Tuesday, November 12, 2024

AINA ZA KISUKARI

 AINA ZA KISUKARI


Kuna aina kuu mbili za kisukari

1. Kisukari kinachotegemea insulin(type 1 diabete)

2. Kisukari kisichotegemea insulin(type 2 diabete)


1. Kisukari kinachotegemea insulin:

Hii ni aina ya ugonjwa wa kisukari ambapo mwili hushindwa kutengeneza au hua una uhaba wa kichocheo aina ya insulin ambacho huwezesha mwili kutumia sukari. Lakini pia aina hii ya ugonjwa wa kisukari huchangiwa na ukosefu/upungufu wa madini aina ya potassiam.

Aina hii ya kisukari inaweza kudhibitiwa kwa utumiaji wa sindano za insulin pamoja na ulaji wa vyakula vyenye kiwango kikubwa cha potassiam.


2. Kisukari kisichotegemea insulin:

Hii ni aina ya ugonjwa wa kisukari ambapo kongosho huzalisha kichocheo aina ya insulin, lakini kichocheo hicho, hushindwa kuruhusu milango ya chembe hai za mwili(seli) kufunguka na kuruhusu sukari kuingia ili kwenda kuzalisha nguvu. Hali hii hutokana na athari mbali mbali za mazingira na ulaji mbovu.

Aina hii ya kisukari inaweza kudhibitiwa kwa kurekebisha aina za ulaji.


DALILI ZA UGONJWA WA KISUKARI

Zifuatazo ni miongoni mwa dalili za ugonjwa wa kisukari kiujumla.

- Kuhisi kiu sana/kunywa maji mengi.

- Kukojoa mara kwa mara.

- Kuhisi njaa mara kwa mara.

- Uchovu bila ya kufanya kazi.

- Kukosa nguvu.

- Kupungua uzito kusiko kwa kawaida.

- Kizunguzungu.

- Wanawake kuwashwa ukeni.

- Kupungua kwa nuru ya macho.

- Kupungua kwa nguvu za kiume.

- Ganzi sehemu za miguu na vidole.

- Kufanya majipu mwilini.


MADHARA YA UGONJWA WA KISUKARI

Ugonjwa wa kisukari hupelekea athari mbali mbali zikiwemo:-

- Kupungua kwa nuru ya macho na hata upofu.

- Figo hushindwa kufanya kazi zake vizuri.

- Kutopona kwa vidonda hasa sehemu za miguu na hata kukatwa kidole na mguu.

- Maradhi ya moyo.

- Kupoteza kwa hisia kwa mikono na miguu.

- Kupata kiharusi.

- Kupoteza nguvu za kiume.


ZINGATIO.

Ugonjwa wa kisukari unakingika na kudhibitika ikiwa tu, tutabadili mfumo mzima wa ulaji/virutubisho lishe na kubadili mienendo ya maisha.


Kwa makala za afya Usiache kufatilia page yetu 


Tuandikie ktk email yetu afyamwili@gmail.com 


Au waweza kutupata Whatsapp 0628873628


Karibuni

Featured Post

FAIZA ZA KULA PAPAI

 _*Siri usioijua kuhusu utajiri wa tunda la papai katika kukulinda na magonjwa hatarishi kutokana na faida zake lukuki*_  Hizi ndizo FAIDA 1...