bila kupiga mswaki au kula chochote.

Piga mswaki na usile chochote sababu yale maji yanahitaji kutoa uchafu kabla ujaweka chakula au  kinywa tumboni.

Bada ya dakika 45 unaweza kunywa breakfast.

Baada ya breakfast usile kitu chochote baada ya masaa 2.

       Kipimo cha maji kulingana na maradhi.

Constipation-wenye matatizo ya kuapa haya kubwa watafata hii kinga ya maji  kwa siku 10

TB-siku 90

Kisukari siku 30

Gastric -kuwa na gesi nyingi tumboni -siku 10

Pressure (high blood pressure) siku 30.

Unatakiwa kunywa maji kwa wingi haswa wale wanaoishi sehemu za joto .Epuka kuwa dehydrated kwani utakaribisha maradhi kwa urahisi...Endelea kuwa nami kwa makala nyingi za afya

Wednesday, June 14, 2017

FAIDA TISA(9) ZA KULA NANASI

FAIDA ZA KULA NANASI KWA AFYA YAKO

Hapa tuta angalia faida kuu za kula nanasi na Wote tunajua kuwa kula matunda mazuri inasaidia mwili kupata vitamin na madini mbalimbali na kuwa mtu mwenye afya njema, na sasa tunda la nanasi ni tunda moja wapo ambalo ni muhimu sana hasa katika msimu huu wa mananasi.

1: Mmeng’enyo wa chakula.

Nanasi linasaidia kurahisisha mmeng’enyo wa chakula kwa kiasi kikubwa sana. Hii inatokana na kuwa nanasi linatoa aina protini katika mwili wako ambayo inarahisisha kazi hii ya kumeng’enya chakula.

2: Nanasi Lina Vitamin na Madini

Tunda la nanasi limejaa madini na protini nyingi ambazo zinafaa kwa mwili wako. Nanasi lina vitamin A Vitamini C calcium, fiber na pia potassium.

3: Kuzuia Kikohozi na Baridi.

Tangu nanasi lina utajiri wa vitamin C linaweza kupigana na virusi amabavyo vinaweza kusababisha kikohozi na ubaridi. Hata kama umeshakuwa na kikohozi nanasi kwa kiasi flan linaweza kukusaidia kupunguza makali. Tunda hili lina madini ya Bromelain ambayo yanauwezo wa kudhoofisha virusi vya kikohozi. Wakati unaumwa kula tunda la nanasi hata wakati unakuwa kwenye dozi ya dawa ambazo umepewa na daktari linaweza kukusaidia sana kuharakisha kupona haraka.

4: Kuimarisha Mifupa.

Je unahisi mifupa yako sio imara? Basi anza kula nanasi. Nanasi pia lina uwezo wa kuimarisha mifupa nakuifanya kuwa yenye nguvu. Hii ni kwa sababu nanasi lina madini ya manganese ambayo mwili wako unahitaji madini haya ili kwa ajili ya kuimarisha mifupa yako. Tena kama ukinywa kikombe kimoja tu cha juice ya nanasi unakua umeongeza asilimia 73% ya madini ya manganese ambayo ni hata zaidi ya mwili unavyoihitaji kitu ambacho ni kizuri kwa afya ya mifupa ya mwili wako. Unakua na mifupa iliyokomaa.

5: Huimarisha Meno yako.

Watu kila mara huwa wanajali sana meno yao, na mara nyingine huwa wanashindwa kuyapa kipaumbele kwa saaana. Kama una matatizo ya meno basi unashauriwa kula nanasi kwa sababu nanasi linasaidia kuimarisha magego ambayo yanashikiria meno. Kula tunda la nanasi linakufanya kuimarisha magego yanayoshikiria meno na pia meno yenyewe yanaimarika.

6: Huzuia Ugonjwa wa Asthma.

Ukila nanasi unajiweka katika hali nzuri ya kuto pata ugonjwa wa asthma. Watu wanaokula nanasi wanakua katika hali nzuri kwa sababu nanasi lina vitamin aina ya Beta Carotene ambayo linausaidia mwili kukabiliana na magonjwa mbali mbali ikiwemo asthma.

7: Blood Pressure.
Unapokula nanasi unaongeza potassium na pia kula matunda mengine yenye madini ya potassium yanaweza kukusaidia kupunguza uwezekano wa kupata blood pressure.

8. Kansa.
Kama kawaida nanasi lina utajili mkubwa wa vitamin C. Hii vitamin C inauwezo wa kuzuia virusi ambavyo vinaweza kukusababishia magonjwa mabali mabli ya kansa.

9. Huimarisha Afya ya Moyo.

Utajiri wa madini ya fiber, potassium na vitamin C ni mojawapo ya faida za tunda hili ambazo pia zina uwezo wa kuimarisha afya ya moyo wako na kuzuia maradhi yanayoweza kuuadhiri moyo wako.

Sasa jamani tuanze kula tunda la nanasi ili tuweze kufaidi madini ya na vitamin zilizojaa katika tunda hili. ili kuepuka magonjwa ya baadaee. 

Endelea ku subscribe blog hii kwa Habari zaidi. >>>>>>>>

Featured Post

FAIZA ZA KULA PAPAI

 _*Siri usioijua kuhusu utajiri wa tunda la papai katika kukulinda na magonjwa hatarishi kutokana na faida zake lukuki*_  Hizi ndizo FAIDA 1...