Tuesday, November 12, 2024

AINA ZA KISUKARI

 AINA ZA KISUKARI


Kuna aina kuu mbili za kisukari

1. Kisukari kinachotegemea insulin(type 1 diabete)

2. Kisukari kisichotegemea insulin(type 2 diabete)


1. Kisukari kinachotegemea insulin:

Hii ni aina ya ugonjwa wa kisukari ambapo mwili hushindwa kutengeneza au hua una uhaba wa kichocheo aina ya insulin ambacho huwezesha mwili kutumia sukari. Lakini pia aina hii ya ugonjwa wa kisukari huchangiwa na ukosefu/upungufu wa madini aina ya potassiam.

Aina hii ya kisukari inaweza kudhibitiwa kwa utumiaji wa sindano za insulin pamoja na ulaji wa vyakula vyenye kiwango kikubwa cha potassiam.


2. Kisukari kisichotegemea insulin:

Hii ni aina ya ugonjwa wa kisukari ambapo kongosho huzalisha kichocheo aina ya insulin, lakini kichocheo hicho, hushindwa kuruhusu milango ya chembe hai za mwili(seli) kufunguka na kuruhusu sukari kuingia ili kwenda kuzalisha nguvu. Hali hii hutokana na athari mbali mbali za mazingira na ulaji mbovu.

Aina hii ya kisukari inaweza kudhibitiwa kwa kurekebisha aina za ulaji.


DALILI ZA UGONJWA WA KISUKARI

Zifuatazo ni miongoni mwa dalili za ugonjwa wa kisukari kiujumla.

- Kuhisi kiu sana/kunywa maji mengi.

- Kukojoa mara kwa mara.

- Kuhisi njaa mara kwa mara.

- Uchovu bila ya kufanya kazi.

- Kukosa nguvu.

- Kupungua uzito kusiko kwa kawaida.

- Kizunguzungu.

- Wanawake kuwashwa ukeni.

- Kupungua kwa nuru ya macho.

- Kupungua kwa nguvu za kiume.

- Ganzi sehemu za miguu na vidole.

- Kufanya majipu mwilini.


MADHARA YA UGONJWA WA KISUKARI

Ugonjwa wa kisukari hupelekea athari mbali mbali zikiwemo:-

- Kupungua kwa nuru ya macho na hata upofu.

- Figo hushindwa kufanya kazi zake vizuri.

- Kutopona kwa vidonda hasa sehemu za miguu na hata kukatwa kidole na mguu.

- Maradhi ya moyo.

- Kupoteza kwa hisia kwa mikono na miguu.

- Kupata kiharusi.

- Kupoteza nguvu za kiume.


ZINGATIO.

Ugonjwa wa kisukari unakingika na kudhibitika ikiwa tu, tutabadili mfumo mzima wa ulaji/virutubisho lishe na kubadili mienendo ya maisha.


Kwa makala za afya Usiache kufatilia page yetu 


Tuandikie ktk email yetu afyamwili@gmail.com 


Au waweza kutupata Whatsapp 0628873628


Karibuni

Saturday, October 26, 2024

FAIZA ZA KULA PAPAI


 _*Siri usioijua kuhusu utajiri wa tunda la papai katika kukulinda na magonjwa hatarishi kutokana na faida zake lukuki*_


 Hizi ndizo FAIDA 10 za kiafya za kula papai

1️⃣ Papai ni katika matunda yanayojenga afya sana kwenye mwili wa binadamu. Papai lina *vitamin C na vitamini A* kwa wingi pia kuna *potassium na folate.* Pia tafiti zinaonesha kuwa *antioxidant aina ya lycopene* iliyomo kwenye papai *husaidia katika kuzuia kupata saratani.* 


2. Tunda hili pia lina *vitamin B, vitamin E na vitamin K.* Pia lina *madini ya calsium (kashiam) potassium, mgnessium na copper.* Pia punje za papai ni *dawa kwa baadhi ya matatizo ya ini na figo.* Pia kwenye papai kuna *protelytic enzymes hii husaidia katika kuuwa bakteria na minyoo pamoja na wadudu wengine hatari ndani ya tumbo (mfumo wa kumeng’enya chakula).* 


3️⃣ Papai linatambulika kwa kuwa na *uwezo wa kuulinda mwili na maradhi ya uzee kama macho, misuli na kuzeeka kwa haraka.* Ndani ya papai kuna *Zeaxanthin hii ni anti oxidant ambayo inakazi ya kuchuja miale hatari ya jua.* Pa inaaminika kuwa *antioxidant hizi husaidia katika afya ya macho na husaidia katika kudhibiti kudhoofu kwa misuli.* 


4️⃣ Vilevile papai huaminika kusaidia kupunguza *hatari ya kuwa na ugonjwa wa pumu.* Hupunguza hatari ya kuugua pumu. Ndani ya papai kuna virutubisho vingi, lakini uwepo wa *beta-carotene ndani ya papai husaidia kwa wagonjwa wenye pumu.* 


5️⃣Ulaji wa antioxidanti zilizopo kwenye papai mfano *beta-carotene* *husaidia katika kupunguza athari za kupata maradhi ya saratani kwa vijana* . Ulaji wa tunda hili husaidia katika *kudhibiti upatikanaji wa saratani ya kwenye via vya uzazi hasa saratani ya korodani.* 

6. Pia papa Lina kiwango kikubwa Cha fibres (nyuzi na kambakamba) zinazosaidia kurahisisha mmeng'enyo wa chakula na kufanya mtumiaji kutopata choo kigumu (Constipation)

 *Hitimisho:* 

Nimalizie kwa kusema kuwa matunda ni dawa. Ni vyema kujitahidi kula matunda na mboga za majani mara kwa mara. Pia viungio vya mboga kama vitunguu, tangawizi, bamia na karoti viungio hivi ni muhimu sana.

Featured Post

FAIZA ZA KULA PAPAI

 _*Siri usioijua kuhusu utajiri wa tunda la papai katika kukulinda na magonjwa hatarishi kutokana na faida zake lukuki*_  Hizi ndizo FAIDA 1...